Joseph Isaack
JF-Expert Member
- Aug 8, 2011
- 450
- 89
Halafu huyu muliza swali atakuwa shabiki wa chadema.Kwa akili alizokuwa nazo lazima niamini hivyo
Kivipi mkuu?
Halafu huyu muliza swali atakuwa shabiki wa chadema.Kwa akili alizokuwa nazo lazima niamini hivyo
Na Mji ambao haujafikia ukubwa wa kiwango cha manisapaa unaitwaje?
Hakuna tofauti kati ya Halmashauri na Manispaa, isipokuwa umekata maneno kwa sababu jina sahihi ni Halmashauri ya Manispaa ya ...... ie Mkoa wa Kigoma kuna Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji (Kigoma/Ujiji Municipal Council-KUMC), Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma (Kigoma District Council - KDC), kuna Kibondo DC,Kasulu DC nk.
Sasa Tofauti ya Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Manispaa nafikiri ndio kusudio la msingi la swali lako, ipo hivi manispaa inapewa baada ya kuwa na vyanzo vya kujiendesha yenyewe angalau kwa asilimia fulani zaidi 30% (sina uhakika sana), pili idadi ya watu kwa eneo yaani population per unit area, watu wamesongamana kiasi gani, concetration per urea.
Kwa sababu idadi ya watu waliopo Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ni kubwa ukilinganisha na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji lakini msongamano wa watu katika eneo dogo la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni kubwa kuliko la Halmashauri ya wilaya ya Kigoma. Naomba nifafanue hapo kwenye msongamano ie unaweza kuta KDC watu 100 wanakaa kwenye wastani wa mita za eneo 1000 lakini lakini KUMC watu 100 wanakaa kwenye eneo la 500, na ndio maana utaona Halmashauri za manispaa nyingi zipo mjini, kwa mfano Dar es Salaam kuna Halmashauri za manispaa tu na hakuna Halmaahauri za wilaya yaani Kinondoni, Ilala and Temeke municipal Council.
Vile vile kuna wilaya hapo tusichanganye vyote viwili yaani Halmashauri ya Manispaa na wilaya zinaweza kuwa katika wilaya moja ie Kigoma/Ujiji Municipal Council and Kigoma District Council zote zipo KIGOMA DISTRICT.
Na Mji ambao haujafikia ukubwa wa kiwango cha manisapaa unaitwaje?
Kwanza napenda kutofautiana na mtazamo wako.Ndio maana nasema hii JF imevamiwa. Sasa kama huelewi hata halmashauri ni kitu gani, unawezaje kupata ujasiri wa ku"post" mada hapa?
1. Halmashauri ya mji
2. Halmashauri ya manispaa
3. Halmashauri ya Jiji
N.K
Ni kweli mkuu, maana hapa duniani kuna watu wanajifanya wanajuwa kumbe hamna kitu, na mbaya zaidi hawajui kama hawajui na wanavyozisi kuelezea maana ya hicho wanachodhani kuwa wanajuwa ndivyo wanavyozidi kutuonyesha jinsi gani hawajui. Ila wa aina hii ni wa kuwapa ukweli tu hata kama utawaume.... JF kiboko yao na ni shule kwa wote kwa namna inayoumiza, inayofurahisha au mchanganyiko.somo zuri mno japo wengine wanzuga kujua na ukweli hawafahamu chochote na hsa waliompinga mtoa mada
kama mimi....... Mapendo..... DAIMAHatimaye nimeelewa sasa...
Mapendo.
Na mimi naongezea ifuatayo ingawa sio rasmi lakini ni halmashauri kamili:Naomba nikuunge mkono, kwa kuongezea zaidi hivi ili hawa vijana waweze kuelewa.
Halmashauri ya Kijiji
Halmashauri ya Mji
Halmashauri ya Wilaya
Halmashauri ya Manispaa
Halmashauri ya Jiji.
Hivi ukisema halmashauri ya manispaa na manispaa ni kitu kimoja au tofauti
Ni Sawa Tu Na Kusema Mchezaji Simon Msuva Wa Yanga Na Klabu Kongwe Ya Mpira Wa Miguu Na Isiyo Na Maendeleo Nchini Tanzania / Duniani Ya Yanga. Umeelewa?