Kiranga nakusoma na kukuelewa vizuri hasa hoja za Watanzania kuhusu uhuru wa maoni na kushiriki.
Gwajima: Ana makando kando mengi kuanzia madhabahuni, jimboni, Bungeni na mitaani. Ni mtata asiye na credibility wala integrity. Hilo halina ubishi. Wakati ndio unampa ''heroism'.
Hoja ya mauaji na utakeji ilipotinga Bungeni Spika aliipiga marufuku. Ukiacha mbunge wa Chadema, wengine 390 na ushee hawakuthubu kusema chochote
Gwajima katoka Bungeni na kuita wanahabari kuzungumzia tatizo linaloikera jamii ndicho kumemfanya awe 'a man of moment''. Mkuu hata saa mbovu husema ukweli mara 2 kwa siku. Yes ni oppotunist lakini kwa hili aligusa Umma ndio maana Umma umesahau makando kando yake! kwasababu tuna huzuni na ndilo tatizo la wakati huu! kalisemea
Fatma: Ni mtata pia! aliyopigania wakati wa Magufuli alikaa kimya wakati wa Samia. Fatma alihamasisha watu wavae nguo nyeupe kama ishara ya kudai Tume huru ya uchaguzi. Sikumbuki kama anadai leo hii.
Fatma alipigania Katiba mpya, lakini pia tulimuona kwa Mkandala akijua si katiba mpya ni ulaghai! kisa Samia
Sikubaliani na watu wanaotaka sote tuwe na fikra sawa, wala sikubaliani kuwa mitazamo tofauti ni usaliti.
Hata hivyo penye utata pasemwe! Fatma na Gwajima ni watata, haina maana ni wasaliti au ni hovyo, la hasha, ni watata tu!