- Thread starter
- #201
Kwa nini unajipa ujuzi usio nao?
Unajua vikao vyote vya kuunda ACT na kuweka mikakati ya kujiimarisha kwake vilifanyika lini, wapi, na nani alikuwapo?
Tarehe iliyosajiliwa ACT ni 5 Mei 2014, takriban miaka 10 iliyopita, na kililazimika kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka uliofuata, yaani 2015. Fatma anadai kuwa aliwashauri ACT washiriki uchaguzi huo miaka 10 iliyopita, lakini hakuna mahali popote kumbukumbu hiyo imewekwa rasmi (japo iwe ni kweli au la, hakuna uthibitisho wowote zaidi ya kauli yake binafsi, hivyo inabaki kuwa hoja ya upande mmoja, yaani subjective).Sasa hoja yako ni ipi hasa? Unataka kusema kuwa Fatma alikuwa akisubiri kwa muda wote huo ili awashauri ACT washiriki uchaguzi, kwenye mikutano yao waliyoamua kususia? (ambapo hata hivyo hakuna ushahidi unaoonesha kuwa hayo mazungumzo yalifanyika). Je, aliwashauri kushiriki uchaguzi mara baada ya chama kuanzishwa? It doesn't make sense, umeingia mjini kirahisi hapa!