Nina 70,000 niifanyie nini

Nina 70,000 niifanyie nini

Habari

Nimefanikiwa kupata kihasi cha 70,000 nahitaji hii pesa initoe kwenye dimbwi la umasikini.

Niifanyie kitu gani ambacho kitakuza mtaji haraka sana.

Nipo Dsm.
Hakuna aliyeanzia pakubwa, hiyo 70, 000 japo ndogo, lakin unaweza kufanya jambo kubwa. Anza biashara ya kuku, tafuta kijiwe , anza hata na kuku watano (25, 000) wa Dar hawaachi kitu, kuanzia utumbo mpaka miguu ya kuku wewe uza.
 
Unaweza usiamini ila Pesa huenda ikawa sio nyenzo ya maana sana katika kufanikiwa....

Unaweza usiwe na hata senti, ila ukauza ulichonacho (skills / nguvu) n.k. na ukafanikiwa...., unaweza usiwe na mali ila ukapewa mali kwa mali kauli...., unaweza ukapewa bilioni mia moja ila ukafilisika baada ya muda mchache na ukabaki na nyongeza ya madeni, mawazo na stress za kutosha....

In short kwa sasa mzunguko wa pesa mdogo, kila mtu anatoa huduma zilezile, na kugombania wateja wachache walewale wasio na pesa... hii imepelekea maisha kuwa kama pata potea...., sikushauri uwe mchuuzi, angalia ulipo kuna uhitaji gani nina uhakika huo mtaji unaweza ukakutosha ili mkono uende kinywani tu na sio zaidi....
 
70k haikutoi kwenye umasikini.
Kama uko low kiasi hicho mkuu nashauri sana uinvest kwenye kupata more skills ambazo ni useful zitakazokusaidia kuingiza kipato. 70k huwezi wekeza kwenye biashara yoyote ile tusidanganyane.
Unataka invest 70k una hela ya kula na pa kulala?
 
Nenda alfajiri pale buguruni sokoni au Temeke streo na elfu 30,000 kanunua matunda ( matango) na vile vimfuko vya plastick na chumvi na kisu cha kumenyea halafu, halafu amza kuyatembeza sehemu yenye mikusanyika ya watu.stendi za daladala au kwenye foleni.

Au nenda kanunua yale maji na zile soda na juice take away pita kwenye foleni.kuna foleni hapa maeneo ya banana kuja airport au kinyerezi kuja majumbasita haina hiyo huduma.utapiga hela.Ukianza utapata pia biashara nyingine hukohuko
 
Ulifanya nini(biashara gani) mpaka ukaipata hio 70,000? Na ilichukuwa muda gani mpaka ukatengeneza hio hela. Weka harama za maisha yako ili upate ushauri utakao endana na hali halisi ya maisha yako.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Niliuza PC.
Wewe kama wewe wazo lako la mwanzo ilikuwa ufanye biashara gani?, unaishi kwenu au unajitegemea? Jee ni lazima hio biashara uifanyie dar au hata nje ya dar?


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Habari

Nimefanikiwa kupata kiasi cha 70,000 nahitaji hii pesa initoe kwenye dimbwi la umasikini.

Niifanyie kitu gani ambacho kitakuza mtaji haraka sana.

Nipo Dsm.
Nenda mbagala rangi tatu waambie unaanza kutembeza samaki. Hiyo pesa unapata samaki wa kutosha na hapo hapo buchani utakutana na watembezaji wengi. Watakufundisha jinsi ya kukata vipande na bbei zake. Chukua samaki tembeza na wakibaki unarudisha pale pale buchani wanakuhifadhia.
 
Nenda mbagala rangi tatu waambie unaanza kutembeza samaki. Hiyo pesa unapata samaki wa kutosha na hapo hapo buchani utakutana na watembezaji wengi. Watakufundisha jinsi ya kukata vipande na bbei zake. Chukua samaki tembeza na wakibaki unarudisha pale pale buchani wanakuhifadhia.
Biashara hii unakata mtaji tuvipande twenyewe tudogo wakibaki je halafu hauna fridge
 
Back
Top Bottom