Ilikuwa Mei Mosi 1985, iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tanga na kuhudhuriwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya Madola Bw. Sherdath Ramphal (or similar sounding name). Siku ya pili yake mvua kubwa ilinyesha mjini Tanga na kufanya barabara kubwa za lami zisipitike hasa kutokea Old Nguvumali, Kisosora, Chumbageni n.k Ikabidi Mwalimu na msafara wake wapite "Uswahilini". Ndipo nilipopata kuona Mwalimu alivyokuwa mtu wa watu... mimi na ndugu zangu tukawa tumejipanga kwenye geti la nyumbani (tulikuwa na kakibanda kakuuza machungwa toka Muheza) basi jua likiwa limeanza kupiga, na akiwa amechelewa kwenda uwanja wa ndege, msafara wake ulipita taratibu katika barabara hiyo ya mashimo (kwani haikuandaliwa kwa ajili ya msafara!) basi tu yeye kageuka upande mmoja tu anapungua watu, ndipo binamu yangu wa kike alipopiga kelele "Na huku!" Mwalimu akitabasamu akageuka na kutupungia... Ilikuwa ni siku ya furaha kwamba na sisi "tumesikiwa"... Since then, I have made it my mission... to be heard by our leaders!!