ngara23
JF-Expert Member
- Aug 31, 2019
- 16,736
- 39,284
Nataka niwatie moyo vijana wanaohangaika na mitaji mikubwa, basi tumieni hicho kidogo ulicho nacho
Hakuna pesa isiyofanya biashara, pesa yoyote ina uweZo wa kufanya biashara na kuzaa nyingine
Hapa nitashare na wadau biashara ya kufanya ukiwa na mtaji kiduchu
1. Nunua WiFi 3 Kwa 70,000 funga sehemu za masoko.
Wifi 1 ina uweZo wa kuhudumia watu 20,
Gharama za bando la internet ni kubwa na watu wengi hawamdu hizo gharama za mitandao ya simu.
Sasa wewe tafuta angalau watu 10 tu wakupe 500 Kwa siku ambapo hapo utakuwa na uhakika wa kupata 15,000 Kwa siku Kwa WiFi zako 3 ukiwa umekaa bila kumwaga jasho
2. Biashara ya mkaa
Mtaji wa 200,000 una uhakika wa kupata gunia zaidi ya mbili
Watu wengi wa uswahilini hawana uweZo wa kutumia gasi au umeme
3. Biashara ya matunda
Nunua madeli mazuri katakata matunda tembeza huko 10,000 ya faida Kwa siku
4. Chuma chakavu
Mtaji wa 200,000 unakutosha kusota na kupambania mavyuma na kwenda kupima Kwa na agent wakubwa, hakika hutakosa faida mpambanaji
5. Biashara ya kuuza uji
Kama mwanamke hii inakufaa zaidi amka alfajiri au jioni uza zako uji mtaani tena kama kipindi hiki cha mfungo utapata pesa nyingi
6. Biashara ya viungo vya vyakula.
Hii biashara inalipa mno na ina mtaji mdogo mno, tunaenda kwenye kipindi cha sikukuu za Eid na pasaka ndo kipindi cha kupiga pesa
Tafuta hizo binzari, vitunguu swaumu, pilau masala, cocoa, karufu, iriki, mdarasani n.k
Uza Kwa watu wa maduka, au tembeza majumbani
Pambania ulipo
Hakuna pesa isiyofanya biashara, pesa yoyote ina uweZo wa kufanya biashara na kuzaa nyingine
Hapa nitashare na wadau biashara ya kufanya ukiwa na mtaji kiduchu
1. Nunua WiFi 3 Kwa 70,000 funga sehemu za masoko.
Wifi 1 ina uweZo wa kuhudumia watu 20,
Gharama za bando la internet ni kubwa na watu wengi hawamdu hizo gharama za mitandao ya simu.
Sasa wewe tafuta angalau watu 10 tu wakupe 500 Kwa siku ambapo hapo utakuwa na uhakika wa kupata 15,000 Kwa siku Kwa WiFi zako 3 ukiwa umekaa bila kumwaga jasho
2. Biashara ya mkaa
Mtaji wa 200,000 una uhakika wa kupata gunia zaidi ya mbili
Watu wengi wa uswahilini hawana uweZo wa kutumia gasi au umeme
3. Biashara ya matunda
Nunua madeli mazuri katakata matunda tembeza huko 10,000 ya faida Kwa siku
4. Chuma chakavu
Mtaji wa 200,000 unakutosha kusota na kupambania mavyuma na kwenda kupima Kwa na agent wakubwa, hakika hutakosa faida mpambanaji
5. Biashara ya kuuza uji
Kama mwanamke hii inakufaa zaidi amka alfajiri au jioni uza zako uji mtaani tena kama kipindi hiki cha mfungo utapata pesa nyingi
6. Biashara ya viungo vya vyakula.
Hii biashara inalipa mno na ina mtaji mdogo mno, tunaenda kwenye kipindi cha sikukuu za Eid na pasaka ndo kipindi cha kupiga pesa
Tafuta hizo binzari, vitunguu swaumu, pilau masala, cocoa, karufu, iriki, mdarasani n.k
Uza Kwa watu wa maduka, au tembeza majumbani
Pambania ulipo