Ushauri wako ni hatua kwangu Biashara gani ya kimkakati kwa mtaji wa Milioni 30

Ushauri wako ni hatua kwangu Biashara gani ya kimkakati kwa mtaji wa Milioni 30

AU UNASEMAJE WEWE

  • Angalia wanaokuzunguka

    Votes: 4 50.0%
  • Kwani huwezi fanya maamuzi

    Votes: 2 25.0%
  • Muachie mungu

    Votes: 0 0.0%
  • Kwani wewe unaonaje?

    Votes: 2 25.0%

  • Total voters
    8

Denis Gregory

Member
Joined
Jan 10, 2020
Posts
97
Reaction score
120
Habari za muda huu waheshimiwa, Salam.
Kabla ya yote, nipende kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa maoni mtakayokwenda kuandika hapa, nami nitayachakata kwa uhalisia. Asante sana.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, nina kiasi cha Tsh Milioni 30,000,000 ambacho kiko tayari kwa ajili ya uwekezaji. Lengo langu ni kuanzisha biashara halali, yenye mzunguko mzuri na inayoweza kukua baada ya muda

Ili mnishauri vizuri na kwa uhalisia, ningependa kuweka mambo machache wazi
Eneo la Uwekezaji Nipo tayari kuwekeza katika maeneo yenye fursa iwe Dar es Salaam, Pwani, au mikoa mingine yenye mzunguko kulingana na fursa ya biashara yenyewe

Sekta ninazofikiria Niko wazi kupokea mawazo kwenye sekta mbalimbali kama vile biashara ya bidhaa za ujenzi/vifaa (Hardware), kilimo-biashara na ugavi (logistics/supply), au biashara yoyote ya jumla na rejareja yenye mzunguko wa haraka wa pesa

Uzoefu: Nina uzoefu wa kiasi fulani wa kusimamia miradi na biashara, lakini nahitaji maoni yenu kuhusu changamoto za sasa za soko (mwaka huu wa 2026) na wapi kuna mianya mizuri ya faida
Naomba mnisaidie kwenye maeneo haya
Ni wazo gani la biashara linalofaa zaidi kwa kiwango hiki cha mtaji kwa sasa
Changamoto gani kubwa ninazopaswa kuzichukulia tahadhari kwenye hiyo biashara
Mapendekezo ya maeneo (Location) ambayo biashara hiyo inaweza kuchangamka haraka
Mawazo yenu, tahadhari, na uzoefu wenu vitakuwa na mchango mkubwa sana kwangu.
Karibuni sana kwa miongozo na ushauri. Shukrani!
 
Kuna sehem Unguja ukiwekeza utapata hela. Ukiwa tayar na hilo DM
 
jitahidi uwekezaji wako ujikite zaidi kwenye Tumbo (chakula) kutoboa ni rahisi sana. Hapo swali ni HOW?
Ntarudi tena
 
Kwenye hiyo million 30 tumia million 10 tu

Tafuta wamiliki wa flemu za biashara, Ambazo zipo karibu na maeno yaliyoendelea tayari lakini hazina hadhi nzuri, Ingia mkataba nao, Rekebisha fremu kuwa za kisasa ili kuongeza thamani, Ongeza kodi inayoendana na thamani mpya, Kula maisha kaka
 
Back
Top Bottom