Nipo Moshi, Bibi Kanitafutia Mdada, ananishawishi nimuoee...

Nipo Moshi, Bibi Kanitafutia Mdada, ananishawishi nimuoee...

Chukua jiko hilo kijana
Robo ya Maisha yangu niliishi Moshi-Kibosho, kuanzia Std 1-form 1. Kwa muda wote nimekuwa nikiishi na bibi.....

Sasa bhana, Tangu nije hapa kuna binti huwa anakuja hapa nyumbani anasaidia saidia kwani kuna shughuli mbalimbali zinafanyika sikukuu hii.....

Mimi sikumtia maanani, na nilijua anaweza kuwa moja ya ndugu zangu kwani tuliokuja huku ni wengi . Ni binti mdogo kama miaka 20 hivi, mwembamba black beauty na karefu hivi....

Sasa jana nikiwa na jamaa zangu tuliokuwa tumeachana kitambo tukipiga stori mbilitatu na mbege taratibu, ndipo Akaja mdogo wangu kuniambia bibi anakuita....

Nilimkuta bibi kabeba Mundu (Panga flani limepindwa mbele) akaniambia nikamsaidie kubeba mkungu wa ndizi shambani....

Tukiwa tunatembea, akaanza kuniuliza maswali ninaoa lini? Au ninataka afe ndio nioe asimuone mjukuu wake na Moli wake (mke wangu)??.....

Nilimweleza kuwa bado naweka mambo sawa, na nina muhaidi hatakufa kabla ya kuona hivyoo vyotee....

Akaniuliza Mchumba umeshampata, nikamjibu bado huku najichekeshaa...

Bibi alikuwa mbele, ndipo akageuka nyumna na kunieleza, unamuona yule binti wa fulani? Nikawa sijampata mana mabinti huku ni wengi. Akanieleza binti mwenyewe alivyo, na kuniambia, tayari ashamwambia Mama yake kuwa anataka Mjukuu wangu(mimi) amuoe binti yake....

Akasema ndio maana yupo hapa tangu umekuja. Akaniambia kamaliza form 4 hakufaulu lkn akiwa hapa kijijini, hakuwahi jihusisha na tabia mbaya, anajua kukata majani ya Ng'ombe, kufagia zizi la ng'ombe anajua kulima, kufanya usafi, kupika na anakwenda sana kanisani...

Akasema kazi zote za nyumbani hufanya yeye, na watu wa hapa kijijini wanampenda sana. Akasema niachane na vibinti vya mjini kwani ni vivivu na havijui kufanya kazi na haviogopi mungu....

Kiukweli aliongea mengi lkn kubwa ni msisitizo kuwa nimuoee. Nilimjibu tutaongea na nitafikiria kwa kuzingatia kuwa, haitakuwa busara kumkatalia au kuanza kubishana nae...

Ilinibidi nianze kufuatilia nyendo za huyu dogo na nikagundua kuwa, hata yeye alikuwa tayari alikwishwa elezwa mpango huu....


Anyway, mkasa ndio huo, kuhusu kuoa au kutomuoa hilo sintalizungumza hapa ila habari kubwa niliyokutana nayo Kibosho ndio hii.

Karibuni Mbege wakuu!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasiwasi wangu kwa huyo mke wako mtarajiwa ni kwamba akishafika mjini kichwa kitaota mapembe mwisho wa siku ataanza kugawa
 
Robo ya Maisha yangu niliishi Moshi-Kibosho, kuanzia Std 1-form 1. Kwa muda wote nimekuwa nikiishi na bibi.....

Sasa bhana, Tangu nije hapa kuna binti huwa anakuja hapa nyumbani anasaidia saidia kwani kuna shughuli mbalimbali zinafanyika sikukuu hii.....

Mimi sikumtia maanani, na nilijua anaweza kuwa moja ya ndugu zangu kwani tuliokuja huku ni wengi . Ni binti mdogo kama miaka 20 hivi, mwembamba black beauty na karefu hivi....

Sasa jana nikiwa na jamaa zangu tuliokuwa tumeachana kitambo tukipiga stori mbilitatu na mbege taratibu, ndipo Akaja mdogo wangu kuniambia bibi anakuita....

Nilimkuta bibi kabeba Mundu (Panga flani limepindwa mbele) akaniambia nikamsaidie kubeba mkungu wa ndizi shambani....

Tukiwa tunatembea, akaanza kuniuliza maswali ninaoa lini? Au ninataka afe ndio nioe asimuone mjukuu wake na Moli wake (mke wangu)??.....

Nilimweleza kuwa bado naweka mambo sawa, na nina muhaidi hatakufa kabla ya kuona hivyoo vyotee....

Akaniuliza Mchumba umeshampata, nikamjibu bado huku najichekeshaa...

Bibi alikuwa mbele, ndipo akageuka nyumna na kunieleza, unamuona yule binti wa fulani? Nikawa sijampata mana mabinti huku ni wengi. Akanieleza binti mwenyewe alivyo, na kuniambia, tayari ashamwambia Mama yake kuwa anataka Mjukuu wangu(mimi) amuoe binti yake....

Akasema ndio maana yupo hapa tangu umekuja. Akaniambia kamaliza form 4 hakufaulu lkn akiwa hapa kijijini, hakuwahi jihusisha na tabia mbaya, anajua kukata majani ya Ng'ombe, kufagia zizi la ng'ombe anajua kulima, kufanya usafi, kupika na anakwenda sana kanisani...

Akasema kazi zote za nyumbani hufanya yeye, na watu wa hapa kijijini wanampenda sana. Akasema niachane na vibinti vya mjini kwani ni vivivu na havijui kufanya kazi na haviogopi mungu....

Kiukweli aliongea mengi lkn kubwa ni msisitizo kuwa nimuoee. Nilimjibu tutaongea na nitafikiria kwa kuzingatia kuwa, haitakuwa busara kumkatalia au kuanza kubishana nae...

Ilinibidi nianze kufuatilia nyendo za huyu dogo na nikagundua kuwa, hata yeye alikuwa tayari alikwishwa elezwa mpango huu....


Anyway, mkasa ndio huo, kuhusu kuoa au kutomuoa hilo sintalizungumza hapa ila habari kubwa niliyokutana nayo Kibosho ndio hii.

Karibuni Mbege wakuu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo ndiyo mke oa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si umesema kafaulu form four? Mkuu, unataka kuchezea 30yrs? Kama vipi hakikisha kabisa kapata chuo cha ualimu ndio uanze mipango ya ndoa. La sivyo, the trouble is looking for you!
 
Hahahahaaaaa umemuwakia nikacheka nusu mbavu zangu zipate crack ila mi kina manka nnawapenda sana halafu nnanyota nao balaaaa sijui kwa kua nnamapesa lukuki ndio maana.
Hahaaaaa Kuna watu wao hupomda makabila ya wengine baada ya kukataliwa kwa kutokujielewa kwao bwana. Kina manka hawana shida kwa mtu muelewa ukiwa mbulula watakusomesha number

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom