Nimeumizwa na tukio hili

Nimeumizwa na tukio hili

pole sana mkuu! laiti usingechepuka yote haya yasingetokea!ungeendelea kuwa na mama yake hivyo huyo mwanaume asingemuoa mama yake! kuhusu huyo mume kuja juu kwa mtoto kulipiwa ada na wewe ex wa mke wake,alikuwa sahihi kabisa.
Mume wa x - wake hakupaswa kuja juu kuhusu mtoto kulipiwa ada, kwa sababu alijua fika kwamba kabla ya kumwoa huyo mke, alikuwa na uhusiano na huyo baba anayemsomesha mtoto. Alitakiwa kutambua tu kwamba yaliyopita si ndwele...
 
quote_icon.png
By Silicon Valley
pole sana mkuu,, NAPATA SHAUKU YA KUELEWA UMRI WA HAWA WATOTO PLEASE
Wakwangu pacha, mvulana na msichana umri miaka 10 wanasoma darasa la 4.
Marehem alikua na umri wa miaka 13, alikua na jinsia ya kike na alikua darasa la 6

acha uongo kijana
 
Kweli inauma sana mkuu.
Wajua ndio shida ya mijanaume mingine inaoa mtu sasa kila siku ni furu kujishtukia shtukia tu.....sasa kamsababishia indirect death mtu asiye na hatia...R.I.P mtoto .
 
Pole ndugu,
Mungu akutie nguvu
la msingi ni dhamira yako kwakuwa hukua na nia mbaya
basi amini kuwa hauhusiki kwa lolote

Be strong and take courage
 
Kabisa ndugu yangu, hoja yangu ni kwamba mtoto, tena wa kike ambaye ni vulnerable, mi nisingekubali kumtoa shule hta iweje! jamani shule haina mbadala

Nimekuelewa mkuu, lakini kumbuka mtoto yule sikuwa hakua wakwangu na hatukua na kiunganishi chochote zaidi ya kipindi nilipokua kwenye mahusiano na mama yake.
pia niliamua kumrudisha kwa mamayake ili nibaki pasipo vikwazo ukizingatia pia mama wa binti alikua tayari ameolewa na pengine mimi kuendelea kukaa na mtoto wao ingepelekea migogoro kuzidi ndani ya ndoa yao.
mwisho niseme tu kwamba hakuna alie taraji kama hili lingetokea.
 
Nahisi walikua na migogoro ya hapa na pale kuhusiana na swala zima la mtoto (marehem)
Pia kunakipinda niliwahi kupata taarifa kwamba jamaa alikua akimtuhumu mkewe kwamba haiwezekani asomeshewe mtoto bure, pengine alihisi kuna kitu au mahusiano yanaendelea

Sawa ulitenda wema lakini pia kitendo chako cha kuendelea kumhudumia yule mtoto hakikuwa sahihi...Any man would doubt that,...ila pole sana...umekuwa mhanga wa wema wako
 
Sawa ulitenda wema lakini pia kitendo chako cha kuendelea kumhudumia yule mtoto hakikuwa sahihi...Any man would doubt that,...ila pole sana...umekuwa mhanga wa wema wako

Nikweli wema umenijeruhi..
Lakini naweza sema jamaa alikua na wivu wa kipuuzi na ukizingatia sikua karibu na familia yao na hata mkewe pia. Nathubutu kusema jamaa hakua mwanaume anaejiamini
 
Back
Top Bottom