Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Niruhusu nikusaidie kutatua changamoto yako kiafya

Salaam JF

Kama mtaalamu wa afya Mungu amenipa msukumo wa kukusaidia kiushauri juu ya changamoto ya kiafya inayokukabiri. Wataalamu tunaamini kutambua msingi wa tatizo ni hatua mhimu katika kulitatua. Natarajia kukusaidia wewe mwana JF na kama si wewe basi ndg yako au jamaa wako wa karibu.

Ki maadili ya kitaaluma sitakiwi kujitangaza nafanya kazi wapi ili isionekane najipigia upatu unaoweza kulenga kujinufaisha, ila ntaomba ushirikiano wako ili ku-maintain Doctor- patient relationship, utakaojengwa kwa msingi wa mutual respect.

Kimsingi , Mimi ni mtaalamu wa fani za afya. Ni mtumishi wa umma na ninauzoefu wa miaka isiyozidi kumi kwenye field hii. Hivyo mambo ya msingi kiutendaji na kimfumo ninayafahamu na kwa msingi huo ninao uwezo wa kukusaidia kitaalamu juu ya issue mbalimbali za kiafya japo kwa sehemu ili kufanikisha wewe au ndg yako kuwa na afya njema na ustawi

Context ambayo nataka uitumie ni kuuliza swali la kiafya linalokusibu either kwa kutaja dalili za hali ya kiafya inayokutatiza nami nitakusaidia kujua msingi wa tatizo na kukupa options za tiba kwa mkutadha wa conventional medicine yaani tiba ya kitaalamu na sio tiba asili.

Kwa kuzingatia unyeti wa suala la afya, nitakua huru kupokea maoni ya wataalamu wenzangu ili kuboresha na kuhakiki kile ntakachokua nakishauri ili ku-ensure safety ya watu wetu. Na kwa msingi huo ntajitahidi kushauri kile tu kinachokubarika as best practice kwenye fani yetu na si vinginevyo.

Kwa watakaojitokeza kupata msaada wangu ninaomba uvumilivu wao hata Kama nitachelewa kukupa msaada unaoutaka. Kumbuka ninashughuri zingine nyeti kwa ujenzi wa Taifa ila nimekusudia kutenga muda ili nitoe mchango wangu kwa jamii.

Idea hii nitaanza kuitekeleza kwa familia hii ya JF ila badae nakusudia kuipanua kwa jamii pana ya watanzania. Hivyo wale wadau wa afya ntaomba ushirikiano wao ili kusaidiana kufikia lengo la uzi huu.

Nakukaribisha ndg yangu ili unufaike na ushauri wa kitaalamu kwa tatizo lako la kiafya yaani medical consultation.
nini chanzo cha baadhi ya wanaume kukosa hamu ya tendo la ndoa( nyege)
 
Kwanini usinishauri tu hapa kwa faida ya wengine pia?
Acha asili ya ubishi.
Ungefaidika na mengi kuliko jibu unalotaka kulisoma hapa.

Kifupi , Kama unaendelea vyema huna haja ya kwenda kupima tena.
Zingatia maelekezo uliyopewa na dkt wako.
 
Jino linauma tangu usiku hadi muda huu sijawahi kuumwa kiasi hichi pengine inaweza kua nini
 
Mdogo wangu ana tatizo la kutosikia vizuri nilimpeleka muhimbili kufanyiwa vipimo na kubainika kuwa tatizo lake haliwezi kutibika anatakiwa kuvaa mashine ya kumsaidia kuweza kusikia kwa gharama ya laki 3 kwa moja na gharama za kumvalisha elfu 70. Cha ajabu kuna sehem nimeambiwa iko kifaa kinauzwa elfu 80 kwa @1. Naomba kujua nini utafauti wake kiutendaji na athari zake. Kijana ameshakwenda kuripoti chuoni anadai haelewi kitu darasani wala hamsikii kabisa mwalim. Ushauri wako plz ili aweze kuendelea vzuri na masomo yake. Asante
 
Pole kwa kuchelewa kujibu.
Kitaalamu Nini kinasababisha fibroids haijulikani, ila ushahidi wa kitafiti unaonyesha mambo mbalimbali yanaweza kuchangia risk ya kupata fibroids ikiwemo:
Genetic factor au vinasaba vya mtu
Wingi wa hormone ya estrogen and progesterone
Ongezeko la growth hormone
Ukosefu wa vitamin D au
Stress
Uzito mkubwa
Pombe etc.

Tiba halisi Ni upasuaji ili kuviondoa vivimbe kwenye mfuko wa uzazi. Ila mbala wake japo sio effective unashauriwa kubadiri mfumo wa maisha kwa kuzingatia yafuatayo

Ulaji mwingi wa mboga za majani na matunda
Cut off vyakula vya mafuta na nyama
Punguza uzito na kitambi
Kama una Magonjwa ya sukari na BP hakikisha unatibiwa
Acha pombe na sigara ikiwa unatumia
Kula vyakula vyenye vit D au vodonge
Pia Kuna dawa za kubalance hormone ya oestrogen ambayo ndo kichocheo kikubwa Cha fibroids.

Karibu kwa maswali specific
Asante Sana Mkuu kwa ufafanuzi na majibu makini toka kwako Daktari. Barikiwa.
 
Pole kwa kuchelewa kujibu.
Kitaalamu Nini kinasababisha fibroids haijulikani, ila ushahidi wa kitafiti unaonyesha mambo mbalimbali yanaweza kuchangia risk ya kupata fibroids ikiwemo:
Genetic factor au vinasaba vya mtu
Wingi wa hormone ya estrogen and progesterone
Ongezeko la growth hormone
Ukosefu wa vitamin D au
Stress
Uzito mkubwa
Pombe etc.

Tiba halisi Ni upasuaji ili kuviondoa vivimbe kwenye mfuko wa uzazi. Ila mbala wake japo sio effective unashauriwa kubadiri mfumo wa maisha kwa kuzingatia yafuatayo

Ulaji mwingi wa mboga za majani na matunda
Cut off vyakula vya mafuta na nyama
Punguza uzito na kitambi
Kama una Magonjwa ya sukari na BP hakikisha unatibiwa
Acha pombe na sigara ikiwa unatumia
Kula vyakula vyenye vit D au vodonge
Pia Kuna dawa za kubalance hormone ya oestrogen ambayo ndo kichocheo kikubwa Cha fibroids.

Karibu kwa maswali specific
Mi nafikiria mtu anapoona ana mauvimbe, haraka saana akimbilie hospitali.

Benign kuja kuwa Malignant inawezekana kabisa.

Hivi Mkuu kama una mauvimbe katika matiti, mfano lilianza moja kisha likaja la pili. Je, nini kinapelekea kuwa hivi? Na inaweza ikawa ni dalili ya Malignant Neopalism?

Sometimez linakuwa na maumivu makali sana ila pia kuna muda maumivu yanakata.
 
Shukran kwa uzi murua na ubarikiwe kwa kujitoa kuhudumia jamii.

Binafsi napenda kujua reasons za missed abortion, na how to prevent it, na je kama mtu akipata missed abortion kwa mimba ya kwanza je kuna possibilit ya kujirudia tena??
Pole kwa uvumilivu. Sikuweza jibu swali lako kwa Wakati.

Kuhusu swali lako umeuliza reasons for missed abortion, Ila ntajaribu kuongelea abortion kwa ujumla has non elective abortion ambayo ufanyika pale kunapokua na grounds za ujauzito Kama utaachwa kuendelea basi afya ya Mama itakua matatani.

Missed abortion Mara nyingine huitwa missed miscarriage Ni hali ambayo kichanga au fetus ushindwa kuumbika au hufa Wakati nyumba ya uzazi inakua Bado iko intact.

Ila spontaneous abortion au miscarriage Ni ile hali ya ujauzito kutoka/kuharibu a kabla ya kutimiza wiki 20.

Kimsingi sababu zinazopelekea ujauzito kuharibika zaweza kuwekwa kwenye makundi makuu 2. Sabu za kinasaba / chromosome au sababu za kiafaya (medical reasons)

Ikiwa inasadikiwa 10-20% ya mimba uharibika. Takwimu zinaweza kuwa kubwa zaidi ya hizo kwani Mara nyingi mimba uharibika hata mwanamke hajajitambua kama ni mjamzito.

Sababu kubwa za mimba kuharibika utokana na titizo la kinasaba au chromosome linalotokea by chance kipindi kichanga kinapokua katika siku za mwanzo pale ujauzito unapotungwa. Ikiwa itilafu ya ukuaji itajitokeza ,mwili umejijenga kuhakikisha kisichosahii lazima kitolewe ,na hivyo ujauzito lazima utaharibika.

Sababu zingine zinaweza kuwa:
Maambukizi kipindi Cha ujauzito Kama magonjwa ya dhinaa, PID au UTI kali
Ugonjwa wa kisukari
Matatizo ya homoni
Magonjwa ya tezi joto- thyroid disease
Matatizo ya nyumba ya kizazi kama uwepo wa vivimbe- fibroids au shida ya mlango wa kizazi kama -cervical incompetence

Mambo mengine yanayoongeza risk for spontaneous abortion ni
Umri wa mwanamke anaposhika ujauzito. Mfano mama mwenye umri wa miaka 35 ana risk ya 20% ya mimba kuharibika Lakini yule mwenye umri wa miaka 40 na 45 risk zao Ni 40% na 80% respectively.

Viatarishi vingine ni kama
Historia ya mfuatano wa kuharibika kwa ujauzito

Utumiaji wa sigara, pombe kali na madawa ya kulevya

Au invasive procedures kipindi cha ujauzito.

Note: mazoezi , sex au kufanya kazi ofsini hakuna hatari ya kusababisha ujauzito kutoka.

Ni ngumu kuzuia ujauzito usitoke ikiwa sababu ni ile itokanayo na kasoro katika ukuaji wa kichanga-fetus. Upende usipende mwili lazima ukichomoe kiumbe hicho.

Ikiwa Sababu Ni zile za kiafaya, kuwahi clinic na kutunza ujauzito chini ya uangalizi wa wataalamu itakusaidia kubaini tatizo na kuchukua hatua stahiki.

Nadhani nimekusaidia, Ila usiache kuuliza swali mahala nilipokuacha.
 
Kidonda mpaka sasa kina miaka mitano tangu alipopata ajali,,,vipi kama unafaham dawa inayoza kumsaidia nijulishe plc..
Pole ndg , vidonda ndugu ni vigumu kuvitibu bila kujua chanzo Cha tatizo. Naomba mjichange mfike hospital kubwa ambazo huduma ya pathology inatolewa. After biopsy mtapata way forward.
 
habarir
tangu nibalehe(miaka mingi ilopita) mpaka leo chunusi(usoni) na vipele pele (kifuani) haziishi

tena nikila vtu vyenye mafuta kama chips,karanga na maharage yaan ndo kabisa sitazamiki usoni ,,,,,,
tatzo laweza kuwa nn et
Kaka pole
Tatizo la chunusi linawasumbua wengi, japo uzidiana kwa level ya severity.

Kimsingi chunusi ni tatizo la ngozi , laweza kuwa la muda mfupi au la kudumu -chronic .

Kinachotokea kwa mtu mwenye chunusi ni kuwa Kuna tezi chini ya ngozi iitwayo sebaceous gland...hutoa oily substance iitwayo sebum. Sasa tezi inayozalisha mafuta haya chini ya ngozi zinaweza kuwa kuziba vinyweleo, na badae kupata maambukizi ya bacteria na kuvimba.

Yako mambo yanayoongeza risk ya kuwa na chunusi Kama vile:

Mabadiriko ya homoni hasa kipindi Cha barehe
Ngozi yenye mafuta mengi
Vyakula vyenye mafuta mengi zikiwemo karanga
Stress
Baadhi ya side effects za dawa Kama steroids, anticonvulsant, barbiturates or lithium ( mniwie radhi nakosa kiswahili chake)

Usafi hafifu wa uso na mwili

Vipodozi vya ngozi na nywele. Kuna baadhi ya makeup, scribe etc zinaweza kusababisha skin irritations.

Zipo dawa ambazo matabibu tunazitoa hasa kwa wale ambao hwajatumia dawa sana. Ila tunashauri mtu mwenye chunusi atibiwe na madaktari wa ngozi.

Kama eneo lako halina dematologist please wasiliana nami tuone tunavyoweza saidiana.
 
Kaka pole
Tatizo la chunusi linawasumbua wengi, japo uzidiana kwa level ya severity.

Kimsingi chunusi ni tatizo la ngozi , laweza kuwa la muda mfupi au la kudumu -chronic .

Kinachotokea kwa mtu mwenye chunusi ni kuwa Kuna tezi chini ya ngozi iitwayo sebaceous gland...hutoa oily substance iitwayo sebum. Sasa tezi inayozalisha mafuta haya chini ya ngozi zinaweza kuwa kuziba vinyweleo, na badae kupata maambukizi ya bacteria na kuvimba.

Yako mambo yanayoongeza risk ya kuwa na chunusi Kama vile:

Mabadiriko ya homoni hasa kipindi Cha barehe
Ngozi yenye mafuta mengi
Vyakula vyenye mafuta mengi zikiwemo karanga
Stress
Baadhi ya side effects za dawa Kama steroids, anticonvulsant, barbiturates or lithium ( mniwie radhi nakosa kiswahili chake)

Usafi hafifu wa uso na mwili

Vipodozi vya ngozi na nywele. Kuna baadhi ya makeup, scribe etc zinaweza kusababisha skin irritations.

Zipo dawa ambazo matabibu tunazitoa hasa kwa wale ambao hwajatumia dawa sana. Ila tunashauri mtu mwenye chunusi atibiwe na madaktari wa ngozi.

Kama eneo lako halina dematologist please wasiliana nami tuone tunavyoweza saidiana.
ok mkuu ntafanya hvo mana hii acne ni chronic....tangu 2012 up to date
 
Mkuu hivi kuwa na sauti nzito kupita kiasi inasababishwa nanini.kama ukipita nje ukanisikia sauti yangu unaeza sema nipo kwenye .....
Mkuu umenichekesha ila usijali

Tatizo la utofauti wa sauti ni la kimaumbile tu kama vile Kuna watu wafupi na warefu, weusi na weupe, wenye sauti ya Kwanza vs sauti ya 4 etc.

Tofauti zetu ziko kwenye organ mbili hizi , larnyx na vocal cords na mfumo wa hewa kwenye mapafu. Msukumo wa hewa kwenye koromeo(larynx) na mwitiko (vibration) wa kiwambo Cha sauti (vocal cord) ndo uleta tofauti hizo.

Wakati sababu kubwa ikiwa ni ya kimaumbile , kwenye organ zinazozalisha sauti, mambo mengine ambayo upelekea utofauti wa sauti ni pamoja na
Umri
Matumizi ya sigara na madawa ya kulevya
Personality ya mtu, Kuna watu huzungumza kwa nguvu kuliko wengine
Tamaduni za watu, kuna tamaduni zinamtaka mdada aongee kwa sauti ya chini na mwanaume akaze sauti

Mazingira ya makuzi. Kuna uhusiano wa mtu kukulia mazingira ya watu waongeaji sana na yenye makele na kuwa na sauti kubwa kuliko mtu aliyekua kwenye mazingira ya utulivu sana.
 
nini tiba mkuu. Kwa mtu alieathirika na kujichua kwa muda mrefu
Kujichua siyo issue...eleza umeathirikaje

Je haudindishi
Je unawahi fika kileleni
Je huna hamu ya tendo
Je je uwezi endelea zaid ya round moja?
Be specific tunone namna ya kukusaidia
 
Mdogo wangu ana tatizo la kutosikia vizuri nilimpeleka muhimbili kufanyiwa vipimo na kubainika kuwa tatizo lake haliwezi kutibika anatakiwa kuvaa mashine ya kumsaidia kuweza kusikia kwa gharama ya laki 3 kwa moja na gharama za kumvalisha elfu 70. Cha ajabu kuna sehem nimeambiwa iko kifaa kinauzwa elfu 80 kwa @1. Naomba kujua nini utafauti wake kiutendaji na athari zake. Kijana ameshakwenda kuripoti chuoni anadai haelewi kitu darasani wala hamsikii kabisa mwalim. Ushauri wako plz ili aweze kuendelea vzuri na masomo yake. Asante
Ndg please kuwa serious na afya ya dogo.
Ni vigumu mm kukupa jibu kipi ni kifaa kizuri coz Sina specifications ya vifaa hivyo kama vinafanana au ni Orginal Vs fake -one.

Je hao waliokuambia utapata kifaa hicho kwa tsh 80,000 ni madaktari au wataalamu wa ENT ?

Unaweza kimbilia cheap Ila kisiwe msaada kwa kijana

Cha mhimu waamini madaktari wa Mhimbili, jichange nenda kawaone wataalamu.

Naelewa changamoto ya kifedha Ila linganisha hiyo laki 370,000 Na usumbufu na kero anazopitia kijana.

Please jipangeni muwahi hospitali
 
Back
Top Bottom