- Thread starter
- #61
Nimesoma kwa umakini tatizo lako , Kama Daktari ninaweza hisi maumivu uliyonayo. Pole ndg .Dr,nisaidie nina mwaka sasa na miezi miwili toka nitembee na binti positive wa VVU toka kipindi hicho nimekua napata dalili tofauti tofauti kama ulimi kuwa mweupe,,kichwa mwanzo kiliuma sana na presha ikapanda ila kwa sasa kimetulia,kuhisi kama mitoki,,sasa nina tatizo la vipele kuwasha sana nimetumia dawa za alegy lakini vinapoa vinaendelea kuwasha,,,nimepima Mara nyingi sana na Mara ya mwisho siku saba zimepita ila majibu ni Negative,,sorry Dr naweza nikawa na tatizo gani au bado nipo kwenye window period!??? asante
Kuhusu VVU ondoa shaka , ikiwa hujashiriki ngono zembe hivi karibuni . Window period ni kipindi kisichozidi week 2-4. Kama vipimo vya HIV Ni negative basi waamini watoa huduma.
Umetaja dalili nyingi sana na hivyo inahitajika clear medical history nzuri ili kujua je dalili hizo ni ugonjwa mmoja au maladhi tofauti.
Kutoka mitoki mingi ni dalili ya systemic infection, ikiwemo maradhi ya kansa za damu au lymphoma.
Ulimi mweupe uenda ikawa ni dalili ya fungus za kinywa....ambazo mara nyingi hutokana na upungufu wa Kinga mwilini
Kupata vipele Mara kwa mara inaweza kuwa allergy au tatizo lingine.
Ntaomba tuwasiliane kwa mawasiliano niliyotoa hapo juu ili nikusaidie kwa ukaribu.