BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Watanzania bwana, mnaongelea ya kumkumbuka mwalimu tu, ongeleeni mmefanya nini kumuenzi mwalimu? Sisi wote kwa kisi kikubwa ni wasaliti wa yale aliyotufundisha Mwalimu.
Sioni hata sababu ya kufurahia siku ya kifo chake, mimi huwa
ni siku ambayo ninaona aibu kwamba siwezi kuyatimiza yale yote niliyokuwa naimba nikiwa kijana, nikiwa chipukizi wa Nyerere, na badala yake naona wote sasa tumejaa ubinafsi tu.
Labda leo mtamkumbuka vizuri Mwalimu kwa kutoa sehemu ya ulicho nacho na kuwasaidia Watanzania wenzetu, ndugu zetu na majirani zetu ambao ni hoi kuliko sisi.
Nakaeribisha mashambulizi.
Si unatuona tunavyochakarika hapa JF kupinga ufisadi, ula rushwa na kusaini mikataba mibovu isiyo na maslahi kwa Watanzania iliyofanywa katika awamu ya Mkapa na inayoendelea katika awamu ya Kikwete. Unadhani kuwashinikiza viongozi katika hayo ni dogo? Tunayoyafanya yanatosha kabisa kumuenzi Mwalimu maana hata yeye angekuwa hai angeyakemea kwa nguvu zake zote.