Nimemaliza degree ya IT , niliomba ajira kila pahala ila nimeambulia patupu,utumishi ya serikali huko ndio nyumban kwan ilikuwa kila siku lazima nipitie portal yao, ninaitwa sana mpk oral ila sikuwahi kubahatika kupata, inafika pahala wanaweza kuitwa hata watu 3 hapo wanatakiwa 2 ila amini ndugu yangu siwezi kuitwa, nimesali sana na kuomba ila wapi, pale home wakaona ni mzigo kukaa pale kwani nikirudi nasimangwa kwa maneno mfano mbona fulani kapata kazi, ww unafeli wapi nk. Nikaona Isiwe tabu nikahama pale home nakaa gheto kwa sasa, kiufupi sasa hivi nauza matunda katika genge na mshikaji wangu niliesoma nae primary, na jioni nafanya betting maisha yanaenda. Sitakaa niombe tena Ajira yaan, najua kuna siku nitatoboa.