Haya. Ila pole sana momy,wanaume wote hatuko kama huyo na kuna uwezekano huyo wako ulimuudhi au kuna kitu alikuwa hakwambii na alikivumilia kwa muda mrefu mpaka alipoona hawezi tena na kubwaga manyanga. Mtu aliekwambia amefurahi umepata ujauzito,hawezi kukukimbia hivihivi tu,lazima kuna kitu.
Kuna vitu wanawake huwa hamchukulii kama ni matatizo ya kukera ila yanafukuza sana wapenzi na mengine ni simple sana mf:Kuongea sana bila kuacha na ukitaka usikilizwe wewe tu na maoni yako ndio ya kufuatwa na ya mwenza wako si ya kusikilizwa wala kufanyiwa kazi.
Kingine ni kununa bila sababu. Unaamka tu ukiwa umekunja ndita bila sababu yoyote ya msingi na hutaki kusema chanzo ni nini. Hilo humfanya ulienae kuishi akiwa roho juu na asijue la kufanya. Wenye akili nyingi kama mimi,tutakuacha na kujiendea baa kutuliza akili,lakini wasiokunywa watakaa na hizo stress mpaka akili yako irudi sawa. Sasa imagine atavumilia stress mara ngapi ikiwa ndio tabia yako?
Kingine ni ulalamishi na manung'uniko. Wengi hapa watanielewa. Unakuta mtu kutwa kucha ni kulalamikia mambo madogo mpaka makubwa,hana kauli yenye matumaini, hataki kushiriki katika kutatua anayoyalalamikia,kazi yake ni kulalamika tu na kuwa mtazamaji wakati mwenzi asietiwa moyo akihangaika kutatua matatizo hayo. Mtu atakuchoka haraka sana ukiwa na attitude kama hiyo.
Kukosoakosoa majambo. Mtu kakununulia viatu,wewe unaanza kuvitoa kasoro na kulinganisha na vya mke wa jirani alienunuliwa mtumbani juzi. Mtu kanunua friji mpya na seti za vyombo,wewe unampigia kelele kuwa havina ubora na hujavipenda. Unadhani siku nyingine atanunua kitu kipya na kuleta kwako ili iweje? Au kama akimpelekea mtu mwingine hereni za elfu sita na bangili za elfu tano akashukuriwa kama kitu gani,ataacha kumpelekea kitu kikubwa zaidi huyo anaeshukuru zaidi? Atahamia kabisa afannye nae maisha na sio kukaa na mtu anaekatisha tamaa.
Vingine ni kiburi,ujuaji usio na msingi na mengine mengi. Hulazimishwi kubadilika,ila kama nia yako ni kuishi na mwanaume unaempenda na yeye akikupenda,basi badilika ili uvumilike,mvumiliane.