Ninaacha Ualimu tangu leo

Ninaacha Ualimu tangu leo

Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.

Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.

Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA

Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?

Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .
usifanye maamuzi makubwa kama hayo kwa hasira mkuu,kama unataka kuacha kazi jipange kwanza ujue utaenda kufanya nini na utakumbana na changamoto gani, kufanya maamuzi yenye impact kwa maisha yako unatakiwa uwe umetuliza akili
 
Mwee masikini walimu,kamshahara kadogo na tufedha hutu wanakatwa daa,hivi Rais,PM,Mama rais wote hawa si walimu?
 
Au mpaka wagosi wa kaya wawasaidie kutetea maslahi yao?Magufuli kama kweli ww unayejitambua angalia upya mishahara yao.
 
Kazi yoyote ya kuajiriwa ina utumwa ndani yake.
Sikubaliani na uamuzi wako kwa sababu umetokana tukio la ktokulipwa. Ulipaswa ufikirie hilo hata kabla ya kuingia ualimu.
Pia nakushauri usiende kwa pupa. Hebu tumia kazi yako ukusanye mtaji kiasi kwa sababu kuna fursa na wewe bado kijana. Ukipata kiasi fulani kulingana na ulichopanga sasa unaweza kuanza mradi wako na kuachana na ualimu. Pia ukimbuke umesaini mkataba.
 
mi nakushauri usiache kazi kama hujapata kazi kwingine na mkataba ukasain, fanya hivii tafuta kishughuli chakifanya unaiba mda wa serikali unazalisha hadi basi, njoo asubuhi unachechemea omba ruhusa, mara una mgonjw ukizalisha hela yako ikarudi na nauli plis mda walokupotezea rudi kazin vizur
 
Mkuu sirudi nyuma, kabla ya kuwa mwalimu mie nilikuwa fighter kitaa na nilikuwa silali njaa. Siwezi kuwa mtumwa kwa haki yangu kabisa nnayohistahili.

Mkuu mkwanza nakupa hongera kwa hatua uliyoichukua.

Ualimu wa Tz ni ukichaa,kazi utafanya weee ila maslahi utayapata kwa kusota.

Maafisa elimu wengi wao ni vichwa maji,wababe,wasiojua wajibu wao wala majukumu yao. Wao ni ngono tu na rushwa zisizokuwa na vichwa wala mkia.

Ukiwa mwalimu utaishia kudharaulika mbele ya jamii yako inayokuzunguka,wanafunzi wako na kila mtu( hata serikali inadharau walimu-nadhani mliona alichokuwa akifanya kikwete na kushangiliwa na wazee wa Dar ambao mimi niliwaona ni wahuni tu).

Zamani ualimu ulikuwa ni kazi ya heshima sana,utapendwa na jamii yote na kuheshimiwa na wanafunzi wako,hali ilishabadilika kitambo sana- leo wazazi wanawachukia walimu,wanafunzi wanawadharau walimu wao na kuwaona maskini wasiojiweza,watu wasio na kipato chakueleweka,waganga njaa na maadui wao! Hakuna upendo tena.
Serikali imewatupa walimu,inawadharau,inawachonganisha na jamii,mfano mkuu wa mkoa anaweza akawatangazia wazazi wasilipe mchango wa mlinzi kwakuwa ni jukumu la serikali,alafu mkurugenzi na afisa elimu wakagoma kutoa mshahara wa mlinzi wakitaka wananchi( haohao waliotangaziwa na mkuu wa mkoa wasilipe- ndio walipe)?

Mwalimu ni yatima kiukweli maana hata hiyo CWT ni ya makada wa CCM,ukiwa kiongozi wa CWT msimamia haki kwa walimu basi utajuta,utavalishwa kila aina ya ubaya na majungu.....

Binafsi niliamua kuacha ualimu mara tu baada ya matokeo yaliyoirudisha CCM madarakani mwaka huu,na niliweka uzi wangu humu jukwaani,nitarudi baada ya miaka minne kutoa ushuhuda wangu wa mafaniko niliyoyapata nje ya ualimu.

NB:- Ajira usiyoifurahia ni utumwa grade A.
 
Dumelang

Wazo zuri mkuu lakini unaenda bila kujiandaa, mwisho wa siku utasema aheri ya jana. Unaweza kuchukua muda mrefu sana kukaa sawa tofauti kama ungeacha wakati tayari una mpango mkononi. Sitisha maamuzi magumu na fikiria maamuzi ya busara kwa mustakabali wa maisha yako.
 
Last edited by a moderator:
Dogo karibu kitaa, huku unajilipa kwa kiwango cha upambanaji na ubunifu wako, kunahitaji nidhamu yaipango na usimamizi binafsi,ukizingatia wewe ndo utakuwa boss na mtekelezaji wa mipango yako, kuna kupiga sana na sometime kupigwa na life pia, ila kujiajiri kutam ukiwa unaona mbali. Nimewahi kuwa teacher 4 2yrs kabla sjabadili mwelekeo, haikuwa rahis but now huwezi amini nimepiga hatua kubwa zaidi ya teacher aliyelipwa mafao japo kitaa nimekuwepo miaka michache. Usiwe mwoga wala kusita kama umeamua
 
Kaka usikate tamaa, lumbuka nchi jnaongozwa na waalimu, nakusihi pigania haki zako na kwa vile una ujanja wa kuja hadi kweny mitandao.. Unaweza kufikisha ujumbe wako kwa wahusika kirahisi sana.
Fight for your right and never give up!

Yale yale ya shemeji unatuachaje! Usijidanganye,hakuna cha mwalimu wala mavi yake mwalimu,kwani hao maafisa elimu na hao wakurugenzi (wanaonyanyasa na kukwamisha juhudi za walimu)si 90% ni walimu?
 
Nafasi itazibwa mwez march. Kuna walimu weng wapo mtaani wanatamani hata kuipata hyo laki4 unayolipwa.
 
Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.

Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.

Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA

Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?

Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .

ualimu ni utumwa na maalumu kwa watu waliokosa mwelekeo wa masomo mengine.,kuwa mwalimu tanzania ni fedhea,minyororo ya kifungo cha ualimu nimizito lakini ukikata kwa kudhamiria unafanikiwa
 
Mkuu pole sana kwa hayo matatizo, ila nakushauri usiiache kazi ya ualimu hata huko uendako kwani Taifa hili lina wajinga wengi kwa hyo endeleza vita ya kuupiga vita ujinga hata huko uendako
 
Hapo kijana mimi naona umekwepa jukumu la kudai haki yako pambana kwanza upewe haki yako alafu ndio utoe maamuzi ya kuacha kazi.Usitukane mkunga ungali bado una kizazi,Andika barua ya likizo isiyo na malipo ndio usepe mambo yakiwa magum utarudi kazin.
 
Dumelang acha upumba.v.u ungekuja kuomba ushauri sio kuja na conclusion zako, eti kuanzia leo naacha kazi. Ebu tafadhali sana fuata ushauri wa post #12 na #14 maana kuna walimu wengi wametoka kwa kuanzisha miradi baada ya kukopa, maisha si lelemama

Punguza hasira mdogo wangu jipange una majukumu mbele

Acha kumfundisha mwenzako uoga wa Maisha,kuajiriwa sio kipimo cha mafanikio kimaisha.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu inauma sana haki yako inapodhurumiwa ukijua, sasa suala langu inaonesha ni mchezo huu maana huwezi sema pesa za wasimamizi zimeisha mie nilipwe kwenye OC wakati idadi ya wasimamizi inajulikana, sasa kazi gani ya kunyonyana hii? Bora ku hustle ukijua nakula kwa haki, na siibiwi naona.
ni kweli kuna maafisa wanafanya usanii but nikushauri ujiridhishe kwanza na huko ueandako, unaweza kuacha kazi kinyemela kwanza
 
Laokini kuwapomya ungemwandikia katibu mkuu sagini, mkurugenzi wako, waziri mkuu, na copy kwa magufuli halafu ndo uondoke uwashe moto watauzima mbeleni huko.
Barikiwa sana
 
Hongera kwa kuacha utumwa, Mimi mwenyewe najipanga kuacha huo utumwa
 
usiache kazi pambana humu ndani kuondoa huo mfumo unadai unanyima haki. lakini kama umekwazika sana omba likizo ya dharura ili utafakari na kuomba ushauri kwa watu makini. uhakika wa fedha kila mwezi hata kama ni kidogo ni bora kuliko bahati nasibu ya mtaani. labda kama umeshakuwa na mradi ukiwa mwalimu na unaenda kuongeza nguvu kazi na capital. kinyume chake unaweza haribu maisha yako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom