Nina maswali kadhaa kuhusu mwenge

Mwenge ni jadi, mila na desturi ya taifa hili, kamwe haitatokea tukaacha kukimbiza mwenge. Jiulize wewe kwanini usirudi tumboni kwa mama yako na uachane na shida na raha za Duniani 🤣🤣
Faida yake ndio hiyo tu katika kudumisha hivyo?
 
Aisee,,,
Unataka kuleta laana kwenye nchi yetu
Nakumbuka niliambiwa na Babu yangu kuwa ule mwenge unatumia mafuta fulani ambayo hayazimiki, kwa kweli nilikuwa mdogo sana kuuliza ni mafuta gani na yanatokea wapi
Na akasema ikitokea ukazimika, nchi nzima itapata majanga ya maafa na watu wengi watapoteza maisha yao
Kwa kweli hapana 🙌🙌🙌,
Na wewe ukakubali kwa maana kwamba kabla ya uwepo wake huo mwenge hayo majanga yalikuwepo?
 
Mwenge ni jadi, mila na desturi ya taifa hili, kamwe haitatokea tukaacha kukimbiza mwenge. Jiulize wewe kwanini usirudi tumboni kwa mama yako na uachane na shida na raha za Duniani

Kipi kilitangulia kuwepo? Mwenge ama Tanganyika / Tanzania? Watu waliishije kabla ya Mwenge kuwepo na walipata faida gani ya ziada baada ya Mwenge kuwepo?


(Husiniambie kuhusu uzinduzi wa miradi)





Mfano uliotoa hauendani.
 
Kun Historia ikonjyuma ya Pazia kuhusu Mwenge. Inasemekana yalikuwa ni maagizo ya zindikiko. Lilifanywa na Wazee baada ya Uhuru hukooo Bagamoyo!
Kuna Mwamba anaitwa Forojo Ganze ndiye aliyemwambia Nyerere aanzishe Mwenge ...na alitamka Yale maneno...Sisi tunataka kuwasha Mwenge...
Like ni zindiko kubwa sana ,Ndio maana VIONGOZI huwa wanaapa na luoazimika.kuushika Mwenge!
Huwa Kuna utani kuwa ukishika tu huo Mwenge lazima uwe ja tabia za kivhawachawa!
Kwa maelezo zaidi google Stori za Forojo Ganze!
 
Hua nashangaa Sana serikali inavyo teketeza mabilioni ya fedha kuzungusha ule moto,

na wakati huo bado zahanati na wataalamu wa afya hawatoshelezi mahitaji, bado maji ni tatizo lisilo na ufumbuzi, umeme pia bado hautoshi, shule na vifaa vya kufundishia ni mgogoro usio na mwisho na mengine mengi ambayo hiyo fedha wanayo iharibu kwenye kuzungusha moto ingetosha kufanya, alafu fedha zenyewe bado wanakopa Kila mwaka na kuja kuziharibu,

Kwa nini ule moto usiwekwe makumbusho tuu atakae kuuona aufate makumbusho akautazame, mbona uingereza walio itawala hii nchi Wana mwenge lakini hawa potezi fedha na muda kwa kuukimbiza 🤔🤔 serikali iache kuchezea pesa na wakati zina mahitaji mengi Sana ya msingi
 
Maswali yangu ni kama ifuatavyo:
1)Tukiachana na blah blah faida inayopatikana kwa kuukimbiza mwenge ni nini hasa baada ya mabilioni kuteketea kwenye ukimbizaji wa mwenge ni kitu gani kinapatikana.

2)Mwenge huwa unahifadhiwa wapi(Mkoa) na mahali gani(jengo)?

3)Kiongozi wa mbio za mwenge huwa anachaguliwa kutoka wapi?

4)Je mwenge ukianza kuzunguka ni kweli hauzimwi?

5)Kuna uvumi nimekuwa nikiusikia wanaokimbiza mwengi huwa wanadanji uvumi huu unatokana na nini?

6)Mwenge unapokuwa sehemu kuna takribani watu wanne au watano wanatengeneza duara kuuzunguka mwenge kwa karibu kiasi cha kuvuta ule moshi na wanakuwa hapo kwa muda mrefu wakiwa wameunganishana je maana yake ni nini na je ule moshi wanaouvuta kwa muda wote ule hauwezi kuwaletea madhara?

7)Je mwenge ni mmoja huo huo miaka yote au huwa unatengenezwa kila baada ya muda fulani?

8)Nini asili ya mwenge na ulianza rasmi lini na kwa nini unahusishwa na uchawi?

Nadhani maswali haya yanatosha pengine nikipata majibu ya maswali haya kutoka kwenu nitaongeza maswali mengine

Huwa nauona mwenge kama ni kitu ambacho kinaabudiwa kama ambavyo masanamu yanavyoabudiwaga vile watu wanavyoukusanyikia nawaona kama wapo kwenye ibada kwa mungu Tamuzi au baphomet
1. Faida: Kukagua miradi mbalimbali iliyojengwa kwa fedha za umma na ile iliyotokana na michango ya Wananchi. Lengo kuwakumbusha watendaji kutolala kwani Mwenge utawaunguza. Pesa zinazohudumia Mwenge wa Uhuru zinatokana na michango ya hiari kutoka kwa Watanzania Wazalendo. Serikali inatoa bajeti ndogo sana ya Mwenge.

2. Baada ya kuzimwa, Mwenge wa Uhuru unahifadhiwa kwenye Makumbusho ya Taifa.

3. Ni jukumu la Rais wa JMT kumchagua Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru akishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) ambao nao huchagua Wakimbiza Mwenge wa Uhuru wengine kufanya wawe Sita Kitaifa.

4. Literary, hauzimwi, lakini linapokuja suala la kuongeza mafuta na kuufanyia services ndogo ndogo, unazimwa ila kwenye sehemu maalum.

5. Kufa ni kwa binadamu yeyote, anayekimbiza na hata ambaye hajawahi kuuona licha ya kuukimbiza wanakufa. Wapo ambao waliwahi kufa, lakini wapo wengine wapo hai hadi Sasa. Mfano, Kamanda Jordan Rugimbana na Mzee Sukwa Said Sukwa kutaja wachache.

6. Wanaouzunguka mara nyingi ni askari (FFU), Skauti au Vijana Shupavu kutoka UVCCM, ila LAZIMA wawe wameandaliwa kwa kazi hiyo. Lengo ni kuukinga na upepo usizimike.

7.Kila mwaka unatengenezwa mpya kwa ajili kuukimbiza kwa mwaka husika. Mwl. Nyerere alikuwa na vifimbo zaidi ya mia, lakini watu waliamini ni kamoja tu! Ahahahahaha!!!

8. Ulianza rasmi mwaka 1961 pale Ndugu Nyirenda alipouweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Asili yake ni kutokana kauli ya hekima kutoka kwa Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliposema, " Sasa tunakwenda kuwasha Mwenge Ili umurike ndani na nje ya mipaka yetu.....!" Hakuna Imani za kishirikina wala nini ingawa huwezi kuzuia waja kunena!

Naamini kwa majibu yangu hayo umepata uelewa kidogo kuhusu Mwenge wa Uhuru. Karibu kwa maswali mengine!
 
Maswali yangu ni kama ifuatavyo:
1)Tukiachana na blah blah faida inayopatikana kwa kuukimbiza mwenge ni nini hasa baada ya mabilioni kuteketea kwenye ukimbizaji wa mwenge ni kitu gani kinapatikana.

2)Mwenge huwa unahifadhiwa wapi(Mkoa) na mahali gani(jengo)?

3)Kiongozi wa mbio za mwenge huwa anachaguliwa kutoka wapi?

4)Je mwenge ukianza kuzunguka ni kweli hauzimwi?

5)Kuna uvumi nimekuwa nikiusikia wanaokimbiza mwengi huwa wanadanji uvumi huu unatokana na nini?

6)Mwenge unapokuwa sehemu kuna takribani watu wanne au watano wanatengeneza duara kuuzunguka mwenge kwa karibu kiasi cha kuvuta ule moshi na wanakuwa hapo kwa muda mrefu wakiwa wameunganishana je maana yake ni nini na je ule moshi wanaouvuta kwa muda wote ule hauwezi kuwaletea madhara?

7)Je mwenge ni mmoja huo huo miaka yote au huwa unatengenezwa kila baada ya muda fulani?

8)Nini asili ya mwenge na ulianza rasmi lini na kwa nini unahusishwa na uchawi?

Nadhani maswali haya yanatosha pengine nikipata majibu ya maswali haya kutoka kwenu nitaongeza maswali mengine

Huwa nauona mwenge kama ni kitu ambacho kinaabudiwa kama ambavyo masanamu yanavyoabudiwaga vile watu wanavyoukusanyikia nawaona kama wapo kwenye ibada kwa mungu Tamuzi au baphomet
Mbio za mwenge kwenye hii karne ya 21 ni 🚮 tu na uchezeaji wa pesa za walipa kodi kwenye mambo ya kipuuzi.
 
Back
Top Bottom