Kwa haraka haraka....
Kwanza wengi hawafahamu kwamba kuna michoro mingi tu kabla ya huyu Leonardo Da Vinci kuzaliwa ilishachorwa na wachoraji wengine na ilikuwa tofauti na huu mchoro wa Da Vinci.....
Pili,hakuna anayejua kwa hakika kuwa Leonardo Da Vinci alikuwa akimaanisha nini kwenye michoro yake kwasababu hakuwahi kuacha maelezo kuelezea alichokuwa akikimaanisha.Kitu pekee ambacho nina uhakika nacho ni kwamba Leonardo Da Vinci alibuni mchoro huo kwa namna alivyouona na kufikiri yeye na huenda alikuwa na maana ambayo hakuna ajuaye....
Kwa maana hii,yote yanayohusu mchoro huu ambao ni wa kubuni nayo pia ni ya kubuni kwasababu hayana uhakika.Sijaona sababu ya msingi ya watu kuhangaika na mambo ambayo yamejengwa kutoka mchoro wa kubuni na usio na ukweli wowote...
Kama akija mtu na kusema kuwa huyu Da Vinci alikuwa anamaanisha chochote nje ya masuala ya Yesu huenda akasikilizwa kwa sehemu,lakini akija na kusema kuwa Da Vinci alikuwa anamaanisha chochote kuhusu Yesu hatasikilizwa kwasababu ni uwongo kwasababu Da Vinci hakuishi wakati wa Yesu na kwa maana hiyo alibuni tu huo mchoro,kama alibuni kitakachosemwa chochote kuhusu mchoro huo nacho kitakuwa cha kubuni tu....
Nikija kwenye unachotaka kuhusu mabaya aliyomaanisha Da Vinci kuhusu mchoro huo nitaeleza kwa kifupi kwa sababu sikujiandaa na hili na pia ni jambo ambalo halina uhakika pia kwasababu nilizozieleza hapo juu....
Karibu kwa ufupi..
Leonardo Da Vinci alizaliwa huko Italia tarehe 15 April 1452 na jina lake kamili ni Lionardo di ser Piero da Vinci.Leonardo Da Vinci alijulikana sana kwa taaluma yake ya uchoraji mahiri sana kwa wakati wake.Wakati wa ujana wake,Da Vinci na vijana wengine watatu walishitakiwa kwa kujihusisha na mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.hii ilikuwa ni mwaka 1476.
Leonardo Da Vinci aliwahi kuwa msaidizi wa anayedaiwa kuwa mtoto wa Papa Alexanda wa 6 mwaka 1502 hadi October 18 1502.Borgia alizaliwa Sept 13,1475,huko Rumi.Wazazi wake wakiwa ni Papa Alexander na mwanamke aliyajulikana kama Vannozza Dei Cattanei....
Inadaiwa kwamba wakati Da Vinci akiwa ni msaidizi wa kijana huyu huko Rome,walianzisha mahusiano ya kingono ya kinyume na maumbile.Inadaiwa kwamba katika kipindi ambacho walikuwa kwenye mapenzi moto moto ndipo Leonardo Da Vinci alichora picha hizi za kubuni na kutokana na mapenzi yake kwa Borgia aliaamua kuchora sura ya Borgia kwenye umbo la mtu aliyebuni kuwa kama Yesu...
Picha hii maarufu inadaiwa kuchorwa kati ya mwaka 1499 na 1503...
Baadhi ya watafiti wanadai kwamba lengo lingine la mchoro wa Leonardo Da Vinci ni kutaka kuonesha kuwa Yesu hakuwa na Uungu wowote bali alikuwa ni mtu tu...
Jambo hili lilionekana kwenye michoro hiyo ambayo alichora michoro yake bila kuwawekea kitu kinachoitwa "Halo"..
Halo ni nini?
Halo ni ule mduara unaoonekana kichwani kwa mtu yoyote anayechukuliwa kuwa ni mtakatifu...
Angalia picha hizi hapa chini....
Mchoro wa Leonardo Da Vinci wa karne ya 15 ukionesha wahusika wa mchoro wakiwa hawana hiyo mizunguko vichwani mwao kuonesha utakatifu....
Mchoro wa karne ya 14 ukionesha karamu ya mwisho kama ulivyobuniwa na mchoraji kipindi hicho.Hapa tunaona wahusika wakiwa na "halo" au round fulani hivi vichwani mwao kuonesha "utakatifu" wao....
Mchoro mwingine wa karamu ya mwisho wa karne ya 14...
Ukiangalia michoro hii inatofautiana,lakini yote ni ya kubuni tu....
Kwa maana hii ni kwamba mchoro wa Da Vinci una maana mbili hasi na ambazo pia hazina uhakika au ushahidi sana au hakuna kabisa ushahidi wowote...
1;Mahali alipoamua kumchora mtu aliyepachikwa kuwa ni Yesu alimchora mtu huyo kwa sura ya Cecare Borgia...
2; Alichora p[icha hizo kuonesha kuwa Yesu hakuwa na Uungu wowote ule...
Ni hayo tu kwa ufupi sana....
Na dhani nimekata kiu yako kwa sehemu....