Nini tafsiri halisi ya picha ya the last supper?

Nini tafsiri halisi ya picha ya the last supper?

Mada kama hizi ndio wale vichwa maji wa JF huingia mitini
 
Kuna mambo huwa yananisikitisha sana tena sana.....

Hii dunia ni yajabu kweli kweli.Yale mambo ambayo ni conspiracy yanaonekana ndiyo ukweli wenyewe na ukweli unaonekana ni conspiracy.Ukiangalia kwa mfano hili suala la hii inayoitwa picha ya last super,inajulikana ilichorea na mtu aliyeishi miaka mingi sana baada ya kuwepo kwa Yesu na inajulikana kabisa ni ya kubuni tu,ni kwanini watu wanaichukulia kwa namna kubwa kiasi hiki?

Mleta mada umetaka tuijadili picha hii,ni kwanini tuijadili wakati siyo kitu halisi na ni cha kubuni tu? Tena aliyebuni ni mtu tu na interest zake.Leonado da Vinci ni nani haswa hadi tuzingatie michoro yake kuhusu nyakati ambapo hakuwepo?

Ninachojua mimi huyu jamaa alikuwa ni mwanachama wa vyama vya siri na alikuwa anajua siri kadhaa ya vyama hivi na baadhi ya siri hizo aliziweka kwenye michoro yake kwa codes fulani fulani lakini hakuwa akijua lolote kuhusu maisha ya Yesu kiasi kwamba tumtilie maanani kwa kiwango hiki....

Kama tukague kile alichokuwa anakijua kuhusu haya mambo yao ya sirini hapo sawa lakini siyo kukagua michoro yake ya kubuni kama vile ni michoro halisi inayowakilisha maisha ya Yesu....
Hakika
 
Kutokana na tafsiri za hiyo picha inasemekana miongoni mwa wanafunzi wa Yesu Maria Magdalena naye alikuwemo.
Na alishiriki chakula na Bwana ambaye pia inasemekana alikua ni bwana wake na walizaa mtoto.
Hii nimeisoma kwenye kitabu cha the Davinc Code.
Utakuja kupigwa mawe humu.wenyewe wana sema hajawahi kuwa na mke wala mtoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zuungukeni kote , lakini mjue Yesu ( Issa) hakuoa na wala hakupata kuwa na hawara wala mtoto na awaye yeyote ataye mzushia uongo huu Nabii Is amezusha na uzushi una adhabu mbele ya Allah
Uislam.haujasema kama yesu alikuwa na mke na watoto.au hakuwa nao.maisha ya yesu yamebaki njia panda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utakuja kupigwa mawe humu.wenyewe wana sema hajawahi kuwa na mke wala mtoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana siyo mimi hii niliisoma kwenye kitabu cha Davinc code
,kina tafsiri ya vitu vingi vingi vinavyotambulika katika ukristo.
Amejaribu kuvidadavua kwa uwazi zaidi.
Ila kikubwa ni kushikilia Imani yako.
Amini unachoamini yeye Da Vinc anaweza asiwe Sahihi ama akawa Sahihi,
Lakini haifai kubadili imani ya mtu.
 
UKRISTO

ALEXANDER,THE GREAT(actually the invader/barbarian)

Alexander,The Great(the barbarian,the invader) aliivamia Kemet(Misri) mwaka 332 BC na kumuondoa mfalme(farao) na yeye kuchukua kiti cha ufalme akiwa hajui chochote kuhusu mila na desturi za Misri.

Aliwalazimisha viongozi wa “dini” iliyokuwa inaabudiwa wamkubali katika dini yao,lakini walimkatalia.Alexander mvamizi alikufa mwaka 323 BC.

Mrithi wa Alexander ,Ptolemy I au Soter(maana ya soter ni mwokozi) naye alikataliwa kuwa sehemu ya “dini” ya wamisri wa kipindi hicho lakini katika mji wa Memphis alipata baadhi ya viongozi wa dini waliosaliti na kumkubali.Walimpa jina la SERAPIS kwa kuunganisha majina Osiris na hepis.Huyu Ptelomy I ndiye aliyetibua misingi ya imani ya wamisri wa kipindi hicho.

Ptolemy I au Soter au Serapis au Christus alijipa cheo cha farao,alitengeneza sanamu ya kichwa yenye sura yake na watu wote walilazimishwa kuabudu lile sanamu.Waliomwabudu serapis walikuwa wanaitwa wakristo(neon la Kigiriki Christus)

SERAPIS 350 BC



ARIUS(256-336 A.D)

Alikuwa mmoja wa viongozi wa dini chini ya utawala wa warumi aliyepaza sauti kuwa kuabudu sanamu la serapis haikuwa sawa hivyo watu wote waache kuliabudu.

MKUTANO WA NICEA 325 A.D(the council of nicea)

Uliwakutanisha viongozi wa juu wa dini chini ya uenyekiti wa mfalme Constantine na ajenda kuu ya kwanza ilikuwa ni kumnyamazisha Arius asiendelee kueneza sumu ya kupinga kumuabudu serapis.Katika kipindi chote kulikuwa hakuna mtu anayeitwa yesu(jesus),aliyeabudiwa alikuwa ni serapis soter au mwokozi kwa Kiswahili.

MAAZIMIO YA MKUTANO WA NICEA 325 A.D

Ambapo ilitolewa “statement” ya imani ya kikristo iliandikwa na makasisi(bishops?) wa kanisa la roma wapatao 318.statement(ambayo ni kanuni ya imani kwenye kanisa katoliki la roma) inasomwa ‘nasadiki kwa mungu baba mwenyezi muumba mbingu na dunia,na kwa yesu kristo mwanae wa pekee’(hapa anaongelewa serapis sanamu).

1.Kubadilisha sanamu la serapis na kuweka la yesu

2. Kumfukuza Arius(exile) asiendelee kupinga imani ya warumi
Acha uongo wewe.
 
Hapana siyo mimi hii niliisoma kwenye kitabu cha Davinc code
,kina tafsiri ya vitu vingi vingi vinavyotambulika katika ukristo.
Amejaribu kuvidadavua kwa uwazi zaidi.
Ila kikubwa ni kushikilia Imani yako.
Amini unachoamini yeye Da Vinc anaweza asiwe Sahihi ama akawa Sahihi,
Lakini haifai kubadili imani ya mtu.
Najua sio wewe.lakini kwani yesu kuwa na mke na WATOTO NI KOSA?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona huyo Mary mwenyewe, anaonekana akiwa BIZE zaidi na Wapambe/Mawaziri/Wanafunzi wa Yesu...!?

Picha inajionesha wazi kuwa Mlengwa/mtajwa (Yesu) as if hausiki na Mary, na yeye wala hajali..!

Da vinci angekuwa hai, maswali ya kumuuliza, ni je...! Mary alivamia kwenye Cabinet au alikuwa ni Mualikwa...?

Na kwa nini kwenye picha ameonesha utovu wa nidhamu, badala ya kuwa beneti na Mr Chairman, ameonekana kuvutiwa na kuwa concetrated na watu upande mwingine...!!

Najaribu kuwaza tu..........huyu Da vinci ameibuni picha hii kutoka wapi...! Kwani naamini miaka hiyo nyuma yeye hakuwepo.

Mawazo na michango iendelee...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Eiyer mimi huwa nakukubali sana kwa kazi yako humu jukwaani.

Mimi nina swali kwako kuwa huyu da vinci kama unavyosema kuwa aliishi kipindi kireefu baada ya Yesu, na mimi sitilii maanani kazi zake za kuchanganya ulimwengu hasa sisi tunaomini katika kristo, lakini mimi najiuliza ni kwanini Wayahudi wamekuwa wakitumiwa sana kuupotosha ukweli wa Neno la Mungu kwa kiasi hiki??????

Pia Huyu da vinci aliyaleta haya ili iweje maana naamini hakuna kitu bila sababu ya hicho kitu huenda unaufaham kidogo kuhusu huyu mtu na mazingira ya kipindi chake alichoishi.

Nipanue ubongo kidogo hapo mkuu.
Mkuu,ngoja nianze na hao Wayahudi....

Binafsi kwanza siamini kabisa kuwa wanaoitwa Wayahudi na wanaoishi kwenye nchi ya Israeli siyo Wayahudi wa kuzaliwa.Hapa ninamaanisha kwamba hao akina Netanyahu siyo wayahudi wa damu.Kwa lugha nyingine hao siyo watoto wa Yakobo....

Hao ni njama au mbinu ya Shetani kusababisha vurugu na kuchanganya watu tu.Hawa Wayahudi wameshiriki katika kuleta mabalaa mengi sana duniani,hakuna uhusiano wowote ule wa hawa wanaoitwa Wayahudi wa leo na wale wa kale kwa namna yoyote ile....

Kwa maana hii jibu la swali lako kuwahudu linakuwa tofauti kwasababu hiyo...

Kuhusu Da Vinci.....

Huyu jamaa,kama ambavyo mambo mengi yaliyoanzishwa na vyama vya siri kwa kushirikiana na kizazi cha nyoka kilichopo duniani hivi sasa na kinakua kwa kasi kabisa ni kwamba malengo yote yana lengo la kuleta vurugu duniani kuhusu watu wanotaka kumfuata na kumtii Mungu....

Wanataka mshindwe kujua ukweli ni upi.Mungu ni mwaminifu sana tena sana na ndiyo maana wapo watu wanaotyoa maisha yao ili kuweka yote haya mbele ya hadhira ili ukweli ujulikane angalau hata kidogo....

Vurugu alizosababisha huyu jamaa ni kubwa sana lakini msingi wake ni uongo mkubwa sana.Ukisoma vitabu vilivyotokana na uongo huu unaweza kushangaa sana.Dhana zipo nyingi tu lakini hakuna ukweli wowote ule....

Da Vinci hakuwahi kujua chochote kilicho sirini mwa Mungu bali anajua yaliyo sirini mwa Shetani na anatumia uwezo huo kuvuruga mambo tu....

Kwa hiyo lengo lake ni kuwavuruga watu wa Mungu na wale wanotaka kumfuata kwa kutengeneza uwongo kama huu....
 
Back
Top Bottom