TMDA yapiga marufuku dawa yenye kiambata cha levamisole

TMDA yapiga marufuku dawa yenye kiambata cha levamisole

Baba mtakatifu91

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2026
Posts
3,674
Reaction score
7,633
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA
MAMLAKA YA DAWA NA VIFAA TIBA (TMDA)
ISO 9001: 2015 IMETHIBITISHWA
TAARIFA KWA UMMA
23 Juni, 2026

KUPIGWA MARUFUKU KWA MATUMIZI YA DAWA ZENYE KIAMBATA HAI CHENYE JINA LEVAMISOLE

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) inafanya kazi ya ufuatiliaji wa bidhaa za tiba zilizosajiliwa nchini kwa kupokea na kupitia ripoti za kiusalama kutoka ndani na nje ya nchi ambapo taarifa husika hukusanywa, kuchambuliwa na kisha kuwasilishwa katika Kamati ya Kitaalamu ya Usalama wa Dawa (VTC) kwa ajili ya tathmini na ushauri.

Kupitia utaratibu huo, TMDA imebaini kuwa dawa za binadamu zenye kiambata hai cha Levamisole, zinazotumika kutibu maambukizi ya minyoo, zinaweza kusababisha ugonjwa katika mfumo wa fahamu unaojulikana kitaalamu kama Leukoencephalopathy. Usipotibiwa mapema, ugonjwa huu huleta madhara makubwa ya kiafya, ikiwa ni pamoja na vifo kwa watumiaji.

Kutokana na muktadha huo, TMDA inapenda kuujulisha umma kuwa dawa zote zenye kiambata hai cha Levamisole zimepigwa marufuku katika soko la Tanzania. Hivyo, dawa hizo hazitaruhusiwa kutengenezwa, kuingizwa, kusambazwa wala kuuzwa nchini kwa matumizi ya binadamu.

Vilevile, waagizaji na wasambazaji wote wa dawa hizo wanaelekezwa kusitisha shughuli husika mara moja kuanzia tarehe ya tangazo hili, na kuziondoa sokoni.
IMG-20260627-WA0004.jpg

HABARI: TMDA ZUIA DAWA ZENYE KIAMBATA CHA LEVAMISOLE.
 
Ifike mahali viwekwe vigezo ili uwe waziri wa sekta fulani lazima uwe umesomea hiyo kada. Inakuwaje dawa imeingizwa kitambo halafu leo ndo wanastuka
 
Ifike mahali viwekwe vigezo ili uwe waziri wa sekta fulani lazima uwe umesomea hiyo kada. Inakuwaje dawa imeingizwa kitambo halafu leo ndo wanastuka

Pamoja na kwamba sijaiona taarifa husika kwenye site ya TMDA, hili ni jambo la kawaida kwenye suala la Uvumbuzi na Uendelezaji wa dawa, vifaatiba na viambata duniani kote.

Dawa inapokidhi vigezo na taratibu za kutumika kwa binadamu, huruhusiwa kwa kuendelea kufanyiwa kitu kinaitwa Post Market Survaillance/uangalizi wa dawa husika ikiwa sokoni.

Ikionyesha kuwa na madhara zaidi ya kiasi kilichotarajiwa hapo mwanzo kulingana na utafiti, na hii inaweza kutokana na matumizi yake kwa watu wengi zaidi ya waliotumika kwenye utafiti, basi huamriwa kuondolewa sokoni/Recall.
 
Back
Top Bottom