Ninawindwa, mniombee...

Ninawindwa, mniombee...

Kwahio nani anastahili DHARAU?,
Je ?, kama na wewe ulimkataa kwa DHARAU ndio maana anakuwinda alipe kiasi kama wewe ulivyomlipia kiasi Rafiki yako.

Wacha Mapambano yaendelee.
Mimi sikumkataa kwa dharau, nilimkataa kistaarabu mno. Nikamuambia wewe ni mzuri ila sijakupenda. Short and clear
 
Ukute anakutishia tu na hana lolote baya atakufanyia.
Usiseme hivyo, mpaka kwa mabosi ameshaanza kuharibu, ukizingatia ni mkubwa wangu kwa cheo. Pia ni mtoto wa mtu mzito sana nchi hii, hii nimekuja kutonywa hivi karibuni na rafiki yake na akataka iwe siri, kifupi wote ni mboga 7
 
Huyu ni binti ambaye alikuja kwangu kwa gia kama ya dada. Ni mfanyakazi mwenzangu.

Kiukweli ni binti mzuri tu Manka wa huko kaskazini. Sasa mimi nilimchana kuwa sijamuelewa so sitaki kumchezea

Ikawa nimetangaza uadui yani ananichukia na sijui sababu, na nina mashaka anaweza nitumia hata majambazi.

Chuki yake kwangu ni kubwa sana, ameahidi kuniharibia, salamu hajibu na kanichunia. Anaeneza sumu mpaka kwa mabosi, uzuri ni waelewa.

Nilimkataa kwa sababu huyu binti ana dharau na mjuaji sana, aliwahi kumkataa kwa madaha jamaa yangu aliyejitosa kumtongoza, tena kwa heshima mno.


Nilichoumia sana ni kuwa jamaa yangu ni mtu mstaarabu sana, ni nice guy mzuri mno sasa kwa nini ajibiwe kwa dharau wakati hakustahili?

Na sio huyo tu, ni tabia zake kwa karibu kila mwanaume anayejitosa kumtongoza. Anajiamini sana for nothing


Napambana naye vipi huyu?

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
Hajawahi kuwa rejected, so haamini na kujiona mzuri, mkazie hapo hapo.
 
Japo kuna watu wamekutusi na wataendelea fanya hivyo, mie kwa upande wangu nakupa heko, mdada akishaonesha dharau kwa mtu yeyote mbaya zaidi huyo mtu nijuee ni mstaarabu basi akarage bao, Kutongozwa sio issue kama hakumuelewa jamaa angekataa kiustarabu kama mtu mzima.

Achana na hizi pimbi zinazokuita we mvulana
Na nyongeza zaidi, mthibitishie kuwa, ye kuwa mzuri haimaanishi anaweza mbambaisha mwanamme yeyote mbele yake.
 
We huoni kama hiyo sio DHARAU, Kama mzuri kwanini hujampenda?.

Ni kheri ungemwambia tu sijakupenda kuliko kumsifia halafu unamtosa.
Sio dharau kabisa ukilinganisha na alivyosema yeye kwa jamaa yangu na wengine. So kwa hapo ni kama hoja yako haina nguvu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom