Nini kilikusaidia kupata kazi?

Nini kilikusaidia kupata kazi?

[emoji3516]
WEWE NI KADA WA CCM BILA SHAKA!!!

Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app
Sina chama.

Ila nataka kujua kwanini wasomi tunaotegemea walete mabadiliko kwenye kada za science,technology na mambo ya tiba au kutengeneza ajira wao ndio wanaomba kazi.

Kwanini wanaomba kazi?

Hapo tunarudi kwenye nini lengo la elimu.
 
Iyo kozi unashindwa vip kujiajiri mkuu.?
Mkuu hata sasa nikipata ishu napiga sichaguagi kazi pia nimedevelop saiti yangu lakin naona bado mambo haendi
Screenshot_20201115-144050.png
 
Mkuu hata sasa nikipata ishu napiga sichaguagi kazi pia nimedevelop saiti yangu lakin naona bado mambo haendiView attachment 1626884
Tunafahamiana? Kama hapana, nina plan yangu ninayoweza kukupatia na ukabenefit from it. We can work together and have different roles in position. Lakini nikachukua 28 percent after profit off.
 
Mimi hata sielewi, niliambiwa tu nenda kwa baba yako mdogo mengine atakwambia huko huko. Nilipata ajira nikiwa na 19yrs hata barua ya kuomba kazi nakumbuka aliniandikia mzee.
Hiyo ilkuwa enzo zile za ufisadi na kumjua Nani kwenye ajira

Bar maid boss akimpenda anampeleka ofisini kwake anamwajiri Kama secretary wakati hajui hata ku taipu atasoma humo humo usekretary akiwa kwenye ajira!!!

Wengi walianza kazi bila interview Wala kuandika barua ya kuomba kazi

Unafika unaanza kazi barua ya ajira inakukuta mezani Sasa hivi enzi hizo zimepita
 
Binafsi bado sijapata kazi wakuu labda nikipata ntarudi kuleta mrejesho ili wengine pia wajifunze.
Nina vyeti "mlima", ujuzi mbalimbali, uaminifu kiwango cha SGR, uadilifu uliotukuka n.k lakini kukosa "connection" ndo kunanifanya niendelee kusota mtaani mwaka wa pili sasa tangu nivue JOHO[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Sasa wandugu wewe uliwezaje kupata kazi tupeane mbinu jamani stress zinazidi
Ukiziendekeza stress utawaza kujiyonga. Mimi nilimaliza chuo mwaka 2009 na kukaa mtaani miaka 3 bila kazi yoyote, wala TV, wala rafiki kwa maana punde baada ya kumaliza chuo tukahama kutoka tulipokuwa tumepanga tukahamia nyumba mpya yetu wenyewe ambayo haikuwa na umeme.

Nimepitia huo wakati mgumu kama wako mdogo wangu. Jipe moyo kuwa Mungu anaweza na ipo siku atakufungulia milango ya baraka.
 
Nimemaliza chuo kipindi cha kusubiri graduation, nikajua aina gani ya kampuni ningependa kufanyia kazi ambazo nyingi zilikuwa SME's ,

Nikaingia mtandao wa linkedin, nikawafollow (connect) maboss wa kampuni chache na kuwatumia ombi langu inbox bila kuweka pesa mbele. Nilijibiwa na baadhi ilibidi niwapelekee CV physically

Nilijibiwa na mtu mmoja seriously lakini ilinichukua kama mwezi mmoja kusubiri then nikaitwa kama intern then nikapewa kazi with low payment

Kwa kiasi kikubwa mitandao imenisaidia kuanzia linkedin, Jamii forums hadi facebook ingawa bado nahustle kufika napotaka, inshallaahh nitafika
 
Vijana wengi wanamaliza vyuo kila mwaka ilihali wengine bado tuko mtaani hatujui hatima ya maisha yetu.Mimi binafsi nimehitimu miaka kadhaa imepita nilipomaliza chuo nilikuwa na haraka sana ya kutafuta kazi miaka inasonga ni kama zile nguvu zimeisha nahisi uchungu kusikia mtu anaongelea mambo yanahusu kazi ilihali wengine tunahangaika sana..

Kwa kweli nimeitwa interview kadhaa lakini naona kama danganya toto tu walio na iyo kazi wapo tayari wengine tunapoteza tu muda..nimefikiria kila mtu anayeweza kunipa connection lakini nako hakuna matumaini.
Pole sana mdogo wangu. Nilikuwa kama wewe mwaka 2009 mpaka 2012 ila yote yamepita na imebaki kuwa historia.

Ninakuombea kwa Mungu wewe pamoja na vijana wengine wanaohangaika kupata kazi kuwa ipo siku utakuwa na pesa nyingi sana mdogo wangu.
 
Back
Top Bottom