GE2025 Nini kimempata Fatma Karume?

GE2025 Nini kimempata Fatma Karume?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
What are you guys trying to say?

That Fatma Karume is indispensable to this movement?

What is your point, if there is one apart from just catching feelings emotionally because someone does not necessarily agree with you 100% for 100% of the time?
 
Mkuu,

Ni wapi hasa amelazimishwa? Naona unakaza fuvu tu kutetea.

Huyo unayesema anaishi maisha yake binafsi anatumia majukwaa ya wazi yanayofuatiliwa na umma. Hawezi kutumia majukwaa hayo kuwatetea wazi wahuni wa kisiasa halafu watu wakae kimya, eti kwa sababu sasa anaishi binafsi.

Anapojitokeza hadharani na kutoa kauli zenye athari kwa wjamii, lazima atambue kuwa atawajibika kwa maoni yake mbele ya umma si kwa kivuli cha maisha binafsi.
Amewatetea wahuni gani wa kisiasa?

Na unajuaje anawatetea wahuni wa kisiasa na si kwamba mna tofauti ya kifalsafa kuhusu jinsi gani ya kumaliza matatizo ya kisiasa?
 
Amewatetea wahuni gani wa kisiasa?

Na unajuaje anawatetea wahuni wa kisiasa na si kwamba mna tofauti ya kifalsafa kuhusu jinsi gani ya kumaliza matatizo ya kisiasa?
Mkuu!
Kwa kutumia akili ya kawaida tu, mtu anayesimamia kushiriki uchaguzi chini ya sheria hizi kandamizi, bila kuzikosoa wala kuzipinga, huoni kama kwa njia moja au nyingine anatoa uhalali kwa wale wahuni waliotunga sheria hizo?

Au ndiyo falsafa hiyo!?
 
Mkuu!
Kwa kutumia akili ya kawaida tu, mtu anayesimamia kushiriki uchaguzi chini ya sheria hizi kandamizi, bila kuzikosoa wala kuzipinga, huoni kama kwa njia moja au nyingine anatoa uhalali kwa wale wahuni waliotunga sheria hizo?

Au ndiyo falsafa hiyo!?
Whether anatoa uhalali au hatoi uhalali si muhimu.

Kitu muhimu ni kwamba anatumia haki yake. Na hutakiwi kumuingilia katika kutumia haki yake hiyo. Unatakiwa kumshawishi kuhusu upande wako, akikubaliana na wewe atajiunga nawe, asipokubaliana nawe, kwa sababu yoyote, kwa ujinga wake, au labda wewe ndiye mjinga kuna kitu yeye kaona wewe hujaona, hiyo ni haki yake.

Hutakiwi kumshikia bango mtu kwa kutumia haki yake ya kidemokrasia.

Mnafanya kosa la kuminya demokrasia za watu wakati mnasema mnapigania demokrasia.

This is a contradiction.
 
Kwahiyo mtu akiwa na mtizamo tofauti na wewe yeye ndo anatatizo kwanini usijiulize wewe una tatizo gani?
 
Hivi karibuni, Fatma Karume ameonekana kubadili mwelekeo wa mijadala yake ya kisiasa kwa namna ambayo imeibua maswali miongoni mwa watanzania, hasa wale wanaoamini katika harakati za mageuzi ya kweli.

Mwanzo, alivamia vikali kauli za Askofu Gwajima aliyekuwa anapinga matukio ya utekaji na ukiukwaji wa haki unaodaiwa kufanywa na vyombo vya dola, akimtuhumu kuwa anatafuta "attention" ya kisiasa, licha ya kwamba hoja za Gwajima zilikuwa na uzito wa kulinda utu na uhuru wa raia.

Sasa, ameibukia tena kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), akizibeza juhudi za CHADEMA na sera yao ya "No Reforms, No Elections", akikariri kuwa kusitisha uchaguzi ni kosa la jinai. Kauli hii imechukuliwa na wengi kama kejeli isiyoakisi hali halisi ya mazingira ya kisiasa nchini, ambapo haki za msingi, uhuru wa kisiasa na uhuru wa kutoa maoni vinaendelea kukandamizwa.

Cha kushangaza zaidi, kauli hizi za Fatma Karume zinatolewa wakati ambapo Tundu Lissu, mmoja wa viongozi wa upinzani na mwanasheria mwenzake, yuko rumande akikabiliwa na mashtaka ya uhaini, ambayo kisheria adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa. Hali hii imezidi kuzua maswali: je, Fatma Karume bado yupo upande wa watetezi wa haki, au amebadili msimamo kwa sababu ambazo bado hazijafahamika wazi?

Ikumbukwe kuwa katika utawala wa Hayati John Magufuli, Fatma Karume alijitokeza kuwa mmoja wa sauti thabiti zilizokuwa zikikemea dhuluma, ukandamizaji, na matumizi mabaya ya madaraka. Lakini katika utawala wa sasa, ambao nao umeonesha mwelekeo wa kukiuka misingi ya demokrasia, sauti yake imekuwa ya mashaka, wakati mwingine ikisikika kama ya kukubaliabiana na mfumo badala ya kuukosoa.
Je, ni mabadiliko ya kiitikadi? Ni mkakati wa kisiasa? Au kuna mambo ya ndani zaidi ambayo bado hayajawekwa wazi kwa umma? Kwa vyovyote vile, hatua na kauli za Fatma Karume zinahitaji tafakari, hasa kwa wale wanaoamini katika dhana ya "principled activism" yaani, kupigania haki bila kujali nani yuko madarakani.
Fatuma Karume ni kama Zitto, Wanasumbuliwa na Udini, Tumewafichia sana hii siri lakini sasa tumeamua kuwalipua.

Huwezi kusema utalinda kura leo wakati 2024 ulishindwa, huu ni utapeli wa kipumbavu sana!
 
Whether anatoa uhalali au hatoi uhalali si muhimu.

Kitu muhimu ni kwamba anatumia haki yake. Na hutakiwi kumuingilia katika kutumia haki yake hiyo. Unatakiwa kumshawishi kuhusu upande wako, akikubaliana na wewe atajiunga nawe, asipokubaliana nawe, kwa sababu yoyote, kwa ujinga wake, au labda wewe ndiye mjinga kuna kitu yeye kaona wewe hujaona, hiyo ni haki yake.

Hutakiwi kumshikia bango mtu kwa kutumia haki yake ya kidemokrasia.

Mnafanya kosa la kuminya demokrasia za watu wakati mnasema mnapigania demokrasia.

This is a contradiction.
Kuna misingi ya kidemokrasia ambayo haibadiliki haki ni haki. Uchaguzi huru na wa haki ni msingi wa lazima katika mfumo wowote wa kidemokrasia. Kuleta uswahili kwa kisingizio cha falsafa za mchongo ni sawa na kuhalalisha utapeli wa kisiasa.

Na kama mtu anatoa kauli hadharani kupitia majukwaa ya wazi, basi ni lazima ajiandae kukosolewa na kuchukuliwa kwa uzito huo huo wa umma. Kama hataki kukosolewa, aendelee na falsafa zake akiwa peke yake chumbani kwake, si hadharani.
 
Kuna misingi ya kidemokrasia ambayo haibadiliki haki ni haki. Uchaguzi huru na wa haki ni msingi wa lazima katika mfumo wowote wa kidemokrasia. Kuleta uswahili kwa kisingizio cha falsafa za mchongo ni sawa na kuhalalisha utapeli wa kisiasa.

Na kama mtu anatoa kauli hadharani kupitia majukwaa ya wazi, basi ni lazima ajiandae kukosolewa na kuchukuliwa kwa uzito huo huo wa umma. Kama hataki kukosolewa, aendelee na falsafa zake akiwa peke yake chumbani kwake, si hadharani.
Tunaweza kukubaliana kuwa uchaguzi huru na wa haki ni haki ya kidemokrasia, lakini jinsi ya kuufikia watu wanaweza kutofautiana wapitie njia gani, na hata wakikubaliana njia moja wanaweza kutofautiana jinsi ya kuudai, ratiba ya kuupata etc?

Au hutaki kuwapa watu uchaguzi wa njia ya kupata uchaguzi huru na wa haki?

Unataka uchaguzi huru na wa haki upatikane kwa njia ya kidikteta unayoiona sawa wewe tu?

Uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki kweli?
 
Hivi karibuni, Fatma Karume ameonekana kubadili mwelekeo wa mijadala yake ya kisiasa kwa namna ambayo imeibua maswali miongoni mwa watanzania, hasa wale wanaoamini katika harakati za mageuzi ya kweli.

Mwanzo, alivamia vikali kauli za Askofu Gwajima aliyekuwa anapinga matukio ya utekaji na ukiukwaji wa haki unaodaiwa kufanywa na vyombo vya dola, akimtuhumu kuwa anatafuta "attention" ya kisiasa, licha ya kwamba hoja za Gwajima zilikuwa na uzito wa kulinda utu na uhuru wa raia.

Sasa, ameibukia tena kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), akizibeza juhudi za CHADEMA na sera yao ya "No Reforms, No Elections", akikariri kuwa kusitisha uchaguzi ni kosa la jinai. Kauli hii imechukuliwa na wengi kama kejeli isiyoakisi hali halisi ya mazingira ya kisiasa nchini, ambapo haki za msingi, uhuru wa kisiasa na uhuru wa kutoa maoni vinaendelea kukandamizwa.

Cha kushangaza zaidi, kauli hizi za Fatma Karume zinatolewa wakati ambapo Tundu Lissu, mmoja wa viongozi wa upinzani na mwanasheria mwenzake, yuko rumande akikabiliwa na mashtaka ya uhaini, ambayo kisheria adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa. Hali hii imezidi kuzua maswali: je, Fatma Karume bado yupo upande wa watetezi wa haki, au amebadili msimamo kwa sababu ambazo bado hazijafahamika wazi?

Ikumbukwe kuwa katika utawala wa Hayati John Magufuli, Fatma Karume alijitokeza kuwa mmoja wa sauti thabiti zilizokuwa zikikemea dhuluma, ukandamizaji, na matumizi mabaya ya madaraka. Lakini katika utawala wa sasa, ambao nao umeonesha mwelekeo wa kukiuka misingi ya demokrasia, sauti yake imekuwa ya mashaka, wakati mwingine ikisikika kama ya kukubaliabiana na mfumo badala ya kuukosoa.
Je, ni mabadiliko ya kiitikadi? Ni mkakati wa kisiasa? Au kuna mambo ya ndani zaidi ambayo bado hayajawekwa wazi kwa umma? Kwa vyovyote vile, hatua na kauli za Fatma Karume zinahitaji tafakari, hasa kwa wale wanaoamini katika dhana ya "principled activism" yaani, kupigania haki bila kujali nani yuko madarakani.
Mnachofeli ni kuwachukulia binadamu kama mawe kwamba hawabadiliki, ila amini amini nawaambia mwanadamu yeyote anaweza kubalika muda wowote ndio maana maandiko matakatifu yanatuasa tusimtegemee mwanadamu
 
Tunaweza kukubaliana kuwa uchaguzi huru na wa haki ni haki ya kidemokrasia, lakini jinsi ya kuufikia watu wanaweza kutofautiana wapitie njia gani, na hata wakikubaliana njia moja wanaweza kutofautiana jinsi ya kuudai, ratiba ya kuupata etc?

Au hutaki kuwapa watu uchaguzi wa njia ya kupata uchaguzi huru na wa haki?

Unataka uchaguzi huru na wa haki upatikane kwa njia ya kidikteta unayoiona sawa wewe tu?

Uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki kweli?
Atupe hizo njia!

Je, ni wapi Fatma amewahi kutoa mapendekezo/njia !?
Mbali na kusisitiza kushiriki katika uchaguzi unaoendeshwa kwa sheria tata na zenye ukakasi!?

Amewahi kueleza kwa kina mbinu au mikakati ya kubadili mfumo huo zaidi ya kushiriki ?"
 
Tunaweza kukubaliana kuwa uchaguzi huru na wa haki ni haki ya kidemokrasia, lakini jinsi ya kuufikia watu wanaweza kutofautiana wapitie njia gani, na hata wakikubaliana njia moja wanaweza kutofautiana jinsi ya kuudai, ratiba ya kuupata etc?

Au hutaki kuwapa watu uchaguzi wa njia ya kupata uchaguzi huru na wa haki?

Unataka uchaguzi huru na wa haki upatikane kwa njia ya kidikteta unayoiona sawa wewe tu?

Uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki kweli?
Atupe hizo njia!

Je, ni wapi Fatma amewahi kutoa mapendekezo/njia !?
Mbali na kusisitiza kushiriki katika uchaguzi unaoendeshwa kwa sheria tata na zenye ukakasi!?

Amewahi kueleza kwa kina mbinu au mikakati ya kubadili mfumo huo zaidi ya kushiriki I ?"
 
Atupe hizo njia!

Je, ni wapi Fatma amewahi kutoa mapendekezo/njia !?
Mbali na kusisitiza kushiriki katika uchaguzi unaoendeshwa kwa sheria tata na zenye ukakasi!?

Amewahi kueleza kwa kina mbinu au mikakati ya kubadili mfumo huo zaidi ya kushiriki ?"
Why are you making her a pillar of society and singularly responsible for this formula for a succesful paradigm shift?

Fatma Karume tumemuona tangu akiwa binti mdogo tu anaenda Masasani kwa Nyerere pale kabla hajaenda Uingereza kusoma.

Why are you making her this crucial oracle all of a sudden?
 
Why are you making her a pillar of society and singularly responsible for this formula for a succesful paradigm shift?

Fatma Karume tumemuona tangu akiwa binti mdogo tu anaenda Masasani kwa Nyerere pale kabla hajaenda Uingereza kusoma.

Why are you making her this crucial oracle all of a sudden?
She is not the pillar of society, she’s just one among many this year pushing citizens to participate in an election that is neither free nor fair.

The list of such individuals is long. And even you, if you one day find yourself on that list and bring that position to the public, we will criticize you too, because what we demand is a truly fair and free election, not some political circus wrapped in baseless 'philosophies.'

Otherwise, keep your personal stances locked away in your room, not in the public space.
 
She is not the pillar of society, she’s just one among many this year pushing citizens to participate in an election that is neither free nor fair.

The list of such individuals is long. And even you, if you one day find yourself on that list and bring that position to the public, we will criticize you too, because what we demand is a truly fair and free election, not some political circus wrapped in baseless 'philosophies.'

Otherwise, keep your personal stances locked away in your room, not in the public space.
Wewe elezea sera zako, usimkataze mtu kuishi anavyotaka na kuelezea sera zake.

Kama Fatma ni mtu mmoja tu, kwa nini mnamshikia bango hivyo?

Kwa nini mnasumbuka na trivial personalities tu wakati mna kazi kubwa ya institutional reforms?

Mbona kama unataka kumnyima mtu mwingine uhuru wa kuishi anavyotaka? Unataka kulazimisha afuate unavyotaka wewe wakati yeye hajakubali kuishi hivyo?

Watu watakaoamua kupiga kura, kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura nao mtawazuia wasipige kura?

Ndiyo demokrasia hiyo?

Screenshot_20250707_155704_X.jpg
 
Wewe elezea sera zako, usimkataze mtu kuishi anavyotaka na kuelezea sera zake.

Kama Fatma ni mtu mmoja tu, kwa nini mnamshikia bango hivyo?

Kwa nini mnasumbuka na trivial personalities tu wakati mna kazi kubwa ya institutional reforms?

Mbona kama unataka kumnyima mtu mwingine uhuru wa kuishi anavyotaka? Unataka kulazimaisha afuate unavyotaka wewe wakati yeye hajakubali kuishi hivyo?

Watu watakaoamua kupiga kura, kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura nao mtawazuia wasipige kura?

Ndiyo demokrasia hiyo?

Acha kuleta usanii hapa na kutwist maneno. Hakuna anayeshughulika na truvial personalities.

Hizi 'institutional reforms' unazozitaja zina maana gani ikiwa mfumo mzima umejaa wasanii wanaoshindwa kutambua umuhimu wa kuwa na uchaguzi huru na wa haki?

Tunawezaje kuzungumzia mageuzi ya taasisi bila uhuru wa kweli wa kuchagua viongozi sahihi ndani ya mfumo wenyewe?

Wananchi wana haki ya kikatiba ya kupiga kura hilo halina ubishi lakini kwa hali ilivyo sasa, sheria za uchaguzi zenyewe zinaminya na kudhoofisha haki hiyo hiyo ya kikatiba.
 
Acha kuleta usanii hapa na kutwist maneno. Hakuna anayeshughulika na truvial personalities.

Hizi 'institutional reforms' unazozitaja zina maana gani ikiwa mfumo mzima umejaa wasanii wanaoshindwa kutambua umuhimu wa kuwa na uchaguzi huru na wa haki?

Tunawezaje kuzungumzia mageuzi ya taasisi bila uhuru wa kweli wa kuchagua viongozi sahihi ndani ya mfumo wenyewe?

Wananchi wana haki ya kikatiba ya kupiga kura hilo halina ubishi lakini kwa hali ilivyo sasa, sheria za uchaguzi zenyewe zinaminya na kudhoofisha haki hiyo hiyo ya kikatiba.
Mkuu,

Kwa nini mnamshikia bango sana Fatma?

Yani hii ndiyo namna efficient kabisa ya kupata mnachokitaka? Kwa kumshikia bango Fatma Karume? Kweli kabisa?

Fatma Karume ndiyo tatizo lenu?



Screenshot_20250707_160310_WhatsApp.jpg
 
Wewe elezea sera zako, usimkataze mtu kuishi anavyotaka na kuelezea sera zake.

Kama Fatma ni mtu mmoja tu, kwa nini mnamshikia bango hivyo?

Kwa nini mnasumbuka na trivial personalities tu wakati mna kazi kubwa ya institutional reforms?

Mbona kama unataka kumnyima mtu mwingine uhuru wa kuishi anavyotaka? Unataka kulazimisha afuate unavyotaka wewe wakati yeye hajakubali kuishi hivyo?

Watu watakaoamua kupiga kura, kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura nao mtawazuia wasipige kura?

Ndiyo demokrasia hiyo?

View attachment 3397716
Hayo ya 2019 yalikuwa maigizo ya Mbowe hamna la maana ! Hamna historia yeyote ya kujifunza hapo!
 
Hivi karibuni, Fatma Karume ameonekana kubadili mwelekeo wa mijadala yake ya kisiasa kwa namna ambayo imeibua maswali miongoni mwa watanzania, hasa wale wanaoamini katika harakati za mageuzi ya kweli.

Mwanzo, alivamia vikali kauli za Askofu Gwajima aliyekuwa anapinga matukio ya utekaji na ukiukwaji wa haki unaodaiwa kufanywa na vyombo vya dola, akimtuhumu kuwa anatafuta "attention" ya kisiasa, licha ya kwamba hoja za Gwajima zilikuwa na uzito wa kulinda utu na uhuru wa raia.

Sasa, ameibukia tena kwenye mtandao wa X (zamani Twitter), akizibeza juhudi za CHADEMA na sera yao ya "No Reforms, No Elections", akikariri kuwa kusitisha uchaguzi ni kosa la jinai. Kauli hii imechukuliwa na wengi kama kejeli isiyoakisi hali halisi ya mazingira ya kisiasa nchini, ambapo haki za msingi, uhuru wa kisiasa na uhuru wa kutoa maoni vinaendelea kukandamizwa.

Cha kushangaza zaidi, kauli hizi za Fatma Karume zinatolewa wakati ambapo Tundu Lissu, mmoja wa viongozi wa upinzani na mwanasheria mwenzake, yuko rumande akikabiliwa na mashtaka ya uhaini, ambayo kisheria adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa. Hali hii imezidi kuzua maswali: je, Fatma Karume bado yupo upande wa watetezi wa haki, au amebadili msimamo kwa sababu ambazo bado hazijafahamika wazi?

Ikumbukwe kuwa katika utawala wa Hayati John Magufuli, Fatma Karume alijitokeza kuwa mmoja wa sauti thabiti zilizokuwa zikikemea dhuluma, ukandamizaji, na matumizi mabaya ya madaraka. Lakini katika utawala wa sasa, ambao nao umeonesha mwelekeo wa kukiuka misingi ya demokrasia, sauti yake imekuwa ya mashaka, wakati mwingine ikisikika kama ya kukubaliabiana na mfumo badala ya kuukosoa.
Je, ni mabadiliko ya kiitikadi? Ni mkakati wa kisiasa? Au kuna mambo ya ndani zaidi ambayo bado hayajawekwa wazi kwa umma? Kwa vyovyote vile, hatua na kauli za Fatma Karume zinahitaji tafakari, hasa kwa wale wanaoamini katika dhana ya "principled activism" yaani, kupigania haki bila kujali nani yuko madarakani.
Uzanzibari una msumbua aliyepo ikulu ni mzanzibari
 
Mkuu,

Kwa nini mnamshikia bango sana Fatma?

Yani hii ndiyo namna efficient kabisa ya kupata mnachokitaka? Kwa kumshikia bango Fatma Karume? Kweli kabisa?

Fatma Karume ndiyo tatizo lenu?



View attachment 3397723
Mkuu!

Ww umeamua kumtetea sio mbaya! Hajashikiwa bango Fatma tu nilisema kwenye post zangu za juu kwamba
"She is not the pillar of society, she’s just one among many this year pushing citizens to participate in an election that is neither free nor fair.

The list of such individuals is long"

Anajichekesha tu lkn dawa imemuingia vzuri aache usanii!
 
Back
Top Bottom