Ninaacha Ualimu tangu leo

Ninaacha Ualimu tangu leo

Daah na inatia hasira ukisikia ESICUROUW imepigwa ka 170billion afu watu wanasema za mboga lazima hasira zikuzidie
 
Nimaamuzi mazito hila yanaitaji weredi Wa kutosha kulingana na ulivo na mishe unazoweza kuanza nazo
 
Dah nilivyosoma nimeumia sana, yaani una deni LA miaka mitatu hujalipwa halafu uandike deni jipya tena! Hii inauma sana, maisha ambayo wanaishi walimu wetu yanatia huruma sana lakini bado kuna watu hawana huruma na walimu, hii ndio kada ya watoto wa maskini. MTU mshahara mdogo nauli humo humo, kodi ya nyumba, chakula kazini(achana na cha family), umeme, maji halafu kuna MTU analipwa mshahara wa ml.5+ na vitu vyote hivyo analipiwa na serikali.

Usiache ndugu yangu komaa hivyo hivyo Magufuli na Majaliwa niamini watafanyia kazi matatizo ya walimu.
 
Vipi ticha number zinasomeka?
Utajuta kwa nini uliuza haki za watu kwa kusaidia mfumo onevu.
Pongezi kwa kula kile ulichopanda.
Sasa panda mbegu sahihi, usirudie makosa.

Unaamini kuwa walimu ndo huwa wanaofanya CCM ishinde?
 
Acha kumfundisha mwenzako uoga wa Maisha,kuajiriwa sio kipimo cha mafanikio kimaisha.

Maana yangu ni kwamba atumie kuajiriwa kama opportunity ya kukopea halafu aanzishe mradi utakaomsukuma mbele. Nina hakika post #12 na #14 umezipitia na kuona advice waliyotoa, iko perfect
 
dada yangu ni mwalimu lakini jamani mbona waalimu wanadharauliwa sana
 
Dogo karibu kitaa, huku unajilipa kwa kiwango cha upambanaji na ubunifu wako, kunahitaji nidhamu yaipango na usimamizi binafsi,ukizingatia wewe ndo utakuwa boss na mtekelezaji wa mipango yako, kuna kupiga sana na sometime kupigwa na life pia, ila kujiajiri kutam ukiwa unaona mbali. Nimewahi kuwa teacher 4 2yrs kabla sjabadili mwelekeo, haikuwa rahis but now huwezi amini nimepiga hatua kubwa zaidi ya teacher aliyelipwa mafao japo kitaa nimekuwepo miaka michache. Usiwe mwoga wala kusita kama umeamua

Tupeane maarifa mkuu na mim nafkria hivyo
 
Mimi nimeshaacha kujitambulisha mwalimu, unaonekana bure mbele za watu
 
Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.

Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.

Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA

Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?

Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .

hapa kuna kundi la waoga litakukatisha sana tamaa ila usirudi nyuma...kwani huku mtaani wanakodai kugumu watu wanaishi vipi?

Mimi pia nilikuwa nafundisha chuo cha private na nikaacha kazi mwaka 2013 baada ya kuona siwezi kutoka kwa namna yeyote ile, wengi walinibeza kwamba nitarudi. tu huko...ila mpaka sasa wanashangaa sina muda na hizo ajira zao na maisha yanaenda!!

Nina miradi ambayo inaniingizia zadi ya 2m kwa mwezi..wapi ningepata mshahara wa aina hiyo?
 
huo ualimu wenzio wanaenda mpaka kuroga walau waupate then we unaukataa.angalia usije lujutia uamuzi wako kijana
 
Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.

Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.

Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA

Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?

Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .
Wapo wa kuacha kazi lakini si wewe,,
 
Ualimu una kero na manyanyaso mengi sana na hasa inapofikia kwenye haki yako. Mimi pia ni miongoni mwa watu ambao naelekea kuacha hiyo kazi. Afisa elimu ananizuia kwenda kusoma na wakat nimepata mkopo kisa sipo kwenye mpango wakati hata ukiwekwa kwenye mpango wanakuambia ujisomeshe. So ukitaka kufanikiwa kwenye ualimu lazima ukubali kutake risk
 
naona ni muda sasa wa mheshimiwa jpm na majaliwa kassim kuliangalia hili la walimu!! haiwezekan nasema haiwezekan kabisaaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom