Hakuna tofauti kati ya Halmashauri na Manispaa, isipokuwa umekata maneno kwa sababu jina sahihi ni Halmashauri ya Manispaa ya ...... ie Mkoa wa Kigoma kuna Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji (Kigoma/Ujiji Municipal Council-KUMC), Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma (Kigoma District Council - KDC), kuna Kibondo DC,Kasulu DC nk.
Sasa Tofauti ya Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Manispaa nafikiri ndio kusudio la msingi la swali lako, ipo hivi manispaa inapewa baada ya kuwa na vyanzo vya kujiendesha yenyewe angalau kwa asilimia fulani zaidi 30% (sina uhakika sana), pili idadi ya watu kwa eneo yaani population per unit area, watu wamesongamana kiasi gani, concetration per urea.
Kwa sababu idadi ya watu waliopo Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma ni kubwa ukilinganisha na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji lakini msongamano wa watu katika eneo dogo la Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni kubwa kuliko la Halmashauri ya wilaya ya Kigoma. Naomba nifafanue hapo kwenye msongamano ie unaweza kuta KDC watu 100 wanakaa kwenye wastani wa mita za eneo 1000 lakini lakini KUMC watu 100 wanakaa kwenye eneo la 500, na ndio maana utaona Halmashauri za manispaa nyingi zipo mjini, kwa mfano Dar es Salaam kuna Halmashauri za manispaa tu na hakuna Halmaahauri za wilaya yaani Kinondoni, Ilala and Temeke municipal Council.
Vile vile kuna wilaya hapo tusichanganye vyote viwili yaani Halmashauri ya Manispaa na wilaya zinaweza kuwa katika wilaya moja ie Kigoma/Ujiji Municipal Council and Kigoma District Council zote zipo KIGOMA DISTRICT.