Nimevunja uchumba wa watu

Nimevunja uchumba wa watu

Kweli nimeona nisiende
Wewe huna kosa mwanamke angekuwa anampenda jamaake asingekukubali kirahis hivyo, sasa huko ukienda kukutana na kosi lakukidhuru utafanyaje ? unaenda mwenyewe ? Alafu kitu kingine mnaenda kudiscuss nini ? mnaenda kuongelea namna wewe ulivyokuwa unamwibia jamaa mchumba ake mpaka akakukuta kwake ? Haya tuseme umefika wakakuomba umwachie jamaa mwanamke wake utafanyaje ? wewe vaa viatu vya jamaa na jamaa awe wewe, UNGEENDA ?
 
Usiende kwao,tulia kwanza huu upepo upite....baada ya hapo we ndio utafanya uamuzi baada ya kuona matokeo
 
We nenda, kaombe msamaha, wala usimlaumu huyo mwanamke, beba dhambi, okoa ndoa ya watu,ni aibu sana kwa wazazi kudaiwa mahari kwa sababu ya aibu ya binti yao.....

Malalamiko ya hao wazazi ndugu yangu yatakupa shida sana sana, hakikisha wanarudiana aisee.... sioni ubaya ya huyo mwanamke, wengi wanakosea na anaweza kuwa mtu mzuri tu sana.....
Duh asee unasema aende tu ? labda Kama hao wazazi ni walokole sio ulokole was gwajimaboy...najenga picha Kama Mimi ningefumania ?, kama Mimi ningekuwa mzazi wa binti ? . kikubwa tulia sikiliza upepo lakini usiende huko ni aibu ya maumivu yanayoumiza kiundani undani .
 
Duh asee unasema aende tu ? labda Kama hao wazazi ni walokole sio ulokole was gwajimaboy...najenga picha Kama Mimi ningefumania ?, kama Mimi ningekuwa mzazi wa binti ? . kikubwa tulia sikiliza upepo lakini usiende huko ni aibu ya maumivu yanayoumiza kiundani undani .

.
Ndo kuwajibika huko, stage ya kufumaniwa imeshapita Mangi....
 
Binti ndiye kajiaribia wala sio wewe kwani angekukatalia seriously kwake ungeenda kufanya nini?
Wanawake wa sasa hawana misimamo

Dadek wanawake wasenge sana ww huna makosa kama alikuweka waz kuwa ametolewa mahar ww ni fala
 
Sawa mkuu nitakuja na taarifa. Ngoja nipate maoni ya wadau

Kama alikuambia ameshakaribia kufunga ndoa ww ukawa kinganganizi bas atakaapoachwa ukubal kumuoa kama mwazo na umpende
 
dah, mm ningekaa mbali kabisa na huyo binti,
kwa kifupi hiyo familia itakumaliza hili ulilolifanya. huku mbelen kila issue watakumbushia hii ili uwatimizie shida zao.
yaani hapa utakuwa masikini ww na uzazi wako.
 
Mkuu nipo tayari kwa kila kitu kuhakikisha familia yao inapata amani na binti anapata heshima niliyoipoteza

Inaonekana unampenda sana...wanasema kila kitu ni fair lipanapokuja swala la mapenzi na vita, ila jiulize tu kama anastahili hiyo sacrifice. Usijenge nyumba yako kwenye msingi wa usaliti. Huyo mwanamke alichofanya ni usaliti kwa mchumba wake. Kama ni mtu wa maana angevunja uchumba kwanza... Ipo siku atakusaliti
 
Inavyoonekana huyo mwanamke alipewa onyo juu yako na alipokushirikisha haukutilia maanani, maana inaonekana anakujuwa vizuri na ukute ulipofika majirani walimpa taarifa hivyo alikuja akiwa tayari ana maamuzi, yaani ndugu zake kumtuliza inakuwa ngumu.
Kibaya utakuta umeoa na haukuwa na nia ya kumuoa, kama unamuona ni mwanamke anayekufaa haupaswi urudi nyuma kama ambavyo ulifanya alipokupa onyo juu ya kuwa na mahusiano lakini haukupunguza mapenzi kwake.
Mapenzi yale yale uliyokuwa nayo ndiyo unapaswa uyaoneshe kwake...
Kwa ushauri wangu kubali kwenda ila usiende leo subiri kidogo papoe, naamini kwasasa labda ndugu wakawa na jazba zaidi.
Utakuta jamaa alikuwa anamtafutia sababu namna ya kumuacha sababu ameipata tena amekukabidhi wewe, lawama hapati tena na mahari akipewa anaanzisha biashara.
Ushauri mzuri. kwa kuongezea tu jamaa hapaswi kwenda peke yake. kwa tahadhari asiende peke yake.
 
Ndugu mteja kwa usafiri wa hara na uhakika wa kwenda huko kwenye kesi yako ya ufirauni panda Kimbinyiko Bus Service.Furaha ya mteja ndio Fahari yetu
 
kwanza mshukuru mungu jamaa hajakudhuru, huyo demu anakuzingua kosa lake pia we achana naye, kama unataka msaidia mpigie jamaa umtetee demu nayo ni upuuzi, we katibu kwa mungu wako mblock huyo demu
 
Mtu akishakuambia nina mchumba usitumie udhaifu wake kumrubuni, kuwa mwanaume na sio picha ya mwanaume.
Unatakiwa kumuepuka ili kulinda heshima ya mshikaji kwani leo kwake kesho kwako.
Wanawake ni dhaifu na wanaweza fanya huo ujinga bila kujua kwa kutambua hilo mwanaume rijal atajiepusha na wale ambao mikono yao haiwamiliki.
 
Back
Top Bottom