Nimezaa na mke wa mtu watoto wawili na ana mimba ya tatu

Status
Not open for further replies.

Hypersonic

JF-Expert Member
Apr 14, 2012
606
1,121
Wakuu asalaam Aleikum, Tumsifu Yesu Kristo, Bwana Yesu Asifiwe, nawasalamu kwa jina la Jamhuri ya Muungano.

Nije kwenye mada mimi ni mwanaume ambaye kidogo nimeshavuta vuta umri kiasi (niko around 40+) nina mke na watoto watatu. Lengo la kuja hapa naomba tupeane ushauri. Binafsi nimezunguka mikoa mbalimbali katika kutafuta riziki, mwaka 2012 nikiwa Dar na familia ikiwa mkoani nilikutana na dada mmoja bank flani hapohapo Dar.

Nikiwa kwenye foleni ya kuchukua visenti vyangu nyuma yangu kulikuwa na mwanadada ambaye ni kama age mate wangu tofauti yetu ni kama miaka miwili, yaani namzidi miaka 2.

Huyu dada alikuwa hana kalamu kwa ajili ya kujazia ile slip ya benki, hivyo akaniomba kalamu, nami bila hiana nikampatia huku nikiendelea kusogea counter ili nichukuwe visenti vyangu. Wakati namaliza kuchukuwa hela naye alikuwa amemaliza kujaza ile karatasi hivo akawa anasogea counter, yeye alikuwa ana depost hela.

Akanipatia kalamu yangu nikajivuta nje ya benki na hatimaye barabarani kusubiria daladala, nikiwa bado nasubiri daladala huyu dada akawa amekuja huku akiwa na ki IST chake akaniuliza unaelekea wapi nikamwambia Mwenge alafu Mbezi, akanIambia twende nikusogeze na hapo ndo mazungumzo yalianza.

Alinieleza mambo mengi kuhusu familia yake kuwa yeye ni yatima hamjui mama wala baba na alikuwa ameolewa mkoa fulani hivi lakini kutokana na tabia za mmewe waliamua kuachana, yeye kachukuwa watoto wake kuja Dar. Tangu siku hiyo tukaanza mazoea na hatimaye mahusiano. Kwa bahati mbaya yeye akataka sana ni muoe kitu ambacho mimi sikuweza kwa sababu tayari nilikuwa na mke.

Baada ya mahusiano ya takribani miaka mitatu huyu dada akapata mtu wa kumuoa na akanijulisha kuwa anaolewa kwa hiyo uhusiano wetu umefika mwisho , nikamwambia sawa na namba akabadilisha. Baada ya miezi sita akanipigia simu na namba mpya akaniomba samahani na kunIambia kama bado uko Dar naomba tuonane na kipindi hiki mimi pia nilikuwa nimeshaleta familia yangu Dar, nikamwambia sawa.

Tukakutana kwenye ile hoteli aliyofia yule mzee wa miaka 80 akiwa na binti. Akaniomba tena samahani na usema kuwa tangu ameolewa hajawahi kuinjoi penzi, kwani mume wake hata dakika hamalizi anakuwa ameshakojoa na hawezi kurudia tena, kinachofuata ni kuomba samahani tu. Nikamuuliza kwa hiyo nikusaidiaje? akasema 'kama kuna dawa unaijua naomba nimpelekee m'ume wangu', nikamwambia sina dawa na akanipa tena mzigo nikagonga na akawa amepata ujauzito siku hiyohiyo.

Tumeendelea na uhusiano mpaka sasa na nimeshamzalisha watoto wawili na ana mimba ya tatu anatarajia kujifungua mwezi wa nane.

Kwa sasa yeye na mume wake hawaishi Dar ila kwa kuwa ni mfanyabiashara mara nyingi anakuja Dar kuchukuwa mzigo na mbinu anayotumia akitaka kuja na akiwa na lengo la kubeba ujauzito anakuja akiwa anakaribia zile siku za hatari, hivyo tunafanya yetu alafu anarudi kwa mumewe.

Akifika kwa mume kwa kuwa mume anaifahamu kalenda yake mwanamke atajifanya ameingia period na kuvaa pedi kama kawaida na baadaye anamtegeshea jamaa anagonga alafu mwanamke anamwambia ameshika ujauzito.

Hii mbinu kwa upande wa mwanamke imefanya kazi vizuri lakini kwangu sasa naumia na natamani damu yangu, kwa lugha nyingine nahitaji hawa watoto wangu. Mke wangu hajui lakini yule mume mwenzangu pia hajui. Lakini ananijua tu kwa jina kwani mara nyingi amewahi kufuma sms zangu kwenye simu ya mkewe na kunipigia simu akiomba niachane na mke wake kwa kuwa anampenda sana mkewe.

Mwaka jana baada ya kuwa amekaa muda tangu kujifungua mtoto wa pili nikamtania hutaki tena kuzaa akasema nataka lakini naona kama wameisha make jamaa miaka yote nimemwachia jamaa lakini sishiki mimba, nikamwambia njoo tujaribu hii ilikuwa ni mwezi akaja na matokeo kashika mimba ya tatu tena. Kiuchumi yuko vizuri tu ana biashara zake, na mume ni mfanyakazi Serikalini.

Hebu tushauriane nini nifanye make natamani hawa watoto wangu ukizingatia mke wangu hazai tena na watoto wetu ni wakubwa wa mwisho amemaliza six anaenda JKT, wawili wako chuo. Na huyu jamaa akijua kinachofuata ni yale ya SAIDI. Mwanamke ananisihi sana nisaidae hawa watoto ila ikitokea mume wake amekufa kabla yangu atawaambia watoto ukweli tofauti na hapo hawezi na ananiomba sana nisithubutu.
 
Dhambi Hiyo itakutesa sana, katubu na ukate mawasiliano na kimada Huyo,anza upya kuhusu watoto si halali kwako hata kama ni damu yako,acha iwe siri yenu mpaka mnakufa ili kwepusha taharuki kwa familia baadaye ni ushauri tu ukitaka kuwa salama na uhuru wa moyo fanya hivyo utanishukuru uzeeni mwako.
 
ukiwa Bado unasubiri Dala dala yeye akaja na ki IST chake...Miaka 40 Unasema Ki IST...Unazeeka na Upumbavu Wako.
kwa akili yako kusubiri daladala ni upumbavu, kuna watu wanapanda daladala na wana hela ya kutosha, kuna watu wanamiliki daladala na wanapanda daladala, kupanga ni kuchagua. Pia hakuna mwanaume awe kijana au mtu mzima ambaye hana mpango wa kando, hata mamako anagongwa na mtu ambaye sibabako, au unalelewa na mtu ambaye si babako. Heshimu wanaume we mvulana
 
Dhambi Hiyo itakutesa sana,katubu na ukate mawasiliano na kimada Huyo,anza upya kuhusu watoto si halali kwako hata kama ni damu yako,acha iwe siri yenu mpaka mnakufa ili kwepusha taharuki kwa familia baadaye ni ushauri tu ukitaka kuwa salama na uhuru wa moyo fanya hivyo utanishukuru uzeeni mwako.
Msamaha unakubalika kwa kumuomba uliyemkosea, natamani kufanya hivo lkn namfikiaje kusiwe na madhara, ukiona mtu anaweka jambo public tambua limeshamsumbua kwa saana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom