Nimeumizwa na tukio hili

Nimeumizwa na tukio hili

ushiboy na x mna makosa makubwa sana.

1. Kitendo cha kuwahusisha/kuwaingiza watoto katika mahusiano yenu ili hali nyie wenyewe hamjui direction ya hayo mahusiano, nimlaumu zaidi x wako kwa kuku introduce kwa bintie wakati hajakufahamu vizuri. Ni vibaya sana kuwa na uhusiano then kwa haraka mnaingiza watoto kwenye mahusiano bila kujadili kwa kina mustakabali wa nyie kuwa pamoja.

2. Wanawake mjifunze hapa, kuwaingiza mahawara wenu katika maswala ya watoto wenu, kabla ya kuhakiki future yenu na hao mahawara.

3. Hii story bado haijakamilika, mie naweza kuhisi ushiboy alishikwa na wivu na ndio maana karudisha mtoto, japo ni sawa kufanya hivyo.

Azawaiz poleni sana..
 
Last edited by a moderator:


Hakika una kesi ya kujibu hapo kwenye bold. Usingechepuka huyo mwenzako asingekupiga kibuti na mtoto angekuwa salama hadi amalize shule. Shame on you!

Shame on you with your comment too
Una judge vitu ambavyo Hata havina close relation
Soma story vizuri uielewe halafu ujipostion wewe ungekua muhusika ungefanyaje🙄
 
Umalaya matokeo yake ndo haya inauma2 mana nguvukazi ya Taifa imepotea kisa ushenzi wenu wote watatu nyoko zenu.
 
Kuna binadamu wengine hawajui maana halisi ya mapenzi,mpaka mtu unafikia kuoa ina maana unakuwa na uhakika wa mapenzi kwa huyo unayemuoa,kifo cha mtoto kilisababishwa na ulimbukeni wa mapenzi usio kuwa na msingi,muoaji angeendelea kulipa tu ada na isingekuwa shida kuliko walivyotaka mpaka kupelekea kifo cha mtoto.
Pole sana mkuu maana yule alikuwa ni mtoto wako kabisa ingawa si wa kumzaa.
 
Salam kwenu wana jamvi.

Mtanivumilia kwa urefu wa habari hii.

Niliwahi kuwa kwenye mahusiano na mdada ambae alikua na mtoto mmoja, huku nami nilikuwa na watoto wawili (mapacha). Wakati wote wa mahusiano wetu tulikubaliana kuwapeleka watoto wetu wakasome kwenye shule moja na niliamua kua namlipia ada pia kama wanangu.

Na wakati wote wa mahusiano yetu tulikua tukiishi mbali mbali nikimaanisha kila mmoja akiwa nyumbani kwake.

Shida ilikuja baada ya kuhisi ninachepuka na mdada mwingine hali iliopelekea kutofautiana na kuvunja mahusiano yetu kabisa. Baada ya muda x-wangu alipata mc
humba na pasipo kuchelewa jamaa akamuoa na maisha yakaendelea.

Matatizo yalianza pale mume wa x-wangu alipogundua kua namlipia ada mtoto wa mke wake na kipindi cha likizo ya watoto waliporudi toka shule, yule mtoto wa x-wangu aligoma kwenda kwa mama yake na alikatalia kubaki nyumbani kwangu kwakua walikua tayari wamezoeana na watoto wangu, huku wakimuita dada kwani alikua amewazidi umri.

Hali hii ilianza kuleta mgogoro kwenye ndoa ya x- wangu hadi kupelekea yule jamaa kuanza kutoa maneno ya vitisho kwangu. Na wakati haya yakitokea kuhusu migogoro mimi sikuwepo Tanzania, zaidi nilikua nikipata taarifa kutoka kwa watu wa karibu.

Niliona isiwe tabu, nikaamua nimtext x- wangu kwamba nikirudi likizo nitamtoa mtoto wake shuleni na nitamrudisha kwake maana sihitaji wema uniponze.

Kipindi niliporudi likizo nilifanya taratibu zote na nikamfuata mtoto shuleni na nikaenda kumkabidhi kwa wazazi wa x, mbele ya mjumbe, x na mumewe na wazazi wa x. Pia niliomba tukabidhiane kwenye maandishi kwa sababu ya kujiweka upande salama.

Cha kushangaza mtoto yule (binti) alilia sana na huku aking'ang'ania kwamba nisimuache, hakika mtoto yule alilia hadi wote tukajiskia huzuni kubwa. Ilibidi nimdanganye mtoto kwamba nitamfuata baada ya kuwasalimia bibi na babu yake.

Siku ya tatu sasa imepita, naambiwa binti (mtoto) yule amefariki dunia kwa kujirusha kwenye kisima cha maji.

HAKIKA NIMEUMIZWA SANA NA TUKIO HILI

e mungu nijalie wiv wa maendeleo
 


Hakika una kesi ya kujibu hapo kwenye bold. Usingechepuka huyo mwenzako asingekupiga kibuti na mtoto angekuwa salama hadi amalize shule. Shame on you!

My shame is your lesson mkuu
Simple as that
 
ushiboy na x mna makosa makubwa sana.

1. Kitendo cha kuwahusisha/kuwaingiza watoto katika mahusiano yenu ili hali nyie wenyewe hamjui direction ya hayo mahusiano, nimlaumu zaidi x wako kwa kuku introduce kwa bintie wakati hajakufahamu vizuri. Ni vibaya sana kuwa na uhusiano then kwa haraka mnaingiza watoto kwenye mahusiano bila kujadili kwa kina mustakabali wa nyie kuwa pamoja.

2. Wanawake mjifunze hapa, kuwaingiza mahawara wenu katika maswala ya watoto wenu, kabla ya kuhakiki future yenu na hao mahawara.

3. Hii story bado haijakamilika, mie naweza kuhisi ushiboy alishikwa na wivu na ndio maana karudisha mtoto, japo ni sawa kufanya hivyo.

Azawaiz poleni sana..

Ingawa siwezi kataa mawazo yako mkuu.
Ila kwa issue hii bibafsi sikupata kujiskia wivu kwasababu sikua karibu sana na x kimawasiliano na kwakuongeza tu nikwamba, wao walikua wakiishi Tz na mimi nimekua nikiishi nje ya Tz. Hata ukaribu wangu wa watoto umekua kwa kipindi nikiwa likizo tu.
Pili nilifanya kumrusisha mtoto baada ya ndoa ya x kuingia migogoro ilikihusisha Jamaa kutaka mtoto arudishwe na akaishi nao kwa madai kuendelea kulipiwa ada na mimi na kusoma shule ya gharama inaongeza dharau kwa familia yao.
 
Last edited by a moderator:
Umalaya matokeo yake ndo haya inauma2 mana nguvukazi ya Taifa imepotea kisa ushenzi wenu wote watatu nyoko zenu.

Good
Pengine imekua ni fundisho kwako pia kwa kupitia sisi.
Ingawa sivema kutoa matusi
 
Kuna binadamu wengine hawajui maana halisi ya mapenzi,mpaka mtu unafikia kuoa ina maana unakuwa na uhakika wa mapenzi kwa huyo unayemuoa,kifo cha mtoto kilisababishwa na ulimbukeni wa mapenzi usio kuwa na msingi,muoaji angeendelea kulipa tu ada na isingekuwa shida kuliko walivyotaka mpaka kupelekea kifo cha mtoto.
Pole sana mkuu maana yule alikuwa ni mtoto wako kabisa ingawa si wa kumzaa.

Nikweli mkuu. Kwangu haikua mbaya kumlipia ada, kwani mungu kanijaalia kiasi cha kumudu huo ulipaji wa ada na tayari alikua amezoeana na watoto wangu kama dada yao.
Kilicho nifanya nimrudishe mtoto ni mambomengi, kero, vitisho, vurugu na kubwa ni kuonekana nakua chanzo cha migogoro kwenye ndoa ya x
 
Nikweli mkuu. Kwangu haikua mbaya kumlipia ada, kwani mungu kanijaalia kiasi cha kumudu huo ulipaji wa ada na tayari alikua amezoeana na watoto wangu kama dada yao.
Kilicho nifanya nimrudishe mtoto ni mambomengi, kero, vitisho, vurugu na kubwa ni kuonekana nakua chanzo cha migogoro kwenye ndoa ya x
Mkuu wewe ulikuwa ni baba kwa huyo mtoto wala hakua anajali ni nani analipa ada,ingekuwa mimi ningekushukuru kwa kazi ambayo ulikuwa unaifanya na tungezungumza nini cha kufanya si kwa vitisho wala maombi ya kujifanya wana uchungu na mtoto,mtoto kapotea kwa jambo dogo sana ambalo lilikuwa linaweza kuzungumzwa na kuwekwa sawa.
Inaumiza sana mtoto kupoteza maisha na ndoto zake,watoto wako wanaumia sana sasa hivi kumpoteza ndugu yao.
 
pole sana ushiboy
binti hayupo tena
kweli umefanya mengi kwa mtoto na ulikuwa kama baba yake maana kuchukua majukumu ya malezi ni baba .
ulifanya maamuzi ya haraka sana kumtoa mtoto shule laiti kungefanyika mazungumzo kabla ya mtoto kutolewa shule labda haya ya singekuwepo (au kuna msemo usemao kifo lazima kuwepo sababu).
 
Last edited by a moderator:
pole sana ushiboy
binti hayupo tena
kweli umefanya mengi kwa mtoto na ulikuwa kama baba yake maana kuchukua majukumu ya malezi ni baba .
ulifanya maamuzi ya haraka sana kumtoa mtoto shule laiti kungefanyika mazungumzo kabla ya mtoto kutolewa shule labda haya ya singekuwepo (au kuna msemo usemao kifo lazima kuwepo sababu).

Asante...
Pia kuoitia kwangu nadhani nifundisho kwa wengine blaki
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom