Alvin Slain
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 6,375
- 3,668
Habari.
Nimepigwa na butwaa sana leo hii.
Nilikua natoka katika banda langu la kuku,Mara akaja jamaa wa mtaani kwetu
,Huku akiniulizia kama nina mayai viza,Mayai ambayo yameshaatamiwa na kuku lakini hayakuanguliwa.
Nilipomuuliza anakwenda kuyafanyia nini,akaniambia ana kazi nayo,
Sasa ningependa kujua ni kazi gani mayai viza hufanya.?
Karibuni wadau mnifungue macho.