Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Nimewahi kuwa changudoa, nimjulishe?

Siijui ndio ya rangi gani?
Nakubali ukweli sawaaa lakin ukweli mwingine hubomoa pia inategemea na akili ya mumee,kama mume akili yake mbayuwayu wataambiwa hadi mawifi hadi marafiki,labda kama huyo mwanaume ni malaikaa mi napinga hilo hakuna cha stara wala stata

Tunarudi kuleee kwamba mume n mpango wa Mungu ndugu yangu so akiwa huyo ndo kapangiwa Awe mmewe asipokua huyo sio rizik ake Ila afaham mficha maradhi kifo humuumbua
 
tatizo baadhi ya wadada wa KENYA nliojiuza nao wamekuja kutafuta maisha ARUSHA na mbaya zaidi hawana kazi za uhakika so muda wowote maisha yakiwawia magumu wanaweza anza kujiuza na kunitaja kama mshirika wao nairobi
Mi nakushauri kuwa rudi kwenye kanisa lako la zamani kawaface hao wadada Wakenya waambie ukweli kuwa hayo mambo uliyoyafanya yalikuwa ni ya kupita tu kwa sababu ulikuwa na hali ngumu, lakini kwa sasa umeokoka na umeacha hayo mambo na Ya kale yamepita kwani wewe ni kiumbe kipya sasa.
 
baada ya matatizo yote ya utotoni kwa sasa nimekuwa mpole sana
nilikuwa kiongozi wa vijana kanisani ila nlilazimika kuhama baada ya MKENYA MDADA flani kuanza kuhudhuria huduma ya hapa kanisani.
BF alinishangaa kwani nahama kanisa ninaloheshimika kwa namna nlivyowaongoza vijana na mchungaji aliingilia akinitaka nisihame....mwishowe nikahama kilazima mkaanza kusali kikanisa kidogo njee ya mji....nayaona maisha yangu yoote yamejaa uongo nateseka sana
my dea kwanza pole hayo ni maisha ,pili tambua ushasamehewa na moyo wako mungu ameona ,mwisho nikutie moyo kuwa ,kuna wanawake wengi tu wamekuwa na mahusiano zaidi ya wanaume 10 na wote hao wamefanya nao ngono ila kutokana na matatizo ambayo tunakutana nayo unajikuta unaacha na unaanzisha na mwingine,huyo hana tofauti na ww,sema tu ww ulikuwa unauza kwa pesa tena kwa masaa ulikuwa hudumu na mtu lkn mwisho wa siku tumeolewa,sasa usiogope,mradi umepima huna ukimwi,basi uko salama,na kuhusu mchumba wako ww ndie unamjua je ukimwambia ukweli atareact kiasi gani,bora usimwambie,tambua na hao pia wadada wa kenya nao wapo hapo kanisani kutubu zambi zao hivyo basi lbd kama yupo hapo kukufatilia ww na si mungu,lkn waweza wafata na kuongea nao kuwa pamoja na ukahaba niliofanya lkn mungu kaniokoa na mume nmepata soon naolewa na nishatubu,na uzuri mchumba wangu anajua hivyo kanipenda na tumepima,mwisho wakkaribishe ktk sherehe,uone kama watasema neno lolote kwa mtu
 
niko mdhaifu sana mbele yake najihisi siwezi kabisa kukataa ikiwa ataelezwa
ukimpenda mtu unageuka mtumwa na zezeta na nampenda sana jamaa

Fikiria zaidi theni jiongeza kidogo bidada, ukiendekeza huo moyo wako utamkosa huyo jamaa yako, watamfaidi wengine shauri yako, tumeona mengi ndo maana tunakushauri umezee!!
 
kama unampenda basi usimuumize na historia yako ya maisha.... ingekuwa vyema kama ungefanikiwa kumuuleza mwanzoni kabisa yeye achagu e anakuwa na mtu wa namna gani.. we mambo yameiva unajifanya kusema bibi wewe utajitafutia safar..... usitengeneze fimbo ya kukuchapia hawa viumbe waone tu wanakojoa wamesimama ni hatari sana ... matatizo yako watayageuza yawe rungu ila kama unajua ana mdomo wa kukusitir mweleze kheeeee nani atakubali kuoa changudoa atajuaaje umeacha? akiona dalili za kuchitiwa bibi utaambiwa umeanza uchangudoa tena... my word usimweleze

Kwani huyo mwanaume ni bikra utakuta alikua zaidi yakee !!umemalizaaa
 
Remember! You only answer to God, yeye ndiye mlishi wetu. Kama umeomba msamaha kwa Mungu utakuwa huru na utakuwa huru tu, hata akija kujua. Kwahiyo carry on.....
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Why not? kwani huyo jamaa yeye msafi kiasi gani? Kama alishalala na mwanamke zaidi ya mmoja na huyo mmoja sio wewe hamna tofauti hapo... but ndio maana nimesema bury the past and move on, ila kama unataka kua honest just tell him kama anakupenda kwa dhati hatakua shida kwake, kama penzi maghumashi atakuacha but that should not dissapoint you!

Asipofuata huu ushauri basiii
 
my dea kwanza pole hayo ni maisha ,pili tambua ushasamehewa na moyo wako mungu ameona ,mwisho nikutie moyo kuwa ,kuna wanawake wengi tu wamekuwa na mahusiano zaidi ya wanaume 10 na wote hao wamefanya nao ngono ila kutokana na matatizo ambayo tunakutana nayo unajikuta unaacha na unaanzisha na mwingine,huyo hana tofauti na ww,sema tu ww ulikuwa unauza kwa pesa tena kwa masaa ulikuwa hudumu na mtu lkn mwisho wa siku tumeolewa,sasa usiogope,mradi umepima huna ukimwi,basi uko salama,na kuhusu mchumba wako ww ndie unamjua je ukimwambia ukweli atareact kiasi gani,bora usimwambie,tambua na hao pia wadada wa kenya nao wapo hapo kanisani kutubu zambi zao hivyo basi lbd kama yupo hapo kukufatilia ww na si mungu,lkn waweza wafata na kuongea nao kuwa pamoja na ukahaba niliofanya lkn mungu kaniokoa na mume nmepata soon naolewa na nishatubu,na uzuri mchumba wangu anajua hivyo kanipenda na tumepima,mwisho wakkaribishe ktk sherehe,uone kama watasema neno lolote kwa mtu

Umemalizaaaaaaaaaaaaa
 
Akaniambia nsiwe narudi rudi kukaa muda mrefu pale nyumbani mpaka atakapoachiwa mama nlikuwa form three-Nairobi,Nilijiuza mpaka nikasoma chuo na wadogo wakaingia sekondari thank god mama aliachiwa baada ya mitatu miaka
Kahadithi km ka Shigongo vile
usome Form III mpaka umalize Chuo ndani ya miaka 3 Mama akaachiwa (Elimu Kenya ni kiboko)
ujiuze usomeshe na kulisha wadogo zako kila siku miaka 3 na kuwasomesha wote boarding (du Kenya biashara hii inalipa)
hakuna haja ya biashara ingine
Bora huyo Mmasaai asieleweshwe
 
Kahadithi km ka Shigongo vile
usome Form III mpaka umalize Chuo ndani ya miaka 3 Mama akaachiwa (Elimu Kenya ni kiboko)
ujiuze usomeshe na kulisha wadogo zako kila siku miaka 3 na kuwasomesha wote boarding (du Kenya biashara hii inalipa)
hakuna haja ya biashara ingine
Bora huyo Mmasaai asieleweshwe

Hhhhaaa maaan inaonyesha alikua analipwa vizuri mnoo hapo atuelewesheeee ndio maana nasema mengine anyamaze maana akisema maswali yatazidi
 
what if i keep it down as posibo ila akajajua baadae kupitia kwa wadada wakenya ambao wako hapa AR?

hao wadada wakenya kaa nao chini waambie wewe umeamua kuzaliwa upya umemfuaa Yesu, na Mungu akipenda utaolewa soon, so waambie yale tuliokuwa tunafanya enzi hizo please wasiyalete kwa mumeo mtarajiwa

Mbona watakuelewa tu!! wangapi tunajua maovu yao hatujathubutu kusema kwa ajili ya kulinda mahusiano ya watu
 
inavoonekana hukubadilika ndio maana iyo dhambi inakuwazisha... kama umebadilika usiwaze hayo mwambie Mungu na ukitumia akili zako umeumia.
 
Ni ngumu kumeza kusikia mke mtarajiwa aliwahi kuwa CD, na si kwa wanaume tu. Weye utakubali kuwa na wifi aliyewa kuwa CD!?

Ndio na sie tunamuambiaa,kwanza akimuambia tu siku wakikosana ndio utakua neno hilo la kuumizwaaaa,chezeaaa mawifi wakijua kaka yao kaoa changu heeeeeeeee unaziju midomo za mawifi,labda amuambiee wakishaoana na kuzaa mtoto
 
  • Thanks
Reactions: BAK
my dear kua muazi kwake kama ulipangiwa awe ndo mumeo atakua bila mashaka hakuna kitu kizuri kama kua mkweli wa nafsi kamwe haikusuti kua makini usijejuta baadae

Akifuata huu ushauri wako ajue mume anamkosa kufumba na kufumbua, wanaume tunajijua!!
 
mwambie ili utuletee mrejesho tujue kama kwenye mapenzi ukweli unalipa make kwenye uongo tunajua faida yake.
 
geniveros umeona ee tumemuambia apige kimya pia akae mbali ana hao marafiki zakeee ,kama anaitaka hiyo ndoaa

ndo hvyo hvyo maana hao wapo na wataendelea kuwepo
ye afanyr yake tu
kimya kimya uchangudoa kitu gani bwana wee
 
Last edited by a moderator:
Kama hiyo story yako ya kweli hauhitaji hata kumwambia uyo bwana ndio maana kwenye sala ya toba huwaga hatutaji aina za dhambi ambazo tulikuwa tunafanya cha msingi rudi kanisani wala ucjushtukie, tatizo lako wemwenyewe hujajisamehe.sio ajabu hao wakenya wanakuogopa wewe usije ukasema background yao.kuwa huru kipindi ulikuwa unafanya hayo haukuwa na nuru na mazingira yalikulazmisha anza kwanza kujisamehe wewe sio kila kitu cha kumwambia mwezanko mengine badala ya kumjenga utambomoa bure unless kama unatatizo la uzazi hayo ndio mambo ya kushare mapema
 
Back
Top Bottom