Nini maana ya kumpa mtoto jina Junior?

Nini maana ya kumpa mtoto jina Junior?

Arusha ndio sana kwa wana apolo.
Na linatumika kama jina kamili.
Ni kutokana na kutoelewa na elimu ndogo.

ati nini?
kwa hiyo wote
tulioita watoto junior
tuna elimu ndogo?huo ni uamuzi
wa mtu,siwezi kuita mtt jina la babu yake
eti hamisi,awe na tabia kama za hamisi?akhaaa!!
na junior ina maana nzuri tu wewe ndio hukuelewa!!
kila kitu kimeongelewa hapo juu,pleeeees!!!
 
Kwanini umuite mtoto wako jina sawa na la kwako? Nao ni umbumbu pia.........

acha ushamba wewe!unataka kunambia wewe hujivunii jina lako?utakuwa na majina yale ya matukio kama matatizo,majuto,chausiku n.k.mm nalipenda jina langu na siku zote nitapambana kimaisha ili one day mwanangu anifanye kuwa role model wake and so ajivunie kutumia jina langu.nitafurahi kujisoma mwenyewe kwa mwanangu na nitajitahidi kumfanya ajivunie mm kuwa baba yake.itz a matter of kujiamini na sio ushamba
 
Nimemsikia mtu mwanawe jina Junior ndio jina kabisa. Hana jengine.

Ni katika kuiga tamaduni za watu bila ya kuzielewa tu

Kuna mtu nilipata shida ya kumuelewesha kuwa Junior sio jina ni utambulisho wa mtu anayetumia jina moja na mzazi wake akakataa kabisa. alikuwa amepata mapacha mooja anaitwa Joven na huyo mwingine Junior nimebaki nikishangaa kila siku.
 
Mimi nafikiri Junior si Jina bali ni "kielezi" (kwa wale waliochukua somo la Kiswahili), kinachoonesha kuwa kuna mtu mwingine katika familia hiyo aliyemtangulia huyo mtoto (au mtu mzima) kupata jina hilo. Kuna watu wanapewa majina ya Babu zao wakati babu zao wangalipo hivyo ni kutofautisha babu na mjukuu wake.

Kwa wazungu jina Juniour (jr) halisimami pekee bali linaambatana na jina halisi. Mfano Rais wa Marekani Kabla ya Clinton anitwa George Bush (bado anaishi) lakini ana mtoto anatwa George Bush ambaye ni Rais wa Marekani kabla ya Obama. Kwa hiyo tunapata majina mawili George Bush (Sr) na George Bush (Jr) ili kuwatofautisha.

Ni maajabu kumpa mtoto jina Junior wakati katika familia ile hakuna mtu mwingine mwenye jina kama hilo. Ila kwa utamaduni wetu tuliojijengea wa "Copy and paste" basi kila kitu tunachukulia ni sawa.
 
Nimemsikia mtu mwanawe jina Junior ndio jina kabisa. Hana jengine.

Ni katika kuiga tamaduni za watu bila ya kuzielewa tu

tatizo lenu kimewauma sana,kwani unavomuita si ili kumpa identity nyie mnaokazania kulitafsiri jina ili iweje?binafsi sina mtoto anaeitwa juniour lakin nawatetea,kwani mtu anaeitwa mwanahamisi,mwanaisha mwanahawa ni kweli kuwa babaa yake au mama yake anaitwa hamisi au mama hawa?its just a matter of identity,ila wanakuwaga watundu sana siadvice wapewe jina hilo
 
Mimi nafikiri Junior si Jina bali ni "kielezi" (kwa wale waliochukua somo la Kiswahili), kinachoonesha kuwa kuna mtu mwingine katika familia hiyo aliyemtangulia huyo mtoto (au mtu mzima) kupata jina hilo. Kuna watu wanapewa majina ya Babu zao wakati babu zao wangalipo hivyo ni kutofautisha babu na mjukuu wake.

Kwa wazungu jina Juniour (jr) halisimami pekee bali linaambatana na jina halisi. Mfano Rais wa Marekani Kabla ya Clinton anitwa George Bush (bado anaishi) lakini ana mtoto anatwa George Bush ambaye ni Rais wa Marekani kabla ya Obama. Kwa hiyo tunapata majina mawili George Bush (Sr) na George Bush (Jr) ili kuwatofautisha.

Ni maajabu kumpa mtoto jina Junior wakati katika familia ile hakuna mtu mwingine mwenye jina kama hilo. Ila kwa utamaduni wetu tuliojijengea wa "Copy and paste" basi kila kitu tunachukulia ni sawa.

sasa si bora hata hilo linajulikana linamaana yaani tafsiri jee hayo ambayo hayana tafsiri,achen hizo,jina kama masawe,mushi nk samahann yana maana gani
 
Siku hizi umezuka mtindo wa baadhi ya watu kuwaita watoto wao Junior. Kwa ninavyoelewa mimi junior ni mamlaka ambayo iko chini ya mamlaka nyingine juu yake (senior). Sasa ni nini mantiki ya kuwapa watoto jina hilo? Au wanamaanisha sawa na kulivyokuwa George Bush baba akiwa raisi, then mwanawe alipokuwa raisi ikabidi watu wawe wananrefer kama Bush junior?
Sasa mimi huku unakuta naitwa Maiko Masamaki, mwanangu namuita Junior!, junior what? Kama yeye ni junior kwangu, mimi si junior kwa baba yangu pia? Au ukoo unaanzia kwangu? Hivi G. Bush "Junior" angekuwa na mtoto nae akaitwa G. Bush, alafu akaja kuwa raisi ataitwaje, Junior square au?
Alafu ni kwa nini mara nyingi ni watoto wa kiume tu wanaitwa Junior?!!! Wa kike hawawezi kuwa junior kwa mama zao?

Kipi unataka ujibiwe ? "Swali lako ni lipi Haswa " au umetutolea Maelezo 2 .
 
sasa si bora hata hilo linajulikana linamaana yaani tafsiri jee hayo ambayo hayana tafsiri,achen hizo,jina kama masawe,mushi nk samahann yana maana gani

Nafikiri majina yote (au mengi) ya kibantu au kitamaduni yana maana yake. Nitakupa mfano wa baadhi ya majina ya kihaya "Ishengoma maana yake Kulwa, Nyangoma pia ni kulwa lakini wa Kike. Tibaijuka maana yake "Hawakumbuki" hasa waliokutendea mabaya, Tibaigana maana yake "hawalingani". Rutashobya maana yake "Asiyekosea nk.
Tatizo ni kwa majina ya kizungu. Mfano George maana yake ni nini?
 

ati nini?
kwa hiyo wote
tulioita watoto junior
tuna elimu ndogo?huo ni uamuzi
wa mtu,siwezi kuita mtt jina la babu yake
eti hamisi,awe na tabia kama za hamisi?akhaaa!!
na junior ina maana nzuri tu wewe ndio hukuelewa!!
kila kitu kimeongelewa hapo juu,pleeeees!!!

Jina Junior ni zuri kwa mtoto akiwa bado dogo.
Kama ni jina la kujitegemea, bora ungemwita Senior.
Imagine akiwa bro halafu madogo wanamwita Junior!
Hapo ni sawa na kumpa mtoto jina Shida au Tabu.
Bora ku stick na conventional names kuliko ku take chances.
Kama Mwislam, pick from the Quran.
Kama Mkristo, pick from the bible.
Mwishowe mtawaita watoto wenu majina ya ajabu.
Mbona usingemwita Scooby Doo, Tom and Jerry, Undertaker....
 
mnanikumbusha mbali.kuna dada mmoja alimwita mtoto wake neighbour,bila kujua maana yake.alivyoulizwa alisema hilo neno alilisikia na alilipenda kwa sababu la kingereza na lina sound vizuri.baadae akauliza maana yake anajua hajui.alivyoambiwa maana alisema haijalishi yeye ameshapenda,kwa hiyo mtoto wake anaitwa neighbour
 
Pia mmenikumbusha kuna mtoto wa kimasai anaitwa Doctor, kisa mama yake baada ya kujifungua hospitalini aliskia doctor akiitwa akalipenda jina so mtoto anaitwa doctor na ndo common name alivyoandikishwa hata shule.
 
Sasa mkuu huoni huo utakuwa ubinafsi? Kwa nini umuite mtoto wako jina lako mwenyewe?!!! Maana kama wewe unaitwa Maiko, ukamuita mwanao Maiko, je na yeye akiamua kumuita mwanaye Maiko, huyo mwanae ataitwa Maiko jr jr?..,

Sijaona ubinafsi kwa maana uridhishaji wa majini ni kitu kilichozoeleka si katika jamii za kiafrika tu bali karibu duniani kote jambo hili linatokea. Kuna wazazi wanaopenda kuenzi majina ya wazazi, mababu nk. Mimi mwenyewe my son nimembatiza jina langu la kwanza ndio heshima niliyokusudia kumwenzi mtoto wangu na kwa kuwa he is my first born na mama yake alikazania hivyo. Kwamba ni ubinafsi ni mtazamo wako na upeo wako kwani kila mtu ana namna yake anayotaka kuienzi familia yake. Thanks.
 
tatizo lenu kimewauma sana,kwani unavomuita si ili kumpa identity nyie mnaokazania kulitafsiri jina ili iweje?binafsi sina mtoto anaeitwa juniour lakin nawatetea,kwani mtu anaeitwa mwanahamisi,mwanaisha mwanahawa ni kweli kuwa babaa yake au mama yake anaitwa hamisi au mama hawa?its just a matter of identity,ila wanakuwaga watundu sana siadvice wapewe jina hilo

Mbona huyu anaitwa Junior do Santos?
 
sio hao tu, kuna wanaowaita/batiza watoto wao family names za wazungu mf. Clinton, Smith na kadhalika.
Najua wengine wanachagua hivyo kwakuwa baadhi ya watu ni role models wao, mf William Clinton, lakini ukimuita mwanao Clinton, inaweza kumaanisha mdogo wake Bill na sio Bill Cllinton
 
wengi siku hizi wanarithisha wanao majina yao ya kwanza....
kama mume anaitwa Edmund na mwanaye atataka aitwe Edmund.... ndo jina la Junior linapoanzia.
Kwa vile tumezoea kumwita mtu kwa jina moja, ukiita Edmund baba ataitika, kwa hiyo mnabaki kuita Junior. hilo jina sasa ndo linakua kiasi kwamba jina halisi linapotea. kwa vile hayo yapo mengi, ndo maana tumekuwa na maJunior wengi.
Ila mimi huwa najiuliza kitu kimoja, yaani katika majina yoote hapa duniani mtu hajaona jina la kumfaa mwanaye zaidi ya jina lake?
na je inapotokea unakuwa na watoto wa kiume wa2, yule mwingine ambaye siyo Junior anajisikiaje?
Sisi tulikataa kabisa kurithisha mtoto yeyote jina la yeyote, kila mtoto amepewa jina lake mwenyewe.
 
sio hao tu, kuna wanaowaita/batiza watoto wao family names za wazungu mf. Clinton, Smith na kadhalika.
Najua wengine wanachagua hivyo kwakuwa baadhi ya watu ni role models wao, mf William Clinton, lakini ukimuita mwanao Clinton, inaweza kumaanisha mdogo wake Bill na sio Bill Cllinton
ha haaa, fanya hima rafiki nimeandaa jina Blair..... unalionaje? atabamba mtoto siyo mchezo
 
Back
Top Bottom