Nina 70,000 niifanyie nini

Nina 70,000 niifanyie nini

Habari

Nimefanikiwa kupata kiasi cha 70,000 nahitaji hii pesa initoe kwenye dimbwi la umasikini.

Niifanyie kitu gani ambacho kitakuza mtaji haraka sana.

Nipo Dsm.
Mchague Lissu
 
Hiyo play master kacheze casino. Weka 40 unacheza Game la fruits & Seven ndani ya dk 6 kwa dau la mia 4 per spin unapata laki.
Kweli maisha ni mtihani, watu tuna akiba ndani , tuna nyumba n.k lakini kuna mtu anataka kufanya business kwa 70k.
Usife moyo
 
Hiyo play master kacheze casino. Weka 40 unacheza Game la fruits & Seven ndani ya dk 6 kwa dau la mia 4 per spin unapata laki.
Kweli maisha ni mtihani, watu tuna akiba ndani , tuna nyumba n.k lakini kuna mtu anataka kufanya business kwa 70k.
Usife moyo
Akiliwa imekula kwake mazima...hili wazo halina afya
 
Fanya kama huna hiyo hela,ifiche mahali usi ione kbsa kisha anza kusaka ajira kibarua yani Teseka lala njaa jitose kwenye maisha na wala usiikumbuke ile 70 kule ulipoificha,nina uhakika utapata tena hela.

ukipata tena kaifiche kule ulipoficha ile 70 ya mwanzo,ingia tena tafuta kbarua,saka pesa,saka kazi teseka hasa usichague kazi,utapata tena najua,chukua hyo amount kaongezee kule kwenye zile za mwanzo.

nenda na mwendo huo huo hadi utakapoona sasa nimechoka nahitaji kufanya biashara yangu nipumzike kidogo,katoe zile hela ulipokua unazificha angalia una kiasi gani kisha kwenye hiyo hela fungua biashara inayohtaji mtaji wa ile 70k ya mwanzo kbsa,yani fanya kama una 70k tafuta biashara ya mtaji huo fanya hela zingine ziache zikulinde na kuipa backup biashara yako itakapoyumba.
Mkuu nimekuona...💪💪💪
 
Ushauri huo Mgumu eti sio mrahisi kama unavyoonekana yahitaji ajikatae kweli

kama haelewi nini maana ya kujikataa huo ushauri hatoweza ufanya maana ni sawa

na morani kutahiriwa bila ganzi,yani ile unasimama wima ngozi inakatwa huku ukitazama.
Kweli kabisa mkuu.
 
Ngoja nikusaidie ili ifike 90,000/= leo leo. Fanya hivi nenda Kurasini Mivinjeni kuna jamaa ana kontena anauza apples frm SA..box 57,000/= chukua box lenye apple 90. Tafuta sehemu kkoo, uweke box upakie baadhi kwenye mfuko. Pita madukani uza apple moja 1000. Masaa mawili mzigo umekata.

Nakupa hii sababu mimi ninaifanya kila ijumaa.

Uzuri wa box linalokaa apple 90 ni makubwa sana so yanamvutia mnunuzi. Utapata wateja parmanent ambao watakua wanachukua lets kila wiki.
Sorry, hv ukimuuzia mwenye duka kea 1000 yy atauza sh ngapi?
 
Fanya kama huna hiyo hela,ifiche mahali usi ione kbsa kisha anza kusaka ajira kibarua yani Teseka lala njaa jitose kwenye maisha na wala usiikumbuke ile 70 kule ulipoificha,nina uhakika utapata tena hela.

ukipata tena kaifiche kule ulipoficha ile 70 ya mwanzo,ingia tena tafuta kbarua,saka pesa,saka kazi teseka hasa usichague kazi,utapata tena najua,chukua hyo amount kaongezee kule kwenye zile za mwanzo.

nenda na mwendo huo huo hadi utakapoona sasa nimechoka nahitaji kufanya biashara yangu nipumzike kidogo,katoe zile hela ulipokua unazificha angalia una kiasi gani kisha kwenye hiyo hela fungua biashara inayohtaji mtaji wa ile 70k ya mwanzo kbsa,yani fanya kama una 70k tafuta biashara ya mtaji huo fanya hela zingine ziache zikulinde na kuipa backup biashara yako itakapoyumba.
Ni Kama masihara hivi ila huu ushauri Ni mzuri Sana.
 
Nenda kwenye duka la vyombo nunua zile bakuri za mifuniko zlizo transparent (maalufu kwa kotena) Kama kontena10 nadhani haizidi buku jelo kwakila1,kisu,kopo2 za tooth pick.kisha ingia Sokoni chukua,nanasi,papai,chungwa,tango,Ndizi,parachichi,Tikiti maji namatunda mengneyo.Menya matunda yako katakata Kisha weka kwakuchanganya kwenye izo kontena zako...ukimaliza nunua mfuko au kikapu,ingia town,maeneo yastend, garage,vijiweni,masaloon nasehemu zote zenye mikusanyiko yawatu ilio changamka.piga kila kontena bukubuku,au pia kata nakiwango chajerojero.nahakika Apo haiwez maliza iyo70 yako ila baada yawiki kadha utakuwa napesa yakutazama kikubwa zaidi
Nilitaka kusema hivi juzi nilikuwa moshi jamaa anauza sahan ya matunda kwa buku2 ila unakula unashiiba unatoa ela yako kwa amani kabisa natamani nikirud nimwone tena
 
Tengeneza salad ya matunda mkuu.
Nunua matunda tofauti tofauti Yani maembe, mapapai, ndizi, mananasi, matango, matikiti n.k
Halafu yaandae yaoshe vizuri, yakate Kate vizuri then weka kwenye vifungashio vile vya plastic vya rangi ya silver vyenye umbo la mstatili hakikisha unapack vizuri ziwe na mwonekano wa kuvutia.
Then tembeza, sahemu nzuri zaidi Ni vituo vya mabasi yaendayo mikoani au fukwe za bahari Kama Coco Beach mida ya jioni huko utakutana na wazungu na hata wabongo wa kishua wanaojali afya zao watanunua tu.
Kile kipact kimoja unaweza uza buku 2 hivi mpaka buku 2 jero. Hakikisha we mwenyewe uko smart kimuonekano ili ushawishi watu kununua bidhaa zako maana wengi wanaofanya biashara ya aina hii wanajiwekaga rafu rafu tu mpaka mtu unaweza hofia kununua hayo matunda kwa kudhani na yenyewe yameoza!
Au pia unaweza tengeneza juice ya matunda uuze.
Au kutengeneza bites mfano karanga za mayai (jaribu kujifunza namna nzuri ya kuzitengeneza hizi kuziongezea mbwembwe ziwe na ladha nzuri sio Kama wengi wanavyotengeneza kimazoea) unaweza ingia hata you tube naamini hutokosa videos zinazofundisha jinsi ya kupika karanga za mayai kiufundi zaidi ukajifunza. Na hizi pia ziweke kwenye vifungashio vile vya plastic vyenye umbo Kama la kakikombe hivi kenye mfuniko wake juu usiotoka. Ikiwezekana tengeneza na kanembo kako uwe unabandika kwenye vifungashio vya karanga zako nembo iwe na mvuto iwe na jina la kibiashara ulilolibuni la hiyo bidhaa yako. Hii itakufanya uonekane professional zaidi na kuongeza ushawishi wa bidhaa yako. Hizi ndude Mimi binafsi nazizimikia kinoma.
SIO karanga za mayai tu, kwa mtaji huo unaweza tengeneza bites za Aina mbali mbali Kama kachori, bagia, sambusa n.k muhimu ujitahidi kuwa mbunifu katika mapishi na uandaaji na USAFI pia.
 
Nenda duka la vyombo nunua birika2,vikombe vya kahawa,njiko la mkaa,chupa mbili za chai ingia Sokoni,chukua tangawizi,kahawa,Anza kupika kahawa na tangawizi,Asubuh wahi stend navituo vyadaladala watembezee watu,ukiweza pika nakashata Tembea nazo.....baada yawiki kadhaa utakuja kuleta mrejesho
Big up
 
Njoo hapa Dar, uuze mahindi ya kuchona, faida fastaa
 
Back
Top Bottom