Nini Kumbukumbu Yako Ya Baba Wa Taifa?

Watanzania bwana, mnaongelea ya kumkumbuka mwalimu tu, ongeleeni mmefanya nini kumuenzi mwalimu? Sisi wote kwa kisi kikubwa ni wasaliti wa yale aliyotufundisha Mwalimu.

Sioni hata sababu ya kufurahia siku ya kifo chake, mimi huwa
ni siku ambayo ninaona aibu kwamba siwezi kuyatimiza yale yote niliyokuwa naimba nikiwa kijana, nikiwa chipukizi wa Nyerere, na badala yake naona wote sasa tumejaa ubinafsi tu.

Labda leo mtamkumbuka vizuri Mwalimu kwa kutoa sehemu ya ulicho nacho na kuwasaidia Watanzania wenzetu, ndugu zetu na majirani zetu ambao ni hoi kuliko sisi.

Nakaeribisha mashambulizi.

Si unatuona tunavyochakarika hapa JF kupinga ufisadi, ula rushwa na kusaini mikataba mibovu isiyo na maslahi kwa Watanzania iliyofanywa katika awamu ya Mkapa na inayoendelea katika awamu ya Kikwete. Unadhani kuwashinikiza viongozi katika hayo ni dogo? Tunayoyafanya yanatosha kabisa kumuenzi Mwalimu maana hata yeye angekuwa hai angeyakemea kwa nguvu zake zote.
 
Game theory,
1. Ndiyo napinga kabisa kuwa Nyerere aliturudisha nyuma miaka 50 kwa sababu hakuna kipimo bora zaidi kama ranking ya nchi yetu ktk Umaskini duniani. Leo hii tumesimama mbele ya mataifa mengi ktk Umaskini kuliko wakati wowote ule, hata Rwanda, Sudan na Ethiopia wako mbele yetu. It never been worse like this.
Kumbuka tu tunapoona sisi tunakwenda mbele nchi nyinginezo pia zinakwenda mbele. Kuna wakati huona Picha za Tanzania ktk TV huwa nashindwa kuamini kama kweli hiyo ni Bongo, kumbe kweli Bob!
2. Kama lilivyo jina lako.... YES nakubaliana sana na AZIMIO la ARUSHA isipokuwa game theory mbovu. Kuweka maelezo haya ktk mwanga mzuri ni hivi. Lengo la Azimio la Arusha lilikuwa zuri sana isipokuwa makosa ni ktk formation tulichukua kutafuta ushindi kama ilivyo ktk mchezo wa Mpira. Kocha anaweza kuwa na makosa ktk kupanga wachezaji, formation tunayotumia pia uwezo mdogo na vipaji vya wachezaji. Kwa hiyo lawama kubwa zinamfuata Kocha ambaye ni Nyerere lakini nasi Wadanganyika tulikuwa ni mchango mkubwa wa kutofanikiwa huko. Na kama alivyosema Mtanzania hapo juu..Tumejifunza kitu gani kutokana na mafanikio ama makosa yale.. ZERO, zero kwa sababu wengi wetu tunaamini kuwa Nyerere ndiye alikuwa mkosa pekee.
Leo hii hakuna kati yetu anayeweza kujibu swali la Mtanzania!.. Tumefanya nini kumuenzi Nyerere?...nothing - zero, yet most of us admit he was a true leader! - AIBU TUPU!
Haya ni mawazo yangu na mtazamo wangu sii lazima yakubalike na kila mtu.
 
BOB, kitu kikubwa ambacho nadhani walio wengi tunashindwa kuelewa ni kwamba Nyerere alikuwa binadamu kama wengine. Au kwamba ukiwa kiongozi unakuwa tofauti na wengine. Nchi yetu TZ hatuongozwi na wala hatutegemei kupata viongozi walio tofauti na sisi kutoka sayari nyingine (BOB, you once said..leadership ni reflection ya sisi wenyewe wananchi). kwa hiyo kama na sisi tulivyo na ubinafsi, kujipendelea na familia zetu, kuwa wanafiki nk, na viongozi wetu wako hivyo hivyo! Jiulize kwa nini wewe uliondoka TZ? ni kwa sababu ya kutafuta maisha kwingine kwa ajili yako na familia yako! kwa hiyo hata hawa viongozi wetu wanamatamanio hayo hayo ya kuwapeleka watoto wao huko ughaibuni, kuendesha magari mazuri nk.

Now, can you get a leader ambaye hayataki mambo wewe unayoyataka ya anasa? hapana! hata sisi kama wananchi tunajua fika kwamba viongozi wetu ni kama sisi, kwa hiyo tunachotaka kutoka kwao ni kuwa na zile minimum standards kusudi wananchi nao wajiletee maendeleo. ni dhahiri kwamba hata huko ulaya na USA viongozi wanaiba, lakini tofauti na sisi wanaiba harafu wanainvest ndani humo humo huku wakizalisha ajira, na wanaiba huku wakiwafikiria watu wao watafaidika vipi, sisi viongozi wetu wanaiba huku wakikimbilia nje, as a result sisi na wao wenyewe hatufaidiki, ila wanafaidika wengine.

Nyerere alikuwa ni bin adam just like you and me, ila sema alikuwa na kipaji cha pekee hakujiweka mbele kuliko wengine na alijaribu KWA NIA NJEMA kujenga mazingira ya wote kufanikiwa (kwa kutoa huduma za muhimu sawa na bure kama elimu, afya nk). Leo hatutegemei JK awe Nyerere, lakini tunategemea hulka ya ubinadam aliyonayo kama wengine ajitahidi atumie zile raslimali tulizonazo kusudi na sisi tujikomboe. So far ameshindwa.
Kama alivyosema BOB, bila ubepari dunia haiwezi kuwa dunia unayoiona na unayoifaidi. Wanaosema kwamba another world is possible, nachelea kukubaliana nayo, hiyo alternative world inawezekana tuu endapo viongozi wataweka mikakati sahihi na kuwaempower wananchi kufaidi raslimali zao, hatuwezi kuendelea kulaumu globalization. I have always said and I will say it again, African Problems emanate from Africans! wazungu wana nafasi ndogo saana katika haya masaibu yayotukuta. Yaani mi nafikiriaaaa mpaka naona kwamba Africa sijui tusaidiwe au tujisaidie vipi!!ahahahah...
 
Game theory,
1. Ndiyo napinga kabisa kuwa Nyerere aliturudisha nyuma miaka 50 kwa sababu hakuna kipimo bora zaidi kama ranking ya nchi yetu ktk Umaskini duniani. Leo hii tumesimama mbele ya mataifa mengi ktk Umaskini kuliko wakati wowote ule, hata Rwanda, Sudan na Ethiopia wako mbele yetu. It never been worse like this.
Kumbuka tu tunapoona sisi tunakwenda mbele nchi nyinginezo pia zinakwenda mbele. Kuna wakati huona Picha za Tanzania ktk TV huwa nashindwa kuamini kama kweli hiyo ni Bongo, kumbe kweli Bob!
2. Kama lilivyo jina lako.... YES nakubaliana sana na AZIMIO la ARUSHA isipokuwa game theory mbovu. Kuweka maelezo haya ktk mwanga mzuri ni hivi. Lengo la Azimio la Arusha lilikuwa zuri sana isipokuwa makosa ni ktk formation tulichukua kutafuta ushindi kama ilivyo ktk mchezo wa Mpira. Kocha anaweza kuwa na makosa ktk kupanga wachezaji, formation tunayotumia pia uwezo mdogo na vipaji vya wachezaji. Kwa hiyo lawama kubwa zinamfuata Kocha ambaye ni Nyerere lakini nasi Wadanganyika tulikuwa ni mchango mkubwa wa kutofanikiwa huko. Na kama alivyosema Mtanzania hapo juu..Tumejifunza kitu gani kutokana na mafanikio ama makosa yale.. ZERO, zero kwa sababu wengi wetu tunaamini kuwa Nyerere ndiye alikuwa mkosa pekee.
Leo hii hakuna kati yetu anayeweza kujibu swali la Mtanzania!.. Tumefanya nini kumuenzi Nyerere?...nothing - zero, yet most of us admit he was a true leader! - AIBU TUPU!
Haya ni mawazo yangu na mtazamo wangu sii lazima yakubalike na kila mtu.

Na mimi nimeagree to disagree na wewe.Na nitaheshimu mawazo yako kuhusu Nyerere japo sikubaliani nayo
 
Ulilipa kodi kiasi gani kumjengea mwalimu hiyo nyumba, au umeamua kuleta uzushi tu?



DUA
kwa faida ya FORUM sitkujibu thread yako yoyote ile kwani mabishano na matusi yako uliyoyatoa kwangu mara ya mwisho ni kithibitisho kuwa hutaki kujadiliana bali unataka shari na frankly speaking i dont have time na drama zako

ADMIN:

Kwa mara nyingine tunaomba IGNORE LIST facility ili tuweze kuepusha mamabo kama haya

 
BOB, kitu kikubwa ambacho nadhani walio wengi tunashindwa kuelewa ni kwamba Nyerere alikuwa binadamu kama wengine. Au kwamba ukiwa kiongozi unakuwa tofauti na wengine. Nchi yetu TZ hatuongozwi na wala hatutegemei kupata viongozi walio tofauti na sisi kutoka sayari nyingine (BOB, you once said..leadership ni reflection ya sisi wenyewe wananchi). kwa hiyo kama na sisi tulivyo na ubinafsi, kujipendelea na familia zetu, kuwa wanafiki nk, na viongozi wetu wako hivyo hivyo! Jiulize kwa nini wewe uliondoka TZ? ni kwa sababu ya kutafuta maisha kwingine kwa ajili yako na familia yako! kwa hiyo hata hawa viongozi wetu wanamatamanio hayo hayo ya kuwapeleka watoto wao huko ughaibuni, kuendesha magari mazuri nk.

Now, can you get a leader ambaye hayataki mambo wewe unayoyataka ya anasa? hapana! hata sisi kama wananchi tunajua fika kwamba viongozi wetu ni kama sisi, kwa hiyo tunachotaka kutoka kwao ni kuwa na zile minimum standards kusudi wananchi nao wajiletee maendeleo. ni dhahiri kwamba hata huko ulaya na USA viongozi wanaiba, lakini tofauti na sisi wanaiba harafu wanainvest ndani humo humo huku wakizalisha ajira, na wanaiba huku wakiwafikiria watu wao watafaidika vipi, sisi viongozi wetu wanaiba huku wakikimbilia nje, as a result sisi na wao wenyewe hatufaidiki, ila wanafaidika wengine.

Nyerere alikuwa ni bin adam just like you and me, ila sema alikuwa na kipaji cha pekee hakujiweka mbele kuliko wengine na alijaribu KWA NIA NJEMA kujenga mazingira ya wote kufanikiwa (kwa kutoa huduma za muhimu sawa na bure kama elimu, afya nk). Leo hatutegemei JK awe Nyerere, lakini tunategemea hulka ya ubinadam aliyonayo kama wengine ajitahidi atumie zile raslimali tulizonazo kusudi na sisi tujikomboe. So far ameshindwa.
Kama alivyosema BOB, bila ubepari dunia haiwezi kuwa dunia unayoiona na unayoifaidi. Wanaosema kwamba another world is possible, nachelea kukubaliana nayo, hiyo alternative world inawezekana tuu endapo viongozi wataweka mikakati sahihi na kuwaempower wananchi kufaidi raslimali zao, hatuwezi kuendelea kulaumu globalization. I have always said and I will say it again, African Problems emanate from Africans! wazungu wana nafasi ndogo saana katika haya masaibu yayotukuta. Yaani mi nafikiriaaaa mpaka naona kwamba Africa sijui tusaidiwe au tujisaidie vipi!!ahahahah...

na je unakubali kuwa Nyerere akuwa divisive figure especially kwa jinsi alivyooachia CANCER ya UDINI kusambaa?
 
GT taratibu mzee!

MASANJA

nasema haya kwa sababu nishaongea na wahusika in Private namna ya kuondokana na confrontration kama hizi lakini naona softly softly approach inanishinda

the easiest way ni Invisible atuwekee IGNORE BUTTON ambayo itakuwa rahisi mtu ukawaweka watu ambao unajaribu kuepusha mtafaruku nao. Hiyo kwanza itakuwa rahisi hutosoma posts zao na maisha yanaweza yakawa simple

 

the easiest way ni Invisible atuwekee IGNORE BUTTON ambayo itakuwa rahisi mtu ukawaweka watu ambao unajaribu kuepusha mtafaruku nao. Hiyo kwanza itakuwa rahisi hutosoma posts zao na maisha yanaweza yakawa simple

Mkuu ndio naingia mjini penye mtandao. Nilikuwa nje kabisa ya mtandao. Natambua kuna mengi ya kushughulikia na naanza moja baada ya jingine. Kuna malalamiko mengi lakini nakuhakikishia kuwa kufikia Jumanne yatakuwa yametafutiwa ufumbuzi. Kumradhi kwa kuchelewa kutoa jibu ama suluhu ya tatizo lako.

Invisible
 

na je unakubali kuwa Nyerere akuwa divisive figure especially kwa jinsi alivyooachia CANCER ya UDINI kusambaa?

GT,

Hiyo cancer ya UDINI iko wapi? Mbona hatukucharazana mapanga kama kulikuwa na matatizo makubwa ya udini kiasi hicho? Hebu fafanua. Nawafahamu Waislamu wengi sana ambao hawakuona matatizo yoyote ya Nyerere katika kuwanyanyasa waislamu na hawa ni wengi wao, na wako wachache ambao walikuwa wakilalama kwamba Nyerere aliwabagua Waislamu. Tafadhali naomba ufafanue kuhusi kusambaa kwa cancer ya UDINI na madhara yake katika nchi yetu.
 
GT naheshimu sana mawazo yako mkuu, lakini kwa kweli swala kwamba Nyerere alikuwa divisive limeniacha na MASIKITIKO sana. Maana mi nimesoma shule ya mission (shule ys Askofu) dini zote tulikuwa tunapewa haki SAWA!! every Friday kulikuwa na chumba kikuuubwa kwa ajili ya waislamu (nakumbuka hata gari la shule lilikuwa linawapeleka waislamu mjini kwenye ibada ya Idd, NA KUWARUDISHA JIONI BAADA YA SHEREHE NA WAISLAMU WENZAO).., Jmosi it was a special day kwa wasabato, kifupi tulikuwa tunaishi kama familia na mimi huu udini nimeanza kuusikia leo baada ya kufika Dar Es Salaam! (Na mind you mi nimefika DAR kwa mara ya kwanza nakuja kusoma Mlimani)! kwamba waislam wanaonewa, na mambo kibao!

Kama nilivyosema, Nyerere alikuwa ni kiumbe kama mimi na wewe, lakini what I can for sure tell you baada ya utawala wake hatujawahi kupata kiongozi BORA kama yeye mpaka leo, labda atokee baadaye vizazi vijavyo. Leo baada ya kunufaika na sera zake za UJAMAA tukapata elimu na mengineyo ndo tunaona huyu mzee hafai. lakini alijua mtoto wa Mkulima kwa kumsaidia Mpe ELIMU and fortunately na mimi mpaka leo naamini kabisa ELIMU ndo mkombozi wa mtoto wa maskini (maana I have been there!). When I go back to see my kinsmen, kweli msaada wangu ni KARO PALE NINAPOWEZA!
 
Mkuu ndio naingia mjini penye mtandao. Nilikuwa nje kabisa ya mtandao. Natambua kuna mengi ya kushughulikia na naanza moja baada ya jingine. Kuna malalamiko mengi lakini nakuhakikishia kuwa kufikia Jumanne yatakuwa yametafutiwa ufumbuzi. Kumradhi kwa kuchelewa kutoa jibu ama suluhu ya tatizo lako.

Invisible

sawa mzee nimekusikia ni kweli ni bora kushghulia mja baada ya lingine
 
Mkuu ndio naingia mjini penye mtandao. Nilikuwa nje kabisa ya mtandao. Natambua kuna mengi ya kushughulikia na naanza moja baada ya jingine. Kuna malalamiko mengi lakini nakuhakikishia kuwa kufikia Jumanne yatakuwa yametafutiwa ufumbuzi. Kumradhi kwa kuchelewa kutoa jibu ama suluhu ya tatizo lako.

Invisible

GT,

Hiyo cancer ya UDINI iko wapi? Mbona hatukucharazana mapanga kama kulikuwa na matatizo makubwa ya udini kiasi hicho? Hebu fafanua. Nawafahamu Waislamu wengi sana ambao hawakuona matatizo yoyote ya Nyerere katika kuwanyanyasa waislamu na hawa ni wengi wao, na wako wachache ambao walikuwa wakilalama kwamba Nyerere aliwabagua Waislamu. Tafadhali naomba ufafanue kuhusi kusambaa kwa cancer ya UDINI na madhara yake katika nchi yetu.

GT naheshimu sana mawazo yako mkuu, lakini kwa kweli swala kwamba Nyerere alikuwa divisive limeniacha na MASIKITIKO sana. Maana mi nimesoma shule ya mission (shule ys Askofu) dini zote tulikuwa tunapewa haki SAWA!! every Friday kulikuwa na chumba kikuuubwa kwa ajili ya waislamu (nakumbuka hata gari la shule lilikuwa linawapeleka waislamu mjini kwenye ibada ya Idd, NA KUWARUDISHA JIONI BAADA YA SHEREHE NA WAISLAMU WENZAO).., Jmosi it was a special day kwa wasabato, kifupi tulikuwa tunaishi kama familia na mimi huu udini nimeanza kuusikia leo baada ya kufika Dar Es Salaam! (Na mind you mi nimefika DAR kwa mara ya kwanza nakuja kusoma Mlimani)! kwamba waislam wanaonewa, na mambo kibao!

Kama nilivyosema, Nyerere alikuwa ni kiumbe kama mimi na wewe, lakini what I can for sure tell you baada ya utawala wake hatujawahi kupata kiongozi BORA kama yeye mpaka leo, labda atokee baadaye vizazi vijavyo. Leo baada ya kunufaika na sera zake za UJAMAA tukapata elimu na mengineyo ndo tunaona huyu mzee hafai. lakini alijua mtoto wa Mkulima kwa kumsaidia Mpe ELIMU and fortunately na mimi mpaka leo naamini kabisa ELIMU ndo mkombozi wa mtoto wa maskini (maana I have been there!). When I go back to see my kinsmen, kweli msaada wangu ni KARO PALE NINAPOWEZA!

someni thread hii

http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=1099
 
ny10st4.jpg


Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (RIP)



ny09np8.jpg


Siku mwili wa Marehemu Mwl J.K. Nyerere
uliporejeshwa Tanzania kutoka UK.


ny08ap7.jpg



nyo4aa1.jpg


Nyumba aliyojengewa Mwalimu baada ya kustaafu.


ny07wm1.jpg

Sanamu ya Mwalimu ikiwa sehemu ambayo alipozaliwa huko kijijini Mwintongo, Butiama

Pictures: Credit Michuzi blog
 
Katika kumkumbuka Baba wa taifa, naomba mchangie kumbukumbu zenu binafsi au zinginezo mlizonazo za hayati Mwalimu.

Nianze mwenyewe: wakati niko mtoto mdogo mwanzoni mwa miaka ya themanini...

Haya washirika wenzangu tuendelee.....

...pamoja na mengi mazuri, mimi namkumbuka na kile kifimbo chake...!

...tangu nipo shule miaka hiyo uloitaja kulikuwepo na hadithi nyingi za ajabu na kweli kuhusu kifimbo kile,

...Sijui kipo makumbusho gani tu nikakiangalie tena(I hope hajazikwa nacho!)
 
ny03ac1.jpg

Mwalimu atakumbukwa daima kama kiongozi wa mfano,
sio wa kushika kiuno na kuamrisha.................


ny01jm6.jpg



Mwalimu akiwa na Samora Machel (RIP), Graca Machel (Mke wa rais mstaafu wa SA Nelson Mandela hivi sasa) na maria Nyerere enzi hizo baada ya ukombozi wa Musumbiji

ny02op3.jpg


Mwalimu akiongozana na mawakili wake wakielekea mahakama ya Kivukoni ambako alipanda kizimbani baada ya kushtakiwa kwa kosa la kutaka kusababisha vurugu baada ya kuandika kile kilichoonekana maneno ya uchokozi kwenye gazeti la tanu ambapo alimsema dc mmoja ambaye alikasirika na kumshitaki. Mwalimu alipatikana na hatia ya kuandika uchochezi na kutozwa faini ambayo ilipwa na wanachama wa TANU
waliopigisha bonge la harambee.

Pictures: Credit Michuzi Blog
 
ny06gf8.jpg


Jengo ambalo ndani yake mna kaburi la Mwalimu.

ny05va7.jpg


Kaburi la Mwalimu hutembelewa kila siku na wadau mbalimbali.

Pictures: Credit Michuzi Blog
 
Tutaongea mengi sana kuhusu mwalimu,lakini ukweli unabaki palepale,itapita miaka mingi kwa Tanzania kuja kupata kichwa kama kile,hivi utamlinganisha Nyerere na manyang'au wa siku hizi?
Hatukatai Nyerere alikua na mapungufu kama binadamu mwingine yeyote yule,hata mwenyewe aliwahi kukiri kuwa kuna makosa alifanya kama kiongozi kwani hakua malaika,.Ila kaleta mengi sana,ukilinganisha na mapungufu,najua huwezi kupendwa na wote,pia huwezi kukubalika na wote,kwani hata Yesu mwana wa Mungu alipingwa na kusulubiwa sembuse Nyerere.

Mie nakuulizeni hapo ulipo umeifanyia nini Tanzania?Au kulaumu tu,Nyerere kaleta umaskini,maendeleo hayaletwi na mtu mmoja,kama jamii nzima tulikua tunategemea Nyerere ndiye atuletee maendeleo basi mmepotea njia.Alitupa elimu bure ili tuelimike tuje kujikomboa wenyewe,ila cha ajabu elimu aliyotupa ya bure,badala ya kutusaidia,imekuwa mbadala,sasa tunaitumia kuuza nchi,mikataba fake,kutelekeza watanzania Ukraine,ebwana mna mambo ya mzaha,yaani ukisema Nyerere ndo katuletea umaskini,mie sitakutofautisha na Ze Comedy,naona kama vile unaigiza tu.Watanzania tupo milioni 40,je niambie ni nani na kaifanyia nini Tanzania,unaweza kujitolea mfano mwenyewe?Wote ubinafsi umetujaa tu,acheni mzee wa watu apumzike,Mungu asije kutulaani bure,kweli nabii hakubaliki kwao.
 
Uko huru kuchangia lakini baki kwenye mada..
Unapoanza kuzungumzia mambo yaliyo nje ya mada ni bora uanze thread mpya la sivyo topiki nzima itachukua detour na kupoteza lengo na mwelekeo kabisa

Sawa mkuu, mimi nina mawazo tofauti sana juu ya hii mijadala ya JF. Mimi naona mijadala ya maana ni ile ile ambayo inachukua a much broader perspective na sio narrow approach ambayo unashauri tufuate. Ndio maana hata siku moja siwezi kumwambia mtu unatoka nje. Hata siku moja creativity haiji kwenye mijadala ya aina hiyo.

Kama ni hivyo sina la kuongea kwenye mjadala huu ili nisije nikatoka nje.
 
Back
Top Bottom