VIGEZO VYA KUANZISHA HALMASHAURI ZA MIJI, MANISPAA NA JIJI:
Vigezo vya ujumla
i. Jiografia ambayo inafanya utoaji huduma kwa Wananchi kuwa mgumu
kwa sababu ya milima, mito, misitu, mabonde au Visiwa.
ii. Kuwepo kwa miundombinu inayohitajika kwa eneo la utawala kuanzishwa,
iii. Kuwepo kwa mtandao wa barabara za uhakika kuunganisha Makao Makuu
ya eneo la utawala lililoanzishwa na maeneo mengine yenye kuhitaji
kuhudumiwa na Makao Makuu,
iv. Uwezo wa Serikali wa kuanzisha eneo jipya la utawala,
v. Utayari wa Wananchi kuchangia uanzishaji wa eneo la utawala.
Aidha, ili maeneo hayo yaweze kuanzishwa/ kupandishwa hadhi vimewekwa
vigezo kwa mujibu wa Sheria ya Mipango Miji Na 8 ya mwaka 2007 (The Urban
Planning Act No 8 of 2007) Kipengele cha Tano cha Jedwali la Tano (Item
number 5 of the Fifth Schedule) kama ifuatavyo:-
Vigezo vya kuanzisha Mamlaka ya Mji Mdogo (Township
Authority)
Mamlaka ya Mji Mdogo ni Mamlaka ya Serikali za Mitaa iliyopo kwenye Mamlaka
za Wilaya. Mamlaka hizi zinaanzishwa pale ambapo palikuwa ni Kijiji ambacho
kimeanza kuendelezwa na kuwa na mazingira ya kimji. Waziri mwenye dhamana
ya Serikali za Mitaa amepewa madaraka ya kutangaza Kijiji au Vijiji vilivyofikia
sifa zilizowekwa kuwa Mamlaka za Miji Midogo.
Vigezo vinavyotakiwa kuzingatiwa:
i. Kuwe idadi ya watu wasiopungua elfu kumi (10,000);
ii. Kuwe na huduma za jamii zifuatazo: Shule ya Sekondari, Kituo cha Afya
na Mahakama ya Mwanzo;
iii. Kuwe na Soko pamoja na Maduka ya rejareja yasiyopungua matano (5);na
iv. Eneo liwe ni Makao Makuu ya Kata au Tarafa.
Vigezo vya kuanzisha Halmashauri ya Mji (Town Council)
i. Kuwe na watu wasiopunga 30,000.
ii. Mji uwe na uwezo wa kujiendesha angalau kwa asilimia 50% ya bajeti
yake.
iii. Mji uwe na kiwango cha juu cha utoaji huduma ya hospitali, kuwe na
shule ya Sekondari, kuwe na angalau maduka ya rejareja yenye leseni
yasiyopungua 50, Kituo cha Polisi na pawe na Makao makuu ya Tarafa.
Vigezo vya kuanzisha Halmashauri ya Manispaa
i. Kuwe na watu wasiopungua laki moja (100,000)
ii. Kuwe na watu wasiopungua laki moja (100,000)
iii. Asilimia 30% ya wakazi wake wawe katika ajira isiyohusiana na kilimo
(Non agricultural Sector)
iv. Kuwe na walau kiwanda kikubwa kimoja (Manufacturing industry)
v. Kuwe na viwanda kadhaa vya “Processing
vi. Asilimia Sabini (70%) ya matumizi ya Manispaa yatokane na vyanzo vya
mapato ya Halmashauri (Own Sources).
vii. Kuwepo na huduma za jamii zifuatazo:-
Kituo cha Elimu ya Watu Wazima;
Hospitali ya Rufaa;
Chuo Kikuu;
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa;.na kiwe ni Kituo cha Taasisi za
Kimataifa (Mult National organization.)
Vigezo vya kuanzisha Halmashauri ya Jiji
i. Kuwe idadi ya watu wasiopungua laki tano (500,000);
ii. Kuwa na uwezo wa kujitegemea kwa asilimia tisini na tano (95%) kwa
mapato yake ya ndani; na
iii. Kuwepo sifa nyingine zaidi ya sifa za kawaida za Manispaa kama vile
maeneo ya kihistoria, maeneo ya utalii; Makao Makuu ya Mkoa; kituo cha
shughuli za Kimataifa na nyinginezo.