Nimewachukia sana wanaume mnisamehe

Nimewachukia sana wanaume mnisamehe

Ukishazaa utamtaka tu tena Abdallah kipara, na utakuwa unamtolea miguno ya utamu kibaooo!
 
Kwa kautaalamu kangu ka saikolojia ya std 7, hio ni hali tu ya ujauzito wengi huwa inawapata isije kuwa hata hamna kitu ni hallucinations tu!! By the way jaribu kukutana na ma dr wa saikolojia.
 
Pole Sana.
Weka focus yako kwenye kulea mimba na kumlea mwanao. Fikiria Kama huyo mwanaume angefariki, ilhali anakupenda bado; ungeumia maradufu. Maadam hajakuchagua wewe kuwa wake wa maisha, Shukuru Mungu na usonge mbele. Mlango mmoja ukifungwa achana nao, kuna milango tisa I wazi mbele yako.
 
Hii huwa mnajitakia wenyewe. Sijui kwa nini hamsikii, mtaendelea kupigwa mimba na kutoswa na kuishia kulalamika humu
 
Wanaume nimewagopa sana sina hamu na nyie. Nilikuwa na mchumba nikapata mimba akawa amefurahi sana basi tukakubaliana tukwaweka mikakati yetu. Tulikuwa tunaishi mkoa moja mm nikapata kazi mkoa mwingine ikabidi tuwe mbali ila tukawa tunaonana mara chache hadi nilipata hii mimba. Tuliwasiliana kwa cm hadi mimba ikiwa na wiki 6 mwenzangu akakata mawasiliano hadi leo ina miezi nane. Nimehangaika kuwasilianà na watu waje wa karibu wananiambia hata wakiongea nae hakuna anachiwaambia akiwemo hadi boss wake maana aliyajua mahusiano yetu vzr tuu akaniambia labda anaogopa majukumu. Nimshukuru tuu Mungu kwani tangu mimba hii sijawahi ugua hata mafua naendelea vrz ba maisha yangu nalea peke yangu. Ila napata shida moja ya kisaikolojia nimewachukia wanaume natamani nizae mtoto wa kike nineenda kucheck utrasound kwa lengo la kuangalia jinsia ikabidi nighairi thou nikuwa nimeshalipia maana nawaza nikiambiwa ni wa kiume nitakuwa dissapointed. Nimehamua tuu hata nikizaa mtoto nimpe jina la ukoo wetu maana baba yake haangaiki na chochote kwanza ndio kaniblock sehemu zote za mawasiliano. Kama yupo mwanasaikolojia naomba anishauri tuu maana niko desparate nimechukia mnoooo!!!!!

Umekutana tu na wrong idiot, wanaume wengi hawako hivyo! Huyo wako Ni kichaa. Usichukie wanaume bila sababu na uje kumlea mtoto wako wa kiume vyema, tena vyema ili asijependezwa kurithi ya babake!

Mungu akujaalie Mdogo Wangu ujirungue salama.
 
Pole sana muombe mungu ujifungue salama , achana naye huyo mwanaume malipo ni duniani
 
Ukijifungua utawapenda wanaume tena mpaka utajishangaa
 
Ivi dada mwenye zaidi ya miaka kumi na nane anapewaje mimba ambayo hamjapanga huku ukiwa na elimu kabisa ya kujua mimba inaingiaje shida ni moja si kila unamwambia njoo malizaa babaa kaamua kuwa baba wengine wanataka starehee ni jambo la kukaa na kupanga pamoja
Ungechukia wanaume na ukaacha kuvua chup ovyo leo ungetuletea somo la ujasiriamali hapa tuelimike by the way jichukie ww kwa kutosikia neno la Mungu kutokutii wazazi kutosikia waalimu pamoja na serekali sbb hata Mweshimiwa alishasema mimba ni kiherehere chenu mabinti
Acha kumlaumu mtu ambaye hukuingia nae mkataba wa kupata watoto mkataba huo ni ndoa na cheti hutolewa angelelewa hata na familia zote mbili sbb wangekuwa ni mashaidi ndefu lkn soma
JICHUKIE WW KWA KIHEREHERE CHAKO
 
Kuachwa ukiwa na mimba sio tatizo tatizo kuachwa na magonjwa
 
Unajitia unajisi kwa uasherati halafu unasema unamshukuru Mungu hujaumwa hata mafua! Acha uisome namba, mlango ulioingilia ndio utakaotokea, kila anavuna alichopanda.

Hatunywi sumu wala hatujinyongi, tumejipanga mwaka huu, mtaisoma namba, wanaume mbele kwa mbele.
 
ninaomba niwe baba mlezi wa mtoto , nipo tayari hizo HASIRA za muda tu ,ila mtoto akisha zaliwa utasikia munaanza kuchepuka tena. .
 
Wanaume nimewagopa sana sina hamu na nyie. Nilikuwa na mchumba nikapata mimba akawa amefurahi sana basi tukakubaliana tukwaweka mikakati yetu. Tulikuwa tunaishi mkoa moja mm nikapata kazi mkoa mwingine ikabidi tuwe mbali ila tukawa tunaonana mara chache hadi nilipata hii mimba. Tuliwasiliana kwa cm hadi mimba ikiwa na wiki 6 mwenzangu akakata mawasiliano hadi leo ina miezi nane. Nimehangaika kuwasilianà na watu waje wa karibu wananiambia hata wakiongea nae hakuna anachiwaambia akiwemo hadi boss wake maana aliyajua mahusiano yetu vzr tuu akaniambia labda anaogopa majukumu. Nimshukuru tuu Mungu kwani tangu mimba hii sijawahi ugua hata mafua naendelea vrz ba maisha yangu nalea peke yangu. Ila napata shida moja ya kisaikolojia nimewachukia wanaume natamani nizae mtoto wa kike nineenda kucheck utrasound kwa lengo la kuangalia jinsia ikabidi nighairi thou nikuwa nimeshalipia maana nawaza nikiambiwa ni wa kiume nitakuwa dissapointed. Nimehamua tuu hata nikizaa mtoto nimpe jina la ukoo wetu maana baba yake haangaiki na chochote kwanza ndio kaniblock sehemu zote za mawasiliano. Kama yupo mwanasaikolojia naomba anishauri tuu maana niko desparate nimechukia mnoooo!!!!!
Kosa lako ni moja! Generalisation! Wewe hapo ni zao la shahawa sijui ni za mwanamke?

Watu wanatofautiana na pia siyo rahisi katika ulimwengu wa leo kufanya judgement kwa kusikiliza upande mmoja wa story maana siku hizi mimba moja inahudumiwa na watu 10 sasa mpk tujiridhishe na ukiona hivyo kuna sababu.

Huhitaji mwana saikolojia hiyo ni sehemu ya maisha japo nahisi hujitambui kama unafikia hatua ya kusema ukigundua mtoto ni wa kiume utakuwa disappointed! Wakupime akili wewe siyo bure
 
Back
Top Bottom