Ninauguliwa na baba watoto wangu

Ninauguliwa na baba watoto wangu

Status
Not open for further replies.

Mamndenyi

Platinum Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
44,623
Reaction score
64,481
Salaam sana wana MMU wote;

Nimekuja kwenu rasmi kuleta taarifa hii ya kuuguliwa na bwana ambaye nimezaa naye watoto wangu wote wanne.

Kweli tulifikia mahali kimaisha tukatengana tokea 2001. Kila mmoja akiwa na maisha yake huku nikiwa na changamoto kubwa na kali za kulea watoto ambao ilibidi nibaki nao, hayo kwa sasa tuyaweke pembeni.

Hadi ninavyoandika huu uzi hakuna mtoto hata mmoja ambaye ameshapata kibarua wote wapo kwenye kuhangaika kutafuta kazi.

Ilipofikia mwaka jana mwishoni nikapata taarifa ya kuwa yule bwana niliezaa naye anaumwa, nikajuwa ni homa za kawaida tu.

Leo kaka yake ndo ananipigia simu na kusema kuwa mdogo wake amezidiwa sana na alikuwa amezimia ila kazinduka tena juzi.

Kwangu hiki kitu ni kikubwa nimeshindwa kukibeba.

Kwenu wana jamii kwa upendo wenu ninaomba mnichangie nauli ili niweze kwenda huko Mbeya kumwona huyo mgonjwa. Kama mnavyojua mahali penye ugonjwa mkubwa pia panahitajika hela ya matumizi mengineyo.

Kwa wana jamii wa Mbeya mnaweza kwenda kumuuona nyumbani ni Sae.

Naomba tu msinitukane maana nitalia;
 
Kwani kwa muda wote huo huna mtu unaembatana naye katika mahusiano?yeye naye anasemaje,katoa ruhusa uende au unataka utoke kiaina ili ukamuuguze huyo ex wako,maana atakuwa anajua in and out ya uhusiano wako na huyo mtu kabla yake yeye...
 
Pole sana dada/mama,
Matatizo yapo na hakuna aliyeumbiwa matatizo, huo ni wakati tu, UTAPITA.

2001-2018 = 17
Sitaki kuhoji sana ila tu nimeguswa na hilo tatizo lako..
Tujulishane ni njia ipi itatumika ili kukuwezesha kwa chochote tutakachobarikiwa.

Haka kamstari katakufaa pia,

Zaburi 121
Nitayainua macho yangu niitazame milima, msaada wangu utatoka wapi?
Msaada wangu u katika bwana aliyezifanya mbingu na nchi.
 
Asanteni kwa wote mlioguswa na ujumbe wangu huu;
Mungu awabariki tu jamani;

Kuna aliyeuliza kama nilishaingia mahusiano mengine, jibu ni hapana;
nilikuwa na changamoto kubwa ya kusomesha sikuweza tena kuanza mahusiano.

Yupo pia alieuliza why nimekosa nauli, hapa siwezi kusema sana ila kweli
hela ingekuwepo wala nisingekuja huku;

Naomba niweke tu namba yangu kwa ajili
ya hao wapendwa waliouliza huko juu 0755 557094.

Asanteni sana!
 
Asanteni kwa wote mlioguswa na ujumbe wangu huu;
Mungu awabariki tu jamani;

Kuna aliyeuliza kama nilishaingia mahusiano mengine, jibu ni hapana;
nilikuwa na changamoto kubwa ya kusomesha sikuweza tena kuanza mahusiano.

Yupo pia alieuliza why nimekosa nauli, hapa siwezi kusema sana ila kweli
hela ingekuwepo wala nisingekuja huku;

Naomba niweke tu namba yangu kwa ajili
ya hao wapendwa waliouliza huko juu 0755 557094.

Asanteni sana!
Mwenyezi Mungu akutie nguvu
 
Duh..mamdenyi kumbe ni mhengaa....!!?? 2001 ndo uliachana na mme...! Na tayari ulikuwa na watoto 4,yaani km ulizaa kwa wastani wa miaka 2.9,ina maana umeolewa kati ya 1989 au 1990. Me wakati huo nasoma darasa la 4 au 5. Hakika we Dada yangu, lazima nikuchangie mhenga!!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom