Nimevunja uchumba wa watu

Nimevunja uchumba wa watu

Wewe huna akili, ila huyo binti hana akili zaidi...

Alafu inaonekana nyie wanaume wote wawili mnaenda kushinda kwa binti badala ya binti aje kushinda makwenu... aibu...


Cc: mahondaw
 
Aaha kama utamuoa wewe sawa.. Ila sasa una uhakika demu anakupenda kweli na yupo tayari umuoe??? Maana mkuu usije kumuoa sababu tu kaachwa na jamaa ake maana jama akirudisha majeshi aisee utakuja unalia hapaa...Atamlaaa anavyotakaa
Aiseee
 
Mwana kulitafta mwana kulipata binti amesha lipata nawew ni zamu yako nenda wakakuokote nyayo za miguu wakuroge unaharibu maisha ya mtoto wa mtu af unaongea kwa uhuru ebu fikiria ingekua uyo ni dadako si aibu ya mtaa iyo.
 
Inavyoonekana huyo mwanamke alipewa onyo juu yako na alipokushirikisha haukutilia maanani, maana inaonekana anakujuwa vizuri na ukute ulipofika majirani walimpa taarifa hivyo alikuja akiwa tayari ana maamuzi, yaani ndugu zake kumtuliza inakuwa ngumu.

Kibaya utakuta umeoa na haukuwa na nia ya kumuoa, kama unamuona ni mwanamke anayekufaa haupaswi urudi nyuma kama ambavyo ulifanya alipokupa onyo juu ya kuwa na mahusiano lakini haukupunguza mapenzi kwake.

Mapenzi yale yale uliyokuwa nayo ndiyo unapaswa uyaoneshe kwake...

Kwa ushauri wangu kubali kwenda ila usiende leo subiri kidogo papoe, naamini kwasasa labda ndugu wakawa na jazba zaidi.

Utakuta jamaa alikuwa anamtafutia sababu namna ya kumuacha sababu ameipata tena amekukabidhi wewe, lawama hapati tena na mahari akipewa anaanzisha biashara.
Baharia sio watu wazuri aisee
 
Kila muosha huoshwa...subiri nawe yatakukuta.Umefanya tabia mbaya sana kwa kukusudia mfyuu
 
Itakugharimu wewe na uzao wako, asilimia 99 ya matatizo yanayowakumba wanadamu na uzao wake ni ya kujitakia.
Karma itamtafuna yeye Pamoja na kizazi chake.
Pia huyo mwanamke hata angeolewa asingekuwa mke mwema kwa jamaa na ndo Maana MUNGU kaamua kumuonyesha muoaji mapema..
 
Kuwa makini na hawa watu wanaoitwa mama zetu inapokuja suala la mapenzi, Ikiwezekana chunguza vizuri historia ya mapenzi yake ya nyuma haswa huyo aiyejitosa kulipa mahari, isije ikawa na yeye alivunja mahusiano serious ya mtu kumpata. Usiruhusu pride ikakufanya ukajiona kuwa wewe ni mwanaume zaidi ya wote waliowahi kuwa na mwanamke wako kabla yako. Nakwambia hivi kwa sababu kma mwanamke alifika hatua ya kukubali kulipiwa mahari na sababu kuu ya kukubali kuvunja mahusiano ni wewe na si nyingine nzito, basi huyo ni mwanamke dhaifu na usibweteke hata ukioa maana kama a=b na b=c basi a=c, uwezekano wa kupata sababu ya kukusaliti huko mbeleni upo kama alivyopata sababu ya kumsaliti huyu wa sasa ambaye alimwaminisha anampenda hadi jamaa kutoa mahari. Ila lisilojulikana ni usiku wa giza, naamini yapo mengi tusiyoyajua yanayokufanya na wewe uchukue risk hiyo. kila la heri.

NB: Kama kuna uwezekano wa kumake peace na x-fiance, fanya hivyo. Huwezi jua analoliwaza moyoni mwake. Na kama mtafunga ndoa pia huwezi jua atawaza nini juu ya hatua yenu.
Yeahhh!
 
sijawah kuona jamaa mpuuz kama wewe, ukienda kubakwa huko ? Umeharibu mipango ya watu alafu unataka kwenda kuongea nao? wakikudhuru ? we huna makosa mwenye makosa ni binti, You guys mbona mpo soft ivyo sikuiz ? mkitekwa mtasemaje ??
Hahahahaa! Anajipeleka machinjioni.
 
Huwenda ukajiweka pabaya zaidi hasa pale binti asipoolewa na kubaki nyumbani kisha wewe ukaoa sehemu nyingine na wakuone ukiwa na furaha na familia yako huku binti yao yupo nyumbani, kumbuka hayupo mzazi aliye tayari binti yake kuzeeka akiwa nyumbani hiyo inaonesha alishindwa kumlea katika maadili mema.

Huku kila mmoja anasema lake ila haitokuwa sababu ya wewe kushindwa kufata maamuzi yako, unayo bado nafasi kwake na kwako wewe jiandae kwa lolote maana inategemea busara za huyo jamaa ila kama ni mtu wa visasi hata ukija kumuoa mwingine atafanya aliwezalo akulize nawewe.
Mimi wapo familia yangu walininyima nisiolewe 19 kisa mdogo ikaja 22 hiyo siyo dini yako sasa ninashanga na wanataka nitoke home nimezeeka so familia zipo ambazo wanakukatalia usiolewe ukiwa mdogo uolewe ukiwa mzee sasa sijui nani atakuoa mzee hivyo.
 
Mapenzi upofu ,hawezi kuona kama anakosea. Niliwahi kuwa na mpenzi yuko form 3 na ni mtoto wa mkuu wa polisi wilaya . just imagine hiyo risk hapo.
umeona ? unajua jamaa alikuwa anawasupport vipi wazazi wa dem ? kuna mambo meng ya kucobsider kabla hujajupeleka kwenye mdomo wa mamba
 
Back
Top Bottom