Nini kazi ya mayai viza?

Nini kazi ya mayai viza?

Habari.
Nimepigwa na butwaa sana leo hii.


Nilikua natoka katika banda langu la kuku,Mara akaja jamaa wa mtaani kwetu

,Huku akiniulizia kama nina mayai viza,Mayai ambayo yameshaatamiwa na kuku lakini hayakuanguliwa.

Nilipomuuliza anakwenda kuyafanyia nini,akaniambia ana kazi nayo,

Sasa ningependa kujua ni kazi gani mayai viza hufanya.?
Karibuni wadau mnifungue macho.
Kukuambia akuambie mwingine sisi ndo tutoe maelezo? Majanga!
 
Zamani mtu akija kumtongoza dada usiku. unamvizia akianza kumkumbatia unampiga nalo. Dada anarudi nyumbani na doezi harudi tena.
 
timu+kalu5.jpg

We jamaaa, hapana, umeshindikana, saluti, we balaa, unatisha aisee, unafanya mambo yawe rahisi ndugu, big up mkuu, hongera sana, uendelee na moyo huo huo na MUNGU AKUBARIKI.
 
Mnao toa sababu za kichawi, mnathibitisha imani zenu, binafsi nnajua yanatumika kupigia mtu endapo una bf naye.
 
Haya sasa hapo namie acha nianze ufugaji wa kuku.
Sasa wataalam nipeni mbinu ya kufanya mayai ya kuku yawe VIZA
Maana bei yake ni kubwa kuliko mayai mazima
 
Mnao toa sababu za kichawi, mnathibitisha imani zenu, binafsi nnajua yanatumika kupigia mtu endapo una bf naye.

Na wewe unayetoa sababu za ugomvi unathibitisha kuwa ni mtu usiye na BUSARA!
 
kuwapelekea washirikina/ waganga ili wakimnuizia mtu wanasema nataka mwajuma mambo yake yavunde kama hili yai viza lilivovunda, pia mambo yake yasifanikiwe kama hili yai viza ambalo halikufanikiwa kuangua kifaranga.
Kazi nyingine ni kuwapiga watu ambao unaugomvi nao lakini kupigana nao huwezi hivo unamvizia anapita mahali unajibanza unampiga nayo kama matatu hivi aiseeee anachukua wiki nzima hiyo harufu ya uviza kuisha mwilini mwake.
Kazi nyingine muulize huyo aliyekuja kukuomba hayo mayai, tena usimpe bure umuuzie.

Nimecheka sana.
 
mayai viza ni bidhaa adimu na muhimu sana kwa waganga wa kienyeji, na yanauzwa bei nzuri, hata wewe waweza kuyahifadhi kwa ajili ya kuyauza hapo baadae....
kazi zake ndio hizo jamaa wamekwambia!

aisee hapa kwangu pana hatchery ninatoa mengi sana aiseee nipeni soko bwana
 
Kule jukwaa la ujasiriamali tumejifunza kuwa mayai viza hutumika kuwawekea kuku wanaoatamia ili wasubiriane. Mfano una kuku 5 unataka waatamie pamoja na kutotoa vifaranga pamoja, wale wanaoonesha dalili ya kuwahi kuatamia unawawekea mayai viza ili wawangojee wenzao, then wakianza wote unatoa viza unaweka mazuri. Ngoja aje Kubota.
 
Last edited by a moderator:
It sound logical, maana wengine wanawaza uchawi tu, ptuuuuuuu.

Angalia mazingira halafu rudi kwenye hizo logics

1. Unafikiri huyo jamaa kweli anataka mbolea? Atakusanya mayai mangapi, na umeshawahi kuona wapi Tz mayai viza yametumika kama mbolea?

2. Au utasema ndo anataka mafuta kwa ajiri kuwashia mot, kweli Bongo? Tuna kuni lukuki na hazihitaji mafuta kuwaka.

3. Au kweli unataka kusema jamaa anataka kutengeneza gunpowder?

Fanya upembuzi wa ulichaoambiwa kwa kuoanisha na mazingira, usikurupuke kusema something is illogical wakati wewe hujafanya analysis.
 
timu+kalu5.jpg

Habari.
Nimepigwa na butwaa sana leo hii.


Nilikua natoka katika banda langu la kuku,Mara akaja jamaa wa mtaani kwetu

,Huku akiniulizia kama nina mayai viza,Mayai ambayo yameshaatamiwa na kuku lakini hayakuanguliwa.

Nilipomuuliza anakwenda kuyafanyia nini,akaniambia ana kazi nayo,

Sasa ningependa kujua ni kazi gani mayai viza hufanya.?
Karibuni wadau mnifungue macho.

........... hujui ! sasa hiyo picha umeipata wapi ??
 
nguvu
Unadhani una uelewa sana wa mambo?
si lazima kuchangia kila post unaweza kupita tu.

Jitambue.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom