Nimfanyeje huyu rafiki

Nimfanyeje huyu rafiki

Kumwambia C ni muhimu, japo yakupasa utumie akili. Waweza igiza, sema umewasikia watu wakimzungumzia B kuwa anammendea mkewe. Mengine utaongezea
Dah thanks hii ni best idea, natumia hii maana uhakikika ninao akikataa atajijuaaaa
 
mkuu mi naona hivi, ongea na mke wa C kama ataweza aweke ushahidi wa sms au chat au hata sauti jamaa akimtongoza halafu amuambie B ushahidi wa anachokitaka anao na akiendelea kumsumbua atamwambia mumewe ambae ni C. hapo jamaa atakuwa mpole na atarudi nyuma na hatamsumbua shemeji yako na urafiki utasalimika..... na akili zikimrudia B anaweza kuona alifanya kosa akamuomba msamaha shemeji yake maisha yakaendelea. maana huwezi jua sasa hivi anatumia kichwa gani kuwaza cha juu au chini.
 
Mara nyingi wanaowagegeda wake zetu ni watu wetu wa karibu. Inasikitisha sana
 
Kama uwezi mwambia c basi mwambie hyo B kua umesikia kila kitu alichokua anamwambia shemeji yako..usipo fanya ivyo siku na wewe ukioa jiandae kwa lolote.

Ila hapo ulipoacha kupokea simu ya B huo sio uwanaume kabisa yaan alietongozwa anune na wewe unune?

POKEA SIMU MCHANE BILA KUYUMBISHA MDOMO!!...alafu urafiki unaendelea kama kawaida!
 
Rafiki hii issue usipo i handle vyema utaharibu hiyo ndoa ambayo unafikiria unatakiwa kuiokoa. Huyo wife kaishaonyesha msimamo wa kumkataa huyo boya, inatosha. watu wengine huwa wanapanic kupita maelezo.Nakushauri uuchune. Kama ni mtu wa kuongea naye ni huyo mtongozaji. Mwambie ulimsikia na kwamba alichofanya siyo vyema
 
Back
Top Bottom