Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

mshana umenigusa sana baba, naamin weng wamefanikiwa kutokana na kujitoa kwa moyo kwa watu wengne tofaut na ndug zao. Umenkumbusha mbal mbal mbaaal sana bado natafakar sana
Pls ukiweza share nasi unaweza kupata relief fulani moyoni
 
Ni jambo la kihisia mno, jambo lililo ndani ya moyo kabisa lisilotoka na ambalo hujirudiarudia kila Mara!

Ni kuhusu wema uliowahi kutendewa na mtu baki halafu ukaahidi kimoyomoyo kumlipa lakini isiwezekane kwakuwa hujawahi kuonana naye tena au pengine keshafariki.

Nakumbwa na hiyo hali! Namkumbuka mno Dada Jamila Mazoea R.I.P alinipenda sana na kunisaidia katika mengi, lakini kabla ya kuwa na uwezo wa kulipa wema wake kwangu alitwaliwa kutoka katika maisha haya.

Nilichoweza kumsaidia ni mwaka 1993 ambapo nilikutana naye akaniomba sh mia mbili ambayo nilimpa ile ya noti kipindi hicho, baada ya siku ile sikuwahi kuonana naye mpaka mwaka 2010 nilipoenda kwake na kuambulia kuonyeshwa kaburi lake!

Bado namkumbuka dadaangu JAMILA MAZOEA na kwenye ulimwengu wa roho analifahamu hili
Pole Mkuu Mshana,hata mimi nina tabia ya kuwa guilty iwapo sijarudisha hisani,hata hivyo Mungu atakufariji kwa kuwa nia yako ni nzuri kwa aliekusaidia Mkuu,R.I.P Jamila Mazoea.
 
Pole sana endelea kumuombea Mungu ili roho yake ipumzike kwa amani.
 
RIP dada Mazoea...........wengine huwa tunasaidia wengine lakini wanakuona kima.......ndio maisha lakini......
Daah Pretta na urembo wote huo mtu akuone kima?,anyway mimi umeshindwa kunisaidia niki rest in peace si utajikula roho sana mamii? au unamuogopa shemeji yangu?
 
Niliwahi kuanguka kutoka ghorofa ya tatu hadi chini, nikapelekwa amana, sio siri yule dada alinihudumia vizuri sana, kama vile private, niliwah kwenda cku moja wakaniambia ameingia shift nyingine, nakushukuru sana dada mary siku moja nitakuja kusema ahsante mbele yako
Mkuuu we ni kamilioni
 
Fb nimemtafuta kwa jina hilo but nahic nakosea unless awe hajaweka picha ambayo naweza kumtambua!

CRB nimeuliza tena kuna baadhi ya watu ambao nawafaham kabisa huko but kwa hilo jina hatambui (kitu ambacho nahic wanajuana kwa majina ya makumpuni yao zaid) unless watu wawe wanafahamian from a long way!

Ilikuwa hiv
Nilikutana na huyu mheshimiwa wakiwa kwenye semina ya CRB Mkoa fulani, hapo mahali walipotumia kisemina ndipo nilipokuwa napatumia sana kupata mkate wangu wa kila siku (tubiashara coz palikuwa panaleta watu sana) mtaji wangu ukiwa laki moja baada ya kuikusanya almost miaka 2 (you won't believe this )

Siku 5 za semina yao,alifanya haya!
1. (Sidhan kama alitaka kweli kununua biashara yangu) akawa ananisema kwa stail ya maswali sanaaaaaaaa! And of the day akanipa ushaur kama napenda na naweza nirud shule! Of which naona aligundua napenda ila maisha hayajaruhusu, (nakumbuka alisema unaonekana ukiwa binti mzuri rudi shule itakusaidia ) I DID AS HE DREAMED (nakumbuka hiyo day 2 ya semina ilikuwa, mda wake wote wa lunch alitumia hapo kupiga story na mimi) mwenyewe nikiwa niko busy kukaribisha watu kwa ajili ya riziki,

2. Day 3 ya semina, the same time, (lunch time) akaja akiwa anataka mrejesho wa ushauri wake je nimeuchukuliaje ! Nilianza kumuona kama ananifuatilia sana maisha yangu, nakumbuka nilimjibu in a very like rude way! Wala hakuonesha kuchkizwa cha ajabu akanipa hela nikale (nakumbuka moyoni nilianza kumuona wale wale kasoro majina) akasema lifanyie kazi suala la shule!! Akaondoka

3. Day 4 ya semina yao, akaja na kunipa business card, aliongea sana siku ile, akiwa kagundua kuwa nampuuza, akasema acha na hizi biashara, nikisema nikusaidie mtaji iko siku utaibiwa na hakutokuwa na biashara tena, umri wako bado unaruhusu kurudi shule nenda shule! Akasema ukiwa tayar mda wowote niambie namba hizo hapo nimekula naongea na wewe kama mdogo wangu wala sio kama unavonifikia! Akaondoka ( only God knows nilivojisikia siku ile nililia sana Nilipofika home)

Siku ya 5 ya semina yao na ikiwa ndo ya mwisho mimi sikuenda , but nilipoenda nikakuta matatizo kwa secretary wa pale kwamba kuna mtu Anasema amekupa namba umpigie! Nilitumia simu ya yule dada, aliongea sana yule kaka, akasema ntapiga baada ya siku mbili uwe umetafuta shule!

In short,
Nilitafuta shule (kimasihara tu maana nilikuwa hata siamin) ajabu alituma hela nakumbuka kwa njia ya basi, akiwa amefunga na vitu vingine kukiwemo na simu (so mtu asingeweza kujua kama kuna hela na alimkabidhi dereva ) nikapokea na kurudi shule tena, na kila nilipohitaj maskin hajawahi kusita hadi nimeliza! (Ilikuwa level ya advance )

Niwakumbushe tu tangu ile semina hatujaonana kwa macho zaid ya kumweleza kwa simu nilipofikia na hajawah kunikatisha tamaa kabisa!
Na alilipa ada zoooooooote na pocket money juu! (Mtaniuliza wazazi wangu je! Yaachen it's another long story )

Nilitafuta kibarua, thank God nikapata, nikamwambia kwa simu tu (I took him more than a brother to me since then) good or bad nikapangiwa mkoa mwingine nikamjuza akanitia moyo sana kuwa maisha ni popote!

Tulivopoteana sasa,
Nikiwa kikazi kule tukavamiwa nilipokuwa naishi, was bad indeed (tuliibiwa kila kitu in short tulisafishwa na simu zikaibiwa)
Story yako japokuwa ni kwa ufupi ila imenipa kitu fulani ndani yangu.Mungu ambariki huko alipo na afanikishe kukutanisha nae kwa mara nyingine tena.
 
Ni ukweli kaka
Mm nilihamishia upendo wangu kwa mtoto wake mpaka mtoto anajiskia rakhaaa Ila namuambiaga kua marehem aliwahi kunitendea wema mkubwa sn. Sina cha kulipa zaid ya upendo Wa dhati kwako.
Wema auozi
 
Hili jambo mimi lilishawahi kunitokea. Mwaka 2013 nilijikuta kwa mara nyingine tena (ya 4) napoteza mtoto 😭. Ilikuwa very painful labour sitokaa kusahau sababu ilikuwa nusura mimi kufa. Nilijifungua na mtoto kupelekwa ICU ya watoto sema sikuwa na hofu sana maana nilimuona analia na Ana nguvu. Basi asubuhi ya tukio nikiwa na kiherehere cha kwenda kumnyonyesha mwanangu nafika nakuta wamama wote wamesubirishwa nje hawajaingia kwenye wodi. Basi sina hili wala lile. .. nasikia jina langu linaitwa. I was very excited to meet my baby. .. sema nikawa nashangaa mbona watu wananitizama sana. Basi mie nikaenda. Ile kufika kwa manesi nikajikuta nashikwa mkono na nesi moja kwa moja kwenye chumba maalum.

Basi sijui chochote naangaza macho kuangalia mwanangu alipo ndio nesi ananiletea kitrey mtoto amefunikwa akaniambia huyu ndio mwanangu amefariki asubuhi ya leo. Nilipigwa na butwaa sijui cha kufanya. Akaanza kuuliza historia yangu ya uzazi. Nikamweleza mimi huyu mtoto ni mimba ya 4 zingine zote zilitoka zikiwa kubwa sema inakuwa bahati mbaya.

Akanishauri sana. Akasema anaona nimekata tamaa ila nisihofu, nimuweke sana mbele Mungu maana kuna mengi yanatokea kwenye ulimwengu wa kiroho. Akaniambia mara hii tulia kwanza upe mwili na akili muda wa kusahau maumivu haya. Akashauri sana niupumzishe mwili kwani nitatengeneza kitu kinaitwa habitual abortion. Mwisho akaniambia nikijitambua nina mimba hata ya wiki 1 niende Muhimbili nitafute maspecialist kadhaa. Basi nikatoka na majonzi nikaendelea na maisha sema nilifuatiza ushauri wake na kuja ku conceive tena mwaka 2016.

Nikajifungua salama ila mara hii hadi madaktari walikuwa wananiambia huyu ana asilimia kubwa ya kuishi. Nikaanza ruti za kunyonyesha kwa masaa kwenye wodi. Siku ya 3 nakutana na yule nesi. Nikamuita kwa jina akashangaa namjuaje. Nikamweleza mimi ni fulani nilikuja hapa mwaka 2013 labda hunikumbuki ila nataka ujue kuwa ushauri wako kwa sehemu kubwa sana hasa masuala ya kiroho na kutibiwa muhimbili kumenisaidia sana Sana. Alishangaa akafurahi mno. Akaniambia ule ushauri alitoa sababu aliona maumivu makubwa kwangu ila anashukuru kuwa hata nilimkumbuka
 
Hii imenikumbusha teja mmoja maeneo fulani
Nikiwa njiani kwenye usafiri wa uma niliumwa kichwa kisichoelezeka,hewa ikawa nzito kupumua nikawa najiskia kutapika ilinibidi nishuke na nilitapika sana macho yakawa kama yanaingiwa ukungu nikaona kifo hichi hapa,huyu kaka alipotokea sikujua alinitafutia maji akanimwagia kichwani na mengine akanipa nikasukutua akatafuta mchanga wa kufukia matapishi na kunifuta miguuni na tshirt alilokua amevaa alisimama pembeni yangu mpk nilipopata nguvu ya kuamka hapo chini

Nilimshukuru na siku nyingine nilirudi hapo nikamuulizia sikufanikiwa kumuona mpk leo,ndani yangu nafeel kama sikumshukuru vizuri lakini sijui wapi naweza muona

Somo nililojifunza ni kitomdharau mtu koz hujui nani atakua msaada kwako,kwa macho ya nje anaonekana ni TEJA ila kwa macho ya ndani alikua MALAIKA kwangu


Cc Kingsmann
 
Dahh umenigusa sana aseeh mwaka 2001 iyo nipo mjin tanga nikiwa naenda shule galanosi nikajikuta nimeibiwa kila nilichokuwa nacho kwenye mazingira ya kutatanisha niliwaona wezi wale wakikimbia kwambali na mtu mmoja alikiwa kama anawakimbiza nikaenda mpaka police kufanya taratib walichukua bag lilikuaga na vitambulisho vyote na pesa.... Ikapita kama nusu saa yule aliekuwa anawakimbiza akaja pale police akiwa na bag lile na alikuwa anavuja damu mikonon inaonekana alipata shubir kidogo dahh alikuwa kaka mmoja mapolice walisema huyu ni mkichaa na kwel mavazi yake tu yalisema alikuwa na upungufu wa akili basi bana alipo kuja na lile bag alipo liweka pale akakimbia mbio dahh nilimkimbiza bila mafanikio ..... Nilienda shule ila nilikuwa namuwaza sana nilikuwa natoroka shule kuja kuzurura town kumtafuta bila mafanikio nikaja kuambiwa amepelekwa mirembe nilifurah kwakuwa mm home dodoma na uncle alikuwa anafanya kaz pale likizo nilipo fika sikulaz damu nikaenda mirembe kwel bana nikamuona alikuwa ameshaaza kupona tulipiga story nikamkumbushia ila hakukumbuka kitu nikamwambia kwa wema alionifanyia hata asipokumbuka nitamfanya kuwa bro wangu kabisa basi likizo yote ile nilikuwa naenda sana kumsalimia pale na alipo pata nafuu alirud tanga nimerud shule kumuulizia nikaambiwa aliporud tu hakukaa sana akafariki dahh RIP brother
 
Aisee nimejifunza vitu vingi sana katika Uzi huu ila cha msingi ni kuwa mwema na kuwatendea wema watu wengine hata bila kutegemea anything in return. Maisha ni mafupi , tuishi kwa wema maana wema hauozi, wema wako utakurudia siku moja
 
Ni jambo la kihisia mno, jambo lililo ndani ya moyo kabisa lisilotoka na ambalo hujirudiarudia kila Mara!

Ni kuhusu wema uliowahi kutendewa na mtu baki halafu ukaahidi kimoyomoyo kumlipa lakini isiwezekane kwakuwa hujawahi kuonana naye tena au pengine keshafariki.

Nakumbwa na hiyo hali! Namkumbuka mno Dada Jamila Mazoea R.I.P alinipenda sana na kunisaidia katika mengi, lakini kabla ya kuwa na uwezo wa kulipa wema wake kwangu alitwaliwa kutoka katika maisha haya.

Nilichoweza kumsaidia ni mwaka 1993 ambapo nilikutana naye akaniomba sh mia mbili ambayo nilimpa ile ya noti kipindi hicho, baada ya siku ile sikuwahi kuonana naye mpaka mwaka 2010 nilipoenda kwake na kuambulia kuonyeshwa kaburi lake!

Bado namkumbuka dadaangu JAMILA MAZOEA na kwenye ulimwengu wa roho analifahamu hili
So touching
 
Dahh umenigusa sana aseeh mwaka 2001 iyo nipo mjin tanga nikiwa naenda shule galanosi nikajikuta nimeibiwa kila nilichokuwa nacho kwenye mazingira ya kutatanisha niliwaona wezi wale wakikimbia kwambali na mtu mmoja alikiwa kama anawakimbiza nikaenda mpaka police kufanya taratib walichukua bag lilikuaga na vitambulisho vyote na pesa.... Ikapita kama nusu saa yule aliekuwa anawakimbiza akaja pale police akiwa na bag lile na alikuwa anavuja damu mikonon inaonekana alipata shubir kidogo dahh alikuwa kaka mmoja mapolice walisema huyu ni mkichaa na kwel mavazi yake tu yalisema alikuwa na upungufu wa akili basi bana alipo kuja na lile bag alipo liweka pale akakimbia mbio dahh nilimkimbiza bila mafanikio ..... Nilienda shule ila nilikuwa namuwaza sana nilikuwa natoroka shule kuja kuzurura town kumtafuta bila mafanikio nikaja kuambiwa amepelekwa mirembe nilifurah kwakuwa mm home dodoma na uncle alikuwa anafanya kaz pale likizo nilipo fika sikulaz damu nikaenda mirembe kwel bana nikamuona alikuwa ameshaaza kupona tulipiga story nikamkumbushia ila hakukumbuka kitu nikamwambia kwa wema alionifanyia hata asipokumbuka nitamfanya kuwa bro wangu kabisa basi likizo yote ile nilikuwa naenda sana kumsalimia pale na alipo pata nafuu alirud tanga nimerud shule kumuulizia nikaambiwa aliporud tu hakukaa sana akafariki dahh RIP brother
Emotional one
 
I had a friend. Mlisoma nae primary. Tulikua darasa la nne, Irene wangu alikua mchaga. It was so hard for me to make friends. And i was bullied so much at school. But when i met her things got better. No one bullied me anymore. Lakini alihama shule. Since then sijawahi kukutana nae tena na sijui alihamia wap. I hope I meet you again Irene you were my bestest friend.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom