Nimeumizwa na tukio hili

Nimeumizwa na tukio hili

Dah hata mm nimeumizwa kwa kweli.yaani hapo naona unajilaumu kwa nn ulimrudisha utajilaumu mengi ila mungu alishapanga hilo.pole mkuu
 
Hii kitu nimeiwaza sana.
- Kwanza mtoto wa miaka 13 asingeweza kusitahimili mambo mliyomfanyia; kumtoa shule, kumkabidhi kwa wazazi yaani mama, baba wa kambo, babu na bibi na serikali ya kijiji - mlimuumiza sana.

- Baada ya makabidhiano, ina maana kwamba yeye shule imekwisha vinginevyo akasome shule za akina lulu za kidumu na mfagio - asingeweza pia.
========================================================================
- Ingekuwa ni huko kwa wenzetu mngeshtakiwa.

========================================================================
- Je, utakuwaje salama wewe na wanao kwenye kijiji ambacho yametokea mambo mazito kama hayo?
========================================================================

======== Wakati mwingine angalia sana wema wako, vinginevyo utazidi kuumizwa ===============
 
Nikweli wema umenijeruhi..
Lakini naweza sema jamaa alikua na wivu wa kipuuzi na ukizingatia sikua karibu na familia yao na hata mkewe pia. Nathubutu kusema jamaa hakua mwanaume anaejiamini

Uko sahihi....tatizo lake lilikua kutojiamini...lakini mtu akipenda pia wivu unakuwepo....kama alikua na uwezo wa kumlipia ada marehemu nadhani isingekua busara wewe kuendelea kulipa...but maji yamemwagika...pole
 
Pole sana mkuu ndio mitihani ya maisha hiyo....inshaallah Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi.
 
Na michepuko pia aisee maana kama si michepuko we na mama yake msingeachana

Mkuu, tunapo kutana na kuanzisha mahusiano tunapaswa kuikabili misukosuko pamoja na tofauti, hizo zote ni changamoto tu katika kila mahusiano.
 
Pole sana mkuu ila kama ungejua ungemwambia huyo mume wa ex- wako amlipie ada aendelee kusoma hapo. Wewe unamlipia wa kwako na yeye anamlipia wa kwake.
 
Dah hata mm nimeumizwa kwa kweli.yaani hapo naona unajilaumu kwa nn ulimrudisha utajilaumu mengi ila mungu alishapanga hilo.pole mkuu

Asante kwa kunifariji mkuu
 
Pole sana mkuu ila kama ungejua ungemwambia huyo mume wa ex- wako amlipie ada aendelee kusoma hapo. Wewe unamlipia wa kwako na yeye anamlipia wa kwake.

Ingekua ngumu mkuu sababu jamaa hatukua karibu kimazungumzo, ukizingatia tayari walikua na migongano kwasababu ya mtoto kugoma kwenda kwa wazazi wake kipindi cha likizo ya mwezi JUNE
Na tayari nilikua nimekwisha pata tuhuma na malalamuko mengi kwamba namsababisha x Kuwa na jeuri kwa mumewe.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana kwa hilo,huna kosa lolote,jisamehe na maisha yasonge mbele
 
Pole sana, wewe huna kosa kwani nia yako ilikuwa ni njema, Mungu atakusaidia na utakuwa na amani moyoni mwako
 
Kipindi kile nilikwambia tuoane msukuma mwenzangu ukanigomea ona sasa

Teh..teeh...teeehh.....!!
Tatizo nimeshakua mzee....
Ukiongeza na huu ushamba, ndo majanga tupu....
Loohh......!!
 
Back
Top Bottom