Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Mi nafikiria mtu anapoona ana mauvimbe, haraka saana akimbilie hospitali.

Benign kuja kuwa Malignant inawezekana kabisa.

Hivi Mkuu kama una mauvimbe katika matiti, mfano lilianza moja kisha likaja la pili. Je, nini kinapelekea kuwa hivi? Na inaweza ikawa ni dalili ya Malignant Neopalism?

Sometimez linakuwa na maumivu makali sana ila pia kuna muda maumivu yanakata.
Ndg kwa uandishi wako unaonekana ni mtaalamu wa fani ya Afya.
Nakushauri Kama Kuna mass na pia ni painful sio dalili nzuri.
Je Kuna discharge?
Je kuna ulcer
Je kuna lymphnode enlargement kwapani,au shingoni?

Ukiwa na moja au zaidi ya mambo hayo niliyouliza fanya hima kwenda Hospitali kwa uchunguzi zaidi.
 
Suluhisho ya tinnitus ni nini!?
Suruhisho ni kujua tatizo la why tinnitus is happening and then you address the cause if possible?

Kwa asili tinnitus sio ugonjwa by itself Ila inaashiria tatizo la kiafya hasa kwenye sehemu ya ndani ya sikio( inner ear sensory hair damage)

Tatizo hili linaweza kuwa la muda au la kudumu Kutokana na sababu inayopeleke kupatwa na makelele sikioni.
Ziko sababu nyingi zikiwemo

Kuzeeka
Kuishi au kufanya kazi maeneo yenye makele mengi, kama viwandani, Kumbi za disco, sokoni etc
Kuongezeka kwa wax sikioni
Magonjwa ya mafua na sikio ( sinus and otitis media infection)
Wakati mwingine tinnitus uletwa na side effects za madawa eg quinine-based medication, diuretics, antidepressant etc

Ukijua kinachosababisha itakusaidia kujua nini Cha kufanya.
 
Kujichua siyo issue...eleza umeathirikaje

Je haudindishi
Je unawahi fika kileleni
Je huna hamu ya tendo
Je je uwezi endelea zaid ya round moja?
Be specific tunone namna ya kukusaidia
nadindisha
Kuwah ndio nawahi
Hamu ya tendo hamna
Naweza enda hata round nne na zaid
Tatizo kubwa ni kuwah kufika na hamu ya tendo. Kuwah haswaaa ndio shida. Yaaan few seconds especially round one
 
Nashukuru sana dr kwa ufafanuzi mzuri na wa kitaalam, nina mwenza ambae mwaka jana alipata hyo issue,sasa tukataman kujua sababu, ili tujiandae endapo ata conceive tena, pia sorry ultrasound inaweza ikaonyesha kiumbe kwa mimba ya mwez mmoja?
 
Mimi nina shida moja,upande wa kushoto wa tumbo kwenye mbavu hua wkt flan naona panadunda,tena kwa spidi kidgo kuzid ata moyo,mara nying hua inantokes nikiwa nanjaa na kuna kipindi hua inapotea


Nna siku kama mbili mshipa wa kichwan,huu ambao uko juu ya sikio ambao nadhan mtu akikasitika hua unavimba,nausikia unadunda(sina neno lingine lakutumia) na hata nikiugusa nauona unavibrate. je jidalili ya ugonjwa au ni hali yakawaida?!?
 
Ndg hongera kwa kutosumbuliwa na magonjwa mbalimbali. Kifupi wewe ni miongoni mwa watu waliobarikiwa na Mungu kuwa na afya njema.

Kwa ufupi hali ya afya ya mtu ni matokeo ya factor mbalimbali zikiwemo:

Vinasaba vya mtu-genetic factors
Lishe
Mfumo wa Kinga (Body immune system)
Mfumo mzuri wa maisha (good health life style)
Mazingira Safi na yasiyo hatarishi
Chanjo
Na mwisho mfumo wa huduma za afya za eneo husika na urahisi wa upatikanaji wake.

Factor hizo zikiwa okay...watu huweza kuishi maisha bila kusumbuliwa na magonjwa.

Hivyo nakushauri keep praying for good health na usisahau ku-maintain mfumo bora wa maisha.

Mfumo wa huduma za afya zinahusikaje na kuto kuumwa
 
Kuwa na mafua yasio isha kipindi cha baridi au mvua na chafya zisizoisha pamoja na muwasho wa kwenye macho ni nin hasa sababu
 
Ndg please kuwa serious na afya ya dogo.
Ni vigumu mm kukupa jibu kipi ni kifaa kizuri coz Sina specifications ya vifaa hivyo kama vinafanana au ni Orginal Vs fake -one.

Je hao waliokuambia utapata kifaa hicho kwa tsh 80,000 ni madaktari au wataalamu wa ENT ?

Unaweza kimbilia cheap Ila kisiwe msaada kwa kijana

Cha mhimu waamini madaktari wa Mhimbili, jichange nenda kawaone wataalamu.

Naelewa changamoto ya kifedha Ila linganisha hiyo laki 370,000 Na usumbufu na kero anazopitia kijana.

Please jipangeni muwahi hospitali
Nashukuru sana kwa ushauri mkuu
 
Mkuu umenichekesha ila usijali

Tatizo la utofauti wa sauti ni la kimaumbile tu kama vile Kuna watu wafupi na warefu, weusi na weupe, wenye sauti ya Kwanza vs sauti ya 4 etc.

Tofauti zetu ziko kwenye organ mbili hizi , larnyx na vocal cords na mfumo wa hewa kwenye mapafu. Msukumo wa hewa kwenye koromeo(larynx) na mwitiko (vibration) wa kiwambo Cha sauti (vocal cord) ndo uleta tofauti hizo.

Wakati sababu kubwa ikiwa ni ya kimaumbile , kwenye organ zinazozalisha sauti, mambo mengine ambayo upelekea utofauti wa sauti ni pamoja na
Umri
Matumizi ya sigara na madawa ya kulevya
Personality ya mtu, Kuna watu huzungumza kwa nguvu kuliko wengine
Tamaduni za watu, kuna tamaduni zinamtaka mdada aongee kwa sauti ya chini na mwanaume akaze sauti

Mazingira ya makuzi. Kuna uhusiano wa mtu kukulia mazingira ya watu waongeaji sana na yenye makele na kuwa na sauti kubwa kuliko mtu aliyekua kwenye mazingira ya utulivu sana.
Sawa mkuu nashukuru nimekuelewa.
 
Swali langu lingine ni kuwa nimekuwa nikisumbuliwa sana na tatizo la kichwa kwa muda mrefu sana takribani miaka 3 huwa kinanigonga sana sehemu ya nyusi(eyebrows) kuna raia walinambia ni kipanda uso nikampata mbabu mmoja hivi akasema anaweza kunitibu nikaenda akanichanja chanja na kunipaka dawa anazozijua yeye kikatulia kwa muda mafupi kama mwiezi 2 hivi kikaanza tena mikaamua kwenda hospitali wakanifanyia uchunguzi wa vipimo vya macho Wakasema sina tatizo la macho.... Kiukweli hali hii inanitesa sana na sijui nifanyeje kikianza inanibidi nilale Weee kama masaa 2_3 ndio kitulie na sana sana muda wa mchana ndio shida zaidi huwa natamani hata kusinge kuwa na mchana coz asubuhi huwa inakuwa fresh tu.naomba kujua nifanyeje nini ili niondokane na haya mateso.
 
Nitajibu maswali yote ndg zangu
Tuvumiliane kidogo ratiba zimekua tight

Wale wanaokuja whasapp pia uvumilivu uendelee kuwepo

Nawapenda watanzania.

Muwe na weekend njema
 
Mawasiliano plz
Ziko sababu nyingi zinazosababisha ganzi mwilini. Ila upatwapo ganzi tambua mfumo wa never hasa Central au peripheral never umepata shida.

Possible causes ni Kama:
Magonjwa sugu Kama kisukari, Ukimwi na kansa

Kuumia ubongo au uti wa mgongo au magonjwa yanayoasili maeneo hayo ikiwemo stroke

Ukosefu wa vitamin has B-12

Unywaji wa pombe kupitiliza

magonjwa ya zinaaa Kama sphilis

Wakati mwingine ganzi uletwa na side effects za madawa Kama baadhi madawa ya kufubaza VVU

Matibabu utokana na tatizo la msingi ila hata hivyo Kuna dawa zinasaidia wengi kuondoa ganzi.

Kwa matibabu tuwasiliane
 
Asante kwa swali zuri.

Nitajibu kwa upana kidogo ili swali lako liwasaidie na wengine wenye swali Kama hili.

Kitaalamu magroup ya damu yaweza kupangwa kwa namna mbalimbali, hata hivyo mfumo wa ABO na Rhesus (Rh) blood grouping ndo unatumiwa sana. Mfumo huu unatupa magroup ya damu kama
Group A
Group B
Group AB
Group O

Magroup haya ya damu hutokana na asili la vinasaba vya mtu ambavyo uvirithi toka kwa wazazi wake.

Jamii mbalimbali zinatofautiana kwa idadi ya asilimia ya watu wenye makundi mbalimbali ya damu. Mfano American watu wenye group O ni wengi zaidi. Denimark ni A na India ni B .

Nikijielekeza kwenye swali la msingi Kuhusu usiano wa kundi la damu na kinga juu ya maradhi . Nianze kwa kusema dhana hiyo ipo Kutokana na Tafiti zilizowahi fanyika katika nchi nyingi za ulaya na Amerika.

Kwa mfano kuna utafiti uliowahi kufanyika Marekani ulionyesha watu wenye group O walikua na kinga dhidi ya ugonjwa wa syphilis(ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa ya zinaa).

Hata hivyo matokeo hayo sio universal na watafiti wanadhani findings hizo zilitokana na sehemu kubwa ya jamii hiyo iliwahi kushambuliwa na ugonjwa huo siku za nyuma. Na kwa kuzingatia kuwa population ya America idadi kubwa ni watu wenye Group O ,matokeo hayo hayakushangaza watafiti.

Ziko tafiti zingine ziliwahi onyesha watu wenye group AB walikua na kinga juu ya ugonjwa wa kipindupindu zaidi ya wale wenye group A and B.

Nikihitimisha hoja ya swali lako la msingi. Si kweli katika jamii zote watu wenye group O wana Kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa. Coz magonjwa ya zinaa yako mengi na hakuna uhusiano wa moja kwa moja na uwepo wa Kinga zidhi ya magonjwa hayo na mtu kuwa na damu kundi O.
Mm nina O naugua kwa soeed ya 4g hasa amoeba haiishi
 
Back
Top Bottom