Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Asante Dr kwa huduma yako nzuri na ushauri unaotupatia hapa,ubarikiwe sana.

Kwenye vipimo vya HIV hua wanacho cha kwanza na cha pili kwa ajili ya kuthibitisha tatizo,imetokea kipimo cha kwanza kikaonyesha mgonjwa anatatizo cha pili kikaonyesha hana tatizo,huu.mkanganyiko kitaalamu hua limekaaje?
Barikiwa.
 
Pole ndg

Sina uhakika ila nitafanya mawasiliano kuthibitosha uwepo wa huduma hiyo.

Ila Kama upo karibu Basi fika Hospitalini pale ukahudumiwe.
Nipo hatua kidogo, kwani CCBRT na MUHIMBILI ni wapi watakuwa na huduma njema zaidi ktk hili?
 
Nina miaka 5 bila kuugua hata homa wala malaria au tumbo! Na siombi kuugua ila napenda kufahamu siri ya hii hali kwenye hiyo field yako ya udaktari?
Watu wengi ambao husema huwa siugui, huwa wanakuja kuugua vibaya mno.

Sijui haya maneno huwa yanaenda wapi na kumrudia mhusika. Siku si nyingi utaugua aisee.

Nilichojifunza, kama una afya njema, kaa kimya na umshukuru Mungu kwa afya.
 
habarir
tangu nibalehe(miaka mingi ilopita) mpaka leo chunusi(usoni) na vipele pele (kifuani) haziishi

tena nikila vtu vyenye mafuta kama chips,karanga na maharage yaan ndo kabisa sitazamiki usoni ,,,,,,
tatzo laweza kuwa nn et
 
Mkuu hivi kuwa na sauti nzito kupita kiasi inasababishwa nanini.kama ukipita nje ukanisikia sauti yangu unaeza sema nipo kwenye .....
 
Naomba kujua sababu za vivimbe katika matumbo ya kinamama... Fibroids. Nini Tiba yake mbadala wa upasuaji kwa sababu huwa zinaota Tena baada ya miaka kadhaa. Asante
Pole kwa kuchelewa kujibu.
Kitaalamu Nini kinasababisha fibroids haijulikani, ila ushahidi wa kitafiti unaonyesha mambo mbalimbali yanaweza kuchangia risk ya kupata fibroids ikiwemo:
Genetic factor au vinasaba vya mtu
Wingi wa hormone ya estrogen and progesterone
Ongezeko la growth hormone
Ukosefu wa vitamin D au
Stress
Uzito mkubwa
Pombe etc.

Tiba halisi Ni upasuaji ili kuviondoa vivimbe kwenye mfuko wa uzazi. Ila mbala wake japo sio effective unashauriwa kubadiri mfumo wa maisha kwa kuzingatia yafuatayo

Ulaji mwingi wa mboga za majani na matunda
Cut off vyakula vya mafuta na nyama
Punguza uzito na kitambi
Kama una Magonjwa ya sukari na BP hakikisha unatibiwa
Acha pombe na sigara ikiwa unatumia
Kula vyakula vyenye vit D au vodonge
Pia Kuna dawa za kubalance hormone ya oestrogen ambayo ndo kichocheo kikubwa Cha fibroids.

Karibu kwa maswali specific
 
hivi hydrocele inaweza tibika bila operation?
Upasuaji ndo tiba halisi kwa tatizo la hydrocele. Kama inaambatana na maumivu unaweza tumia dawa za maumivu.

Acha kuchelewa, fika Hospitali iliyokaribu na wewe wataalamu wakusaidie ili kuhepuka complications na usumbufu.
 
Upasuaji ndo tiba halisi kwa tatizo la hydrocele. Kama inaambatana na maumivu unaweza tumia dawa za maumivu.

Acha kuchelewa, fika Hospitali iliyokaribu na wewe wataalamu wakusaidie ili kuhepuka complications na usumbufu.
Post no 80 hujaijibu mkuu.
 
Mimi natokwa sana na jasho kwapani kiasi hadi nikivaa nguo nyeusi inaacha alama ya chumvi, kwakweli nakosa raha kabisa, msaada wako tafadhali
Pole ndg
Tatizo la kutokwa jasho lisilo la kawaida linawasumbua wengi. Mara nyingine humfanya mtu kupoteza ujasiri na unazifu wake coz y
jasho na harufu itokanayo na tatizo hili.

Nianze kwa kusema hivi, kutokwa jasho jingi Mara nyingi huwa ni harmless, ila ikitokea kuwa unatokwa jasho hadi inakua kero hapo nilazima kuchukuawa hatua za kukabiliana na tatizo hilo.

Kuna utokwaji wa jasho mwili mzima, kiasi kwamba mtu hata akifanya kazi nyepesi tu jasho linakua jingi na kumsumbua mhusika.

Ila Kuna aina nyingine jasho linakua maeneo maalumu tu Kama kwenye kwapa, shingoni, usoni , miongoni, au sehemu za siri na kwenye mapaja.

Kutokwa jasho kunaweza sababishwa na mambo mengi Kama stress and fear, homa, ujauzito, kitambi, ukomo wa hedhi yaani menopause, au mazoezi. Mara nyingi mambo haya yakiwa addressed maisha uendelea.

Sababu zingine zinafanya tatizo kuwa endelevu na pengine kuleta kero kubwa kwa mtu. Mfano watu wenye maradhi kama hyperthyroidism, parkinsonism, rheumatoid arthritis, Gout, au lymphoma. Watu wenye matatizo haya jasho liwatokalo mara nyingi huwa ni mwili mzima na uweza ambatana na homa .

Kitaalamu tunaweza kugawa tatizo la kutoka na jasho jingi Kama ifuatavyo.

1: primarily hyperhidrosis: ni pale sababu yake haitambulikani, watafiti wanazani tatizo hilo uanza toka utotoni, na wengi huusianisha na namana sweat glands-(tezi za jasho) zilivyo sensitive na uzaniwa Kuna elements za vinasaba.

2: Secondary hyperhidrosis: Ni pale tatizo la kutokwa jasho jingi linakua na kisababishi Kama maladhi ya mwili (Kama nilivyo yaorodhesha hapo juu) au mabadiriko ya kihomoni.

Kwa msingi huo niruhusu nijibu swali lako la msingi. Kutokwa na jasho jingi hasa kwapani inaweza kuwa linaangukia kwenye aina ya kwanza primary hyperhidrosis.

Ikiwa jasho linakua metabolize na bacteria, tatizo hili uambatana na harufu kali inayogeuka kero na kuondoa utanashati wa mtu.

Tiba yake Mara nyingi ni supportive kwa maana ya hatua za kupunguza jasho na kudhibiti harufu Kama:

Kuhakikisha mwili unakua safi
Unywaji wa maji mengi
Kuhepuka animal products foods
Matumizi ya antiperspirants
Matumizi ya deodorant
Unaweza tumia umeme hafifu kublock tezi za jasho -Iontophoresis
Matumizi ya botulinum toxins
Matumizi ya anticholinergic drugs
Na Kama njia hizo juu zitafeli basi upasuaji mdogo ufanyika kuziharibu tezi za jasho ...but this method is reserved for worth scenarios.

Namna ya matumizi ya vitu hivyo unaweza patiwa na dk hasa dematologist au physician.

Tumia mawasiliano yangu niliyoweka huko juu tuwasiliane kwa msaada zaidi
 
Ahsante kwa msaada wako,
Mwezi huu tarh 3 nilikuw nahs maumivi ya tumbo nikaenda kupima typhod na vidonda vya tumbo,typhod sikuw nayo ila wakaniambia nina bacteria pylori(vidonda) nikaandikiwa dozi na nimeimaliza sahv naendelea vzr, je nipime tena lini ili kuangalia kama hao bacteria wameisha?
 
Asante Dr kwa huduma yako nzuri na ushauri unaotupatia hapa,ubarikiwe sana.

Kwenye vipimo vya HIV hua wanacho cha kwanza na cha pili kwa ajili ya kuthibitisha tatizo,imetokea kipimo cha kwanza kikaonyesha mgonjwa anatatizo cha pili kikaonyesha hana tatizo,huu.mkanganyiko kitaalamu hua limekaaje?
Barikiwa.
Brother pole kwa mkanganyiko.

Usijari ndio changamoto za kitaalamu

Kifupi iko hivi. Tanzania tume adapt utaratibu wa upimaji VVU Kama inavyopendekezwa na shirika la Afya duniani WHO.
Sisi tuna tumia serial test ,yaani tuna vipimo viwili vilivyowekwa kwenye algorithm ya upimaji, SD Bioline and Unigold.

Upimwapo VVU, kipimo Cha kwanza Ni SD Bioline , kipimo hiki Kiko more sensitive and specific , ikiwa jibu ni negative, huna budi kupima Tena , mtu huyo Ni negative, hana virus vya Ukimwi.

Lakini ikiwa jibu Ni positive kwa kipimo hiki unashauriwa ku-confirm kwa kipimo Cha Unigold ambacho Kiko more specific. Na majibu yakiwa positive Tena Basi mtu huyo atakua Ni kweli ameathirika.

Lakini ikitokea scenario hiyo uliyoitoa kipimo Cha kwanza positive but Cha pili negative...majibu haya uitwa discordant results.

Kwa utaratibu tulionao kwa scenario Kama hii utalazimika kuchukua sampuli nyingine ya damu na kuipeleka kwa kipimo kingine kwenye reference lab ambacho Ni HIV ELISA test .

Na majibu ya kipimo hicho Cha mwisho ndo yatakayo determine status ya mtu either Ni positive au lah. Kipimo Cha mwisho, HIv -Elisa kikisema negative Basi mtu huyo Hana maambukizi, ila kikisema positive Basi mtu huyo atakua ameathirika.

Nadhani nimekusaidia kuondoa mkanganyiko.
 
Ahsante kwa msaada wako,
Mwezi huu tarh 3 nilikuw nahs maumivi ya tumbo nikaenda kupima typhod na vidonda vya tumbo,typhod sikuw nayo ila wakaniambia nina bacteria pylori(vidonda) nikaandikiwa dozi na nimeimaliza sahv naendelea vzr, je nipime tena lini ili kuangalia kama hao bacteria wameisha?
Wasiliana nami kwa mawasiliano niliyoyatoa. Kuna kitu ntakushauri
 
Back
Top Bottom