Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Well, ulianza vzr kama vile mtu aliyejutia ile kazi, yale maisha na consequence zake, na nikachukulia sasa umeamua kurudi kwa Mungu ki ukweli hivyo Yesu Kristo achukue adhabu yako(mshahara wa dhambi=mauti),misiba yako,aibu yako na kukubali kununuliwa kutoka jela ya shetani(kwako uchangu) kwa kulipiwa kwa Damu ya Thamani ya Yesu Kristo Mkombozi wetu. Hapo nilikupenda na nilitaka kukuombea upate msaada wa kimungu huyo uliyemkimbilia! Sasa unasema,eti ukimwambia akikumwaga, huyo aliyekushauri akutafutie mdhambi mwingine, mmmh, bado hujapona! Ushauri, jiachilie kwa Mungu wako wholy, jinyenyekeze kwake,mtumikie na kumtegemea yeye tu mbona Mungu huyu nimtumikiaye Anaweza? Yesu anasema alikuja kwa wenye dhambi ili wapate kutubu. Ukitubu kisawasawa mpaka ukawekwa huru, utaona unakuwa na ujasiri wa kutamka ulikopitia, tena sio kwa huyo mchumba tu, (ambaye kuna kazi ya kufanya ili awe wako) bali utapata ujasiri wa kupanda madhabauni na kutoa hiyo stori kama 'ushuhuda'! Kuanzia hapo, hata hao machangu wa Kenya kama bado wapo kwenye hiyo fani watakuogopa, lkn kama wameacha au wanataka kuacha, basi watakuona wewe ni shujaa, nawe utakuwa kioo kwao. Huyo njemba kama ni wako atakupenda zaidi, akiishia ujue yupo aliye wako anakuja! Lkn haya yote inategemea na kanisa unalosali, je wanaelewa maana ya 'Deliverance of the Soul'! Kama hamna, huko kwenye wazo mbadala mie siko! Mkubali Yesu na Mtumikie Mungu wa Moyo wako wote. Barikiwa mama.
 
Khaaa weee nawe kwani kabila gani?
Si unakataa

mmh!nna roho mbaya na ngumu sana ila huyu mwanaume nampenda na niko dhaifu sana kwake sina ukakamavu hata wa kumkatalia ikiwa ataniuliza....the problem ni mapenzi nliyonayo juu yake yananifanya always niwe honest
 
kwan mim nmekukataa?? teh teh anyways yote hayo yanatokana na uelewa wa huyo mumeo mtarajiwa na pia atlist utakuwa umetua mzigo mzito na utajua hilo ni gubu la kawaida tu mama coz ukwel unajua hukufanya kwa nia mbaya na nafs yako iko huru!
nataman nikukutanishe naye umshauri pindi ntakapomwambia ukweli
 
Duh!pole sana japo kuna mambo mengine niyakuyanyamazia tu rohoni ili siku ziende maana huo uchangudoa ulioufanya hata ukimwambia sioni kama utasaidia chochote katika maisha yako ya sasa hivi
asante sana
niliapa kuiweka siri milele ila tatizo naogopa kuna wadada wa KIKENYA wamehamiaga ARUSHA na nliwahi kujiuza nao NAIROBI wanaweza mbeleni kuja vujisha siri
 
Pole sana, ila hizi details ulizoweka humu mhhhhhh! Kama hayumo humu ni ahueni kwako au mtu mliyekuwa mnasali pamoja ambaye anaweza kujumlisha hizi details na kupata jawabu wewe ni nani. Pole sana tubu kwa mola wako kisha umuombe akusaidie. Ukiamua kufunguka hujui mwenzio ataumia vipi na maamuzi yake anaweza kabisa kukupiga chini. Pole sana.

unajua wadogo zangu hawajui kama nlijiuza wanafurahia maisha na kama wapo huku jukwaan ni vizuri wajue dada yao nlikopitia.
hawa wadogo nlikuwa nkigombana nao sana wakidhania nina akaunti za mama na natumia hela nyingi kivyangu na sasa ni wakati wa kujua ukweli
nimeteseka sana kwa kuficha ukweli.........i am tire of this na naishi kwa kuwaogopa watu (wale wadada wa nairobi waliopo tanzania) imagine ni maisha gani haya??????
 
  • Thanks
Reactions: BAK
....... kuna tofauti ya ndugu zako kujua ulikopitia na mume mtarajiwa. Ndugu hawawezi kukupiga chini na undugu haufi mtaendelea kuwa ndugu hata kama wataumia, lakini kwenye penzi linaloelekea kufunga pingu za maisha hali ni tofauti. Wanaume wachache sana wanaweza kukubali kuendelea na mipango ya ndoa wakijua mke mtarajiwa aliwahi kuuza mwili wake. Akili mkichwa Mkuu.

unajua wadogo zangu hawajui kama nlijiuza wanafurahia maisha na kama wapo huku jukwaan ni vizuri wajue dada yao nlikopitia.
hawa wadogo nlikuwa nkigombana nao sana wakidhania nina akaunti za mama na natumia hela nyingi kivyangu na sasa ni wakati wa kujua ukweli
nimeteseka sana kwa kuficha ukweli.........i am tire of this na naishi kwa kuwaogopa watu (wale wadada wa nairobi waliopo tanzania) imagine ni maisha gani haya??????
 
Hayo yalishapita mdada, unapoamua kuishi maisha chanya yae yote ya nyuma huwa tunayasahau na kuangalia ya mbele unless kama ungekuwa bado upo kwenye fani kidogo hata mie ningepata cha kukushauri,kila mtu ana mambo mabaya ambayo alishayafanya nyuma tofauti tu la kwako linaonekana kubwa kwa kuwa linaonekana lipo against na watu wengi na ndio maana unaona kama dhamira inakusuta lakini mbele za mungu aliekuwa changudoa, mzinzi kama ilivyo mie naweza nikawa na mke na bado natoka na wanawake wengine wote tunahesabika ni wale wale tofauti wewe ulikuwa unauza na mie nilikuwa natongoza alafu wananikubali kwa hiari yao wenyewe lakini mwisho wa siku wote tunaangukia kundi moja. Sasa iweje wewe ujione mkosaji sasa kiasi kwamba kutaka kumwambia mwanadamu mwenzako mambo ya nyuma ambayo umeachana nayo tayari

Kama ingekuwa ameambiwa na watu alafu anakuuliza wewe unasita kumwambia hapo hata mie ningekushauri umwambie lakini kwa sasa amekufuata wewe kwa kujua tabia zako njema baada ya kumrudia Mungu hivyo basi yale ya nyuma yote sahau na yatumie kama funzo katika maisha yako mapya ili yasiweze kujirudia tena si kwako wala kwa familia yako au hata sie wengine tunaokuzunguuka

Kila watu wanapotaka kuoana wangekuwa wanaambiana makosa yao ya nyuma au historia zao za nyuma, watu wanaohusika na mambo ya stationery wangebuni na kadi za kuhairisha harusi na kusogeza mbele kwa jinsi wengi wanekuwa wanaji-withdraw, hapa tu mtu amekukubali na mlikutana kila mtu alikuwa na mahusiano nyuma ukizungumzia issue kidogo tu ya mpenzi wako wa nyuma ananuna je hili la kwako
 
Back
Top Bottom