Nini Kumbukumbu Yako Ya Baba Wa Taifa?

Nini Kumbukumbu Yako Ya Baba Wa Taifa?

Tutaongea mengi sana kuhusu mwalimu,lakini ukweli unabaki palepale,itapita miaka mingi kwa Tanzania kuja kupata kichwa kama kile,hivi utamlinganisha Nyerere na manyang'au wa siku hizi?
Hatukatai Nyerere alikua na mapungufu kama binadamu mwingine yeyote yule,hata mwenyewe aliwahi kukiri kuwa kuna makosa alifanya kama kiongozi kwani hakua malaika,.Ila kaleta mengi sana,ukilinganisha na mapungufu,najua huwezi kupendwa na wote,pia huwezi kukubalika na wote,kwani hata Yesu mwana wa Mungu alipingwa na kusulubiwa sembuse Nyerere.

Mie nakuulizeni hapo ulipo umeifanyia nini Tanzania?Au kulaumu tu,Nyerere kaleta umaskini,maendeleo hayaletwi na mtu mmoja,kama jamii nzima tulikua tunategemea Nyerere ndiye atuletee maendeleo basi mmepotea njia.Alitupa elimu bure ili tuelimike tuje kujikomboa wenyewe,ila cha ajabu elimu aliyotupa ya bure,badala ya kutusaidia,imekuwa mbadala,sasa tunaitumia kuuza nchi,mikataba fake,kutelekeza watanzania Ukraine,ebwana mna mambo ya mzaha,yaani ukisema Nyerere ndo katuletea umaskini,mie sitakutofautisha na Ze Comedy,naona kama vile unaigiza tu.Watanzania tupo milioni 40,je niambie ni nani na kaifanyia nini Tanzania,unaweza kujitolea mfano mwenyewe?Wote ubinafsi umetujaa tu,acheni mzee wa watu apumzike,Mungu asije kutulaani bure,kweli nabii hakubaliki kwao.

Hawa kweli sasa wanakuwa manyang'au, walioweka mbele maslahi yao badala ya nchi, wanaojilimbizia mali kwa kasi kubwa mno kwa kutumia njia za haramu bila woga wowote, kwa kifupi wamewatekeleza Watanzania.
 
Mkuu ndio naingia mjini penye mtandao. Nilikuwa nje kabisa ya mtandao. Natambua kuna mengi ya kushughulikia na naanza moja baada ya jingine. Kuna malalamiko mengi lakini nakuhakikishia kuwa kufikia Jumanne yatakuwa yametafutiwa ufumbuzi. Kumradhi kwa kuchelewa kutoa jibu ama suluhu ya tatizo lako.

Invisible

Nashari uanze kwa kutuwekea FORUM YETU ambayo iwe closed to the public lakini open kwetu sisi ambao tna umri zaidi ya 18

na huto tuona ngo humu kwenye siasa sisi kule tutakuwa tunaangalia wapita njia tuu
 
DUA
kwa faida ya FORUM sitkujibu thread yako yoyote ile kwani mabishano na matusi yako uliyoyatoa kwangu mara ya mwisho ni kithibitisho kuwa hutaki kujadiliana bali unataka shari na frankly speaking i dont have time na drama zako

waswahili walisema Nyani haoni k******.

GAME THEORY said:
............Kodi zetu zilitumika kumjengea nyumba kwenye jiwe huko kijijini kwake lakini baada ya miezi michache aliamua kurudi Msasani......


Kama kawaida yako hoja inapokushinda lazima utafute mahali pa kukimbilia. Tunachofahamu Mwalimu alijengewa nyumba na Marehemu Samora Machel na Wananchi wa Mozambique lakini kuna wadini humu kama wewe ambao kutwa kucha kazi yao ni kuleta uzushi na maneno ya kejeli. WorM alikuwa na taa yake ya kuwamulika natumaini itairudisha ili tuendelee kuwamulika. SASA WEWE UNASEMA KODI YAKO ILIJENGA HIYO NYUMBA KWA VIPI? TUFAFANULIE?
 
waswahili walisema Nyani haoni k******.

[/SIZE]

Kama kawaida yako hoja inapokushinda lazima utafute mahali pa kukimbilia. Tunachofahamu Mwalimu alijengewa nyumba na Marehemu Samora Machel na Wananchi wa Mozambique lakini kuna wadini humu kama wewe ambao kutwa kucha kazi yao ni kuleta uzushi na maneno ya kejeli. WorM alikuwa na taa yake ya kuwamulika natumaini itairudisha ili tuendelee kuwamulika. SASA WEWE UNASEMA KODI YAKO ILIJENGA HIYO NYUMBA KWA VIPI? TUFAFANULIE?



nilishakuambia kuwa sitaki na wala sitotaka kuendelea kutukanana na wewe. Lakini mindhali una insist kunifuata fuata i am not sure how far you wanna go na huu mchezo wako

Nishavumilia vya kutosha na naona huna nia ya kujadiliana bali wewe unataka vita. Basi mimi sina tatizo na hilo lakini baadae tusilaumiane

nishawaarifu wahusika na naona inabidi sasa niende public

now the only question ni je, How far do you want this to go?
 
Kama unakubali kodi yako haikujenga nyumba ya mwalimu futa kauli yako. Hilo ndio la msingi hapa. Hakuna tusi kwenye hilo, habari uliyoandika siyo sahihi. PERIOD.
 
Kama unakubali kodi yako haikujenga nyumba ya mwalimu futa kauli yako. Hilo ndio la msingi hapa. Hakuna tusi kwenye hilo, habari uliyoandika siyo sahihi. PERIOD.

matusi uliyaanza Last week na wikiendi hii umerudia tena siongelei mambo ya kodi hapa

ndio maana nakuuliza how far do you want to take this?
 
Tumshukuru kwa kutuletea umoja na kujitahidi kufuta matabaka si tajiri au maskini si waislamu si wakristu ote tulisoma shule hizo hizo.
Kumbukumbu za/yangu itakuwa ni kipindi niko Shule ya msingi pale karibia na St Peters mimi na baadhi ya marafiki zangu tulikuwa na kawaida ya kwenda kanisani na kumsubiria Mwalimu atoke ilitupate fursa ya kumuona, na ninakumbuka kuna siku alituambia tusome kwa bidii. Na kwa wale waliopata fursa ya kusafiri naye kwenye ndege(walikuwa wanaiita CCM) Mwalimu alikuwa na kawaida ya kusalimiana na abiria wote kwenye ndege.
 

matusi uliyaanza Last week na wikiendi hii umerudia tena siongelei mambo ya kodi hapa

ndio maana nakuuliza how far do you want to take this?

Kama wewe ulitukana ulitegemea nini? Wewe umeleta hoja hapa leo ya kodi yako kujenga nyumba ya mwalimu mimi nimekwambia hiyo habari yako ni uongo na upotoshaji wa hali ya juu. Unachotakiwa ni kukubali kwamba hiyo habari sio sahihi bali unang'ang'ania kutaka kupotosha ukweli ambao hapa kwangu hupati kitu.

Weka habari sahihi hapa sio unazi na uzandiki. Anyway huna jipya hoja uliyoleta imekushinda na sina sababu ya kuendelea kuharibu hii thread ambayo wengine wanaendelea kuchangia mambo ya Mwalimu lakini JF members wote wameshaelewa ukweli nyumba ya mwalimu ilijengwa na hayati Samora na wanachi wa Mozambique.
 
Personal i had never get a chance to met Mwalim face to face, however i read a lot of his publications from Ungozi wetu na hatima ya Tanzania to many others.

I belive Mwalim was a hamble man. He had a lot of things in his mind, however he had a poor team that could not enforce anything from mwalim wishes. Many of this greed leaders we have today are the products of Mwalim team. I always ask my self many questions, did Mwalim knows that one day Tanzania will get where it is now? Did he knows about all corruptions and wizi ndani ya CCM.I never get the answers, lather i strong believe wote hawa viongozi waleo ni wanafiki na mandumi ya kuwili.

Imagine, your middle of no where, na baba yako anakufa kisha anakuachia familia wewe kama kiongozi, haujui alitafutaje pesa, aliwezaje kuwalisha na kuwaongoza, then what will you do? this is the same as Mwalim, when Tanzania was announced as independent country in 1961, We didnt have alot of PhD holders, we didnt have a lot of Teachers, No MD's. We had a lot of poor people, very poor. Mwalim at that time he believed that it won't be hard because he thought all the leaders are like him, hamble, dreamers, hard workers but it wasn't that way. Most of the leaders at that time walikuwa wabinafsi, wala rushwa, wezi and waongo. That why Mwalim strategies hazikufanikiwa.

As mwalim said "Ujamaa never failed". I always respect this leader, i dont care about all this consipirancy about Uganda war, ujamaa and many others. I always ask this people who said bad about Mwalim, "ingekuwa wewe ungefanya nini"? You will never get a straight asnwers, and some of the kids who are wining about Mwalim their fathers and family members are corrupted from head to tores.
 
Kama wewe ulitukana ulitegemea nini? Wewe umeleta hoja hapa leo ya kodi yako kujenga nyumba ya mwalimu mimi nimekwambia hiyo habari yako ni uongo na upotoshaji wa hali ya juu. Unachotakiwa ni kukubali kwamba hiyo habari sio sahihi bali unang'ang'ania kutaka kupotosha ukweli ambao hapa kwangu hupati kitu.

Weka habari sahihi hapa sio unazi na uzandiki. Anyway huna jipya hoja uliyoleta imekushinda na sina sababu ya kuendelea kuharibu hii thread ambayo wengine wanaendelea kuchangia mambo ya Mwalimu lakini JF members wote wameshaelewa ukweli nyumba ya mwalimu ilijengwa na hayati Samora na wanachi wa Mozambique.


aliyeanza matusi nani? Nimekuuliza how far do you wanna take this?




DUADOSSIERPNG.jpg
 
Kwani bila yeye, nisingeweza kufikia hapa nilipofikia katika uhai wangu kielimu; that is a fact. And that was not premised on privileged status but purely on merit.

Ahsante Mwalimu kwa Azimio la Arusha. That was a vision from a true leader of the people.

Mtu anayetafuta kumvisha Mwalimu kofia ya udini analo lake. Hata hakumbuki mabandiko yake mengi humu yanayotafuta shari za kidini kila mara! Tafuta sababu nyingine za kumdhalilisha Mwalimu, lakini sio udini.
 
game theory, nisaidie jambo moja ni nchi gani ya Kiafrika ambayo chini ya viongozi wake imefanya vizuri zaidi katika kipindi cha miaka 23 wakati Mwalimu anatawala Tanzania? Hiyo itatusaidia kuona ni nchi gani zilipiga hatua kuuuuuuuubwa ya maendeleo kuliko Tanzania ya Mwalimu ambayo imerudi nyuma miaka 50!?
 
game theory, nisaidie jambo moja ni nchi gani ya Kiafrika ambayo chini ya viongozi wake imefanya vizuri zaidi katika kipindi cha miaka 23 wakati Mwalimu anatawala Tanzania? Hiyo itatusaidia kuona ni nchi gani zilipiga hatua kuuuuuuuubwa ya maendeleo kuliko Tanzania ya Mwalimu ambayo imerudi nyuma miaka 50!?

Mwanakijiji,
Mtu yeyote unayeona anasema Mwalimu,katurudisha nyuma,ni kheri kumuonea huruma tu,maana hajui alifanyalo,na wala hamjui mwalimu hata kidogo,tunaomjua mwl,sina hata la kuongea,Narudia tunaomjua mwl,basi Mungu ndiye ajuaye alitupa mtu gani?Kweli mnadiriki kusema mwl katurudisha nyuma kwa lipi?The guy was smart,na nia yake ilikua
kumkomboa mlala hoi,ndiyo maana hata yeye alikua anaishi maisha ya kawaida kabisa,haijawahi kutokea Afrika kiongozi kuishi kama maisha alioishi Nyerere,kufanya kazi kwa vitendo.Huyu mzee amelima hadi anaenda kaburini,binafsi nitembelea nyumbani kwake Butiama mara kadhaa,alikua na mashamba makubwa sana,Nyerere alikua anaenda asubuhi shambani,na kurudi saa 8 au tisa,ambapo utamkuta anacheza
bao na wazee wenzake.Alibuni sera nzuri,alichosema ukitaka kumsaidia maskini,ukitaka kufuta umaskini,ukitaka kumkomboa kila mtanzania,basi mpe elimu,na hicho ndicho alichokifanya katupa elimu ya bure,tumesoma bure,tumetibiwa bure,hakujali upuuzi wa IMF na WB,alichojali ni mtanzania anafaidika na uhuru wa nchi yake.

Kuhusu nyumba ya Butiama,navyojua mimi,hiyo nyumba alijengewa na Jeshi,tena alilipinga sana hilo suala la ujenzi wa hiyo nyumba,alisema mimi sio tembo,haka kanyumba nilikonako kananitosha.Niambie Nyerere kachukua kodi yako ipi?Ana makampuni gani?Ana viwanja gani?Ana hisa gani?Nyerere alikua ni maskini kama sisi tu,na hakutaka kuwa tajiri,mbona kama angetaka kuwa tajiri,enzi hizo watanzania tulikua tumelala,mbona angechukua kila kitu.

Kuna siku Nyerere akiwa rais wa nchi,alienda kukopa sukari,kwenye duka la mhindi,akamwambia nikipata mshahara,nitakulipa hela yako.Yule mhindi,akasema chukua mzee hiyo sukari,sitaki uje unilipe hela,Nyerere akasema kama hutaki nije kukulipa deni lako,basi hii sukari sichukui,mie sitaki bure,nitakulipa hela yako.

Eti Nyerere alikua mdini,nyie mnaongea vitu gani jamani?
 
game theory, nisaidie jambo moja ni nchi gani ya Kiafrika ambayo chini ya viongozi wake imefanya vizuri zaidi katika kipindi cha miaka 23 wakati Mwalimu anatawala Tanzania? Hiyo itatusaidia kuona ni nchi gani zilipiga hatua kuuuuuuuubwa ya maendeleo kuliko Tanzania ya Mwalimu ambayo imerudi nyuma miaka 50!?

Afrika Kusini...(?)
 
ningequalify kuwa ukiondoa Afrika ya Kusini, kwa maana sidhani kama jinsi Afrika ya Kusini ilivyopiga hatua ya maendeleo kwenye baadhi ya miji yake ndiyo ingekuwa hatua ya Tanzania kufuata. ama?
 
Nyerere (BINAFSI)aliiga CULTURAL REVOLUTION TOKA CHINA na kuunda AZIMIO LA ARUSHA lakini kwa ubishi wake hakuiga namna ya utekelezaji.

Kufanikisha Azimio la Arusha isingewezekana bila mtulinga kama Wachina walivyokuwa wanafanya, hata nchi yao waliifungia ili kuwashughulikia raia wabishi bila kuingiliwa na mataifa ya nje. Lakini kimsingi China ilibaki masikini tokana na hizo siasa mbovu.

Hata hivyo tokana na propaganda, enzi za Mao Ze Dong au baada tu kifo chake sifa zake zilikua kemkem China nzima lakini sasa hivi utadhani hajawahi kuwepo ama utadhani China ipo chini ya chama cha upinzani.

Tofauti na enzi za Mao, wachina wamejawa na 'smiles' na 'great hopes' inayoonekana wazi wazi na kati ya viongozi wanne waliopita, wanamsifia na kumtukuza kiongozi mmoja tu na siasa zake za '.....opening to the outside.....on the long run some flies will get in......... and a few of our people will be given oportunity to get rich first....communism with Chinese characteristics...' ambae ni Deng Xiaoping. Sasa hivi China maisha ni safi na uchumi unapaa tokana na uongozi, siasa au msingi wake mahiri. He is the real great leader. Mao hana mpango. Jiang na Hu ni watekelezaji tu wa siasa zake.

Kuiga cultural revolution, kimsingi wachina walimwingiza mjini Mwl. maana hayakua mawazo yake asilia na mbaya zaidi viongozi ktk serikali ya Nyerere hawakuamini siasa za kijamaa na bado Nyerere hakufanya chochote kuwabadilisha kazi ama fikra. Propaganda za CCM zimefanya kazi kubwa sana kuweka waTZ wengi sawa mpaka wanaamini Nyerere ni kiongozi mahiri. Ukiondoa harakati za uhuru, Mwl Nyerere in real life and his leadership hakuwa wala hajawahi kuwa kiongozi bora km 'MODEL' kwani tu bado masikini. Ubora utoke wapi, bora ni yule anayetuongoza kujikomboa umasikini na kutuletea neema. Ila kwa kua nchi yetu haijawahi kutoa kiongozi bora basi Nyerere anaonekana safi kwa sababu alifanikiwa ktk baadhi ya fani km kutuletea hisia ya utaifa na si ukabila, ukombozi, bla...bla... He could do better. Na pamoja na upungugu wa kibinadamu ambao wote tunao, Deng kaperform wonders, hivyo pia kama Nyerere angeperform na ndipo kweli angekua 'REAL MODEL'.

Nyerere!!. utakomboaje NCHI nyingine kwa kutumia rasilimali chache ulizonazo wakati hata hujui utakula nini kesho, ni ajabu kubwa, si mtakufa ama dhurika wote? Nchi marafiki walikaa wanashangaa ama walitoa msaada wakisubiri kwa hamu na kujiuliza 'hivi motokeo yatakua nini?'.Kila mtu anajua matokeo yapoje TZ.

Ni mlolongo wa mambo mengi tu ambayo hayakustahili kufanywa, lakini na Nyerere aliamua kuyafanya. Ikiwa na maana hakuingoza nchi vyema.
 
jn11az1.jpg


Hata baadhi ya viongozi wanaowabeza wanyonge wasingekanyaga mjini. Elimu ya bure na huduma nyingine za kijamii ndizo zilizowajengea nguvu ya kufika walipo sasa. Naam! Leo tunaadhimisha miaka 8 tangu kifo cha Mwalimu. Laiti, Mwalimu na wenzake wangekuwa wenye kujali ubinafsi na kutanguliza maslahi yao, Tanzania ingekuwa haina tofauti na Congo, Rwanda, Uganda na nchi nyingine zilizopigana vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mwalimu na wenzake walitanguliza mbele maslahi ya nchi zetu na watu wake. Mwalimu aliumiza kichwa kwa ajili yetu.

Pichani ni Nyerere, Kaunda na Kawawa, Mbeya 1963. Katika kitabu chake "The Long Walk To Freedom" Nelson Mandela anaelezea kushangazwa kwake mara ile alipokutana na Nyerere kwa mara ya kwanza miaka le ya mwanzoni mwa uhuru. Kwamba Rais wa nchi aliacha kuishi Ikulu ya kifahari akaamua kwenda kujenga kwa mkopo nyumba yake ya kawaida pale Msasani. Kwamba Rais wa nchi aliendesha mwenyewe Ford Cortina iliyochakaa. Je, hali ikoje siku hizi?


Picture: Credit Mjengwa blog
 
Nikiwa Mtoto Mdogo- Nili sukumwa na Polisi au hata kukanyagwa-nilikua nina jaribu kusogea alipo kua ana pita Nyerere!!
 
ningequalify kuwa ukiondoa Afrika ya Kusini, kwa maana sidhani kama jinsi Afrika ya Kusini ilivyopiga hatua ya maendeleo kwenye baadhi ya miji yake ndiyo ingekuwa hatua ya Tanzania kufuata. ama?

....makes sense now
 
Yapo mengi ya kujiuliza,Tofauti ya kipato kati ya walioko juu na wa chini kwa sasa na enzi ya uongozi wa Mwalimu ikoje? Idadi ya watu wanaopata elimu kwa asilimia inatofautianaje? Ufisadi na ubadhilifu wa mali za umma unatofautianaje? maswali ni mengi sana. Lakini hitimisho ni kuwa Mwl alikuwa kiongozi wa Taifa na si wa kikundi au tabaka fulani teule.Na kwa kuwa aliweka mbele maslahi ya taifa,hata kama mipango mingi haikufanikiwa ile dhamira yake njema pekee inamfanya kuwa kiongozi aliyetukuka.
 
Back
Top Bottom