Countrywide
JF-Expert Member
- Mar 2, 2015
- 18,186
- 27,231
Leo imenibidi niliongee hili ili niae huru kwa maana moyo unauma kuona uongo uzushi chuki na fitna kwa Mama Samia.
Ninaona ni kama watu wamejipa ajira ya kudumu ya kukosoa maraisi. Kukosoa sio dhambi Ila inategemea na unachokosoa.
Hadi Sasa sijaona kama kuna jambo la kumkosoa Mama Samia, nasema SIJAONA KABISA.
Kuna watu pengine wanalipwa kwa kuikosoa serikali, hivyo serikali ifanye vizuri au vibaya wao wanakosoa tu.
Sasa jiulize unamkosoa mama Samia kwenye lipi? Ni kipi kakosea hadi Sasa hadi muanze midomomidomo?
Mara sijui kwa nini avunje vibanda, sasa kama kaona hawafati Sheria kwa nini asivunje?
Mtu anakurupuka anasema ooh kwa nini sijui kampa mwinyi gari, gari kweli? Tena kwa raisi mstaafu ni issue?
Wengine ooh sijui kasababisha mechi isichezwe? Akili za namna gani hizi? Ikatokea ukakutana na kibaka huko mtaani akakukaba utasema pia Mama Samia ndio kamtuma?
Hakuna mwenye hoja kabisa ya kukosoa zaidi ya ushabiki tu. Tuache ushabiki tuchape kazi.
Wanaojiita wanaharakati na yule jamaa yenu mliekuwa mnamuabudu kule Twitter nao kila siku wanatafuta kwa nguvu la kuzusha ili tu Mama Samia aonekane hafai, sijui wenzetu walisaini mikataba ya kukosoa serikali?
Unamkosoa Mama Samia kwa lipi baya? Acheni hizo, Ila tutaenda sawa maana kukosoa mnasema ni Uhuru wenu Ila hata sisi kuwakemea nyie ni Uhuru wetu.
Mama Samia kanyaga twende!
#kazi iendelee
Ninaona ni kama watu wamejipa ajira ya kudumu ya kukosoa maraisi. Kukosoa sio dhambi Ila inategemea na unachokosoa.
Hadi Sasa sijaona kama kuna jambo la kumkosoa Mama Samia, nasema SIJAONA KABISA.
Kuna watu pengine wanalipwa kwa kuikosoa serikali, hivyo serikali ifanye vizuri au vibaya wao wanakosoa tu.
Sasa jiulize unamkosoa mama Samia kwenye lipi? Ni kipi kakosea hadi Sasa hadi muanze midomomidomo?
Mara sijui kwa nini avunje vibanda, sasa kama kaona hawafati Sheria kwa nini asivunje?
Mtu anakurupuka anasema ooh kwa nini sijui kampa mwinyi gari, gari kweli? Tena kwa raisi mstaafu ni issue?
Wengine ooh sijui kasababisha mechi isichezwe? Akili za namna gani hizi? Ikatokea ukakutana na kibaka huko mtaani akakukaba utasema pia Mama Samia ndio kamtuma?
Hakuna mwenye hoja kabisa ya kukosoa zaidi ya ushabiki tu. Tuache ushabiki tuchape kazi.
Wanaojiita wanaharakati na yule jamaa yenu mliekuwa mnamuabudu kule Twitter nao kila siku wanatafuta kwa nguvu la kuzusha ili tu Mama Samia aonekane hafai, sijui wenzetu walisaini mikataba ya kukosoa serikali?
Unamkosoa Mama Samia kwa lipi baya? Acheni hizo, Ila tutaenda sawa maana kukosoa mnasema ni Uhuru wenu Ila hata sisi kuwakemea nyie ni Uhuru wetu.
Mama Samia kanyaga twende!
#kazi iendelee