Nimetofautiana na jirani yangu, naombeni ushauri

NAKWEDE

JF-Expert Member
Aug 1, 2007
27,971
35,113
Nilishajiridhisha siku nyingi kuwa hapa JF ni kisima cha faraja na pia kuna maudhi madogo madogo. Nina tatizo na jirani yangu kiasi kwamba nimekosa ufumbuzi hadi nimefikia maamuzi ya kuwaomba ushauri wanaJF.

Ni kwamba kuna jirani yangu ambaye yeye hajajenga bado (ni uwanja/kiwanja) tu. Katika kiwanja chake hicho amepanda miti ya aina ya mikaratusi imekuwa mirefu sana. Miti hiyo amepanda hadi mpakani kabisa na kwangu. Kunapokuwa na mvua na upepo mkali miti inainama hadi inakwaruza bati la nyumba yangu.

Nimemuomba sana akate miti minne ambayo ndio hatarishi lakini yeye majibu yake siku zote ni kwamba, hawezi kukata miti yake kwa kuwa ndio inayokipa kiwanja chake thamani siku akitaka kukiuza. Nilimuliza ni vipi athamini hela kuliko uhai wangu na nyumba yangu akasema kwa hilo nitamsamehe labda akate mti mmoja tu.

Naomba mnisaidie je hili suala nilipeleke kwenye mamlaka ipi ya serikali? Nakiri kuwa negotiation na mediation vimekwama kabisa.

Petro E. Mselewa nisaidie mkuu na wengineo wengi
 
Mkuu NAHUJA, hilo jambo lako lina sura mbili. Mosi, linaweza kutatuliwa kijamii nje ya vyombo vya kisheria. Yaani, kukutana au kukutanishwa wewe na jirani yako ili kuyaongea na kuyatatua. Pili, linaweza kumalizwa katika namna ya kimahakama. Napo hapo kuna njia mbili.

Ya kwanza ni kulipeleka kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kama kuna kuingia kwa miti hiyo katika eneo lako, yaani trespass. Ya pili ni kufungua shauri chini ya sheria za madhara (law of torts) kwa usumbufu na kuingiliwa na hiyo mikaratusi katika eneo lako. Shauri hilo linafunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi.

Ni shauri linaloweza kuomba kuondolewa kwa kero na fidia kwa madhila yote uliyoyapata. Chagua na uamue.
 
Ningekuwa ni mm ningeenda kutafuta mashine ya kukatia miti/mbao then nasubir usiku mnene uingie naenda kuikata hyo miti yote na kurejesha mashine kwa mwenye nayo usiku kwa usiku,kesho asbh akniuliza nitamwambia sifaham chochote na nilikuwa safarini na familia yangu (nitamuonyesha na tiketi kama ushahidi)

Aaaaagh! Mahakamani,kwa balozi na kwenye mabaraza ya ardhi au kata ni kupotezeana muda!
 
Ningekuwa ni mm ningeenda kutafuta mashine ya kukatia miti/mbao then nasubir usiku mnene uingie naenda kuikata hyo miti yote na kurejesha mashine kwa mwenye nayo usiku kwa usiku,kesho asbh akniuliza nitamwambia sifaham chochote na nilikuwa safarini na familia yangu (nitamuonyesha na tiketi kama ushahidi)

Aaaaagh! Mahakamani,kwa balozi na kwenye mabaraza ya ardhi au kata ni kupotezeana muda!
Ahahahahahahahahahahahah we una akili kama mimi
 
Mkuu NAHUJA, hilo jambo lako lina sura mbili. Mosi, linaweza kutatuliwa kijamii nje ya vyombo vya kisheria. Yaani, kukutana au kukutanishwa wewe na jirani yako ili kuyaongea na kuyatatua. Pili, linaweza kumalizwa katika namna ya kimahakama. Napo hapo kuna njia mbili.

Ya kwanza ni kulipeleka kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kama kuna kuingia kwa miti hiyo katika eneo lako, yaani trespass. Ya pili ni kufungua shauri chini ya sheria za madhara (law of torts) kwa usumbufu na kuingiliwa na hiyo mikaratusi katika eneo lako. Shauri hilo linafunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi.

Ni shauri linaloweza kuomba kuondolewa kwa kero na fidia kwa madhila yote uliyoyapata. Chagua na uamue.
Ahsante sana Wakili msomi Petro E. Mselewa. nashukuru
 
Ngoja nisubiri wanasheria wadadavue hili jambo
Mkuu NAHUJA, hilo jambo lako lina sura mbili. Mosi, linaweza kutatuliwa kijamii nje ya vyombo vya kisheria. Yaani, kukutana au kukutanishwa wewe na jirani yako ili kuyaongea na kuyatatua. Pili, linaweza kumalizwa katika namna ya kimahakama. Napo hapo kuna njia mbili.

Ya kwanza ni kulipeleka kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kama kuna kuingia kwa miti hiyo katika eneo lako, yaani trespass. Ya pili ni kufungua shauri chini ya sheria za madhara (law of torts) kwa usumbufu na kuingiliwa na hiyo mikaratusi katika eneo lako. Shauri hilo linafunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi.

Ni shauri linaloweza kuomba kuondolewa kwa kero na fidia kwa madhila yote uliyoyapata. Chagua na uamue.
 
Mkuu NAHUJA, hilo jambo lako lina sura mbili. Mosi, linaweza kutatuliwa kijamii nje ya vyombo vya kisheria. Yaani, kukutana au kukutanishwa wewe na jirani yako ili kuyaongea na kuyatatua. Pili, linaweza kumalizwa katika namna ya kimahakama. Napo hapo kuna njia mbili.

Ya kwanza ni kulipeleka kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kama kuna kuingia kwa miti hiyo katika eneo lako, yaani trespass. Ya pili ni kufungua shauri chini ya sheria za madhara (law of torts) kwa usumbufu na kuingiliwa na hiyo mikaratusi katika eneo lako. Shauri hilo linafunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi.

Ni shauri linaloweza kuomba kuondolewa kwa kero na fidia kwa madhila yote uliyoyapata. Chagua na uamue.
Tatizo hapa litatatulika 100%
 
Unamuwaza huyo waki? Tafuta chain saw kata miti hiyo mwekee hapo kiwanjani kwake aje achukue kuni. Ukimwendekeza atakuona lofa.

Akileta za kuleta mtandike kisha mpeleke sero alale siku tatu apate akili.
 
Ningekuwa ni mm ningeenda kutafuta mashine ya kukatia miti/mbao then nasubir usiku mnene uingie naenda kuikata hyo miti yote na kurejesha mashine kwa mwenye nayo usiku kwa usiku,kesho asbh akniuliza nitamwambia sifaham chochote na nilikuwa safarini na familia yangu (nitamuonyesha na tiketi kama ushahidi)

Aaaaagh! Mahakamani,kwa balozi na kwenye mabaraza ya ardhi au kata ni kupotezeana muda!
hahahahh, monde arabe, hiyo ngumu kwa sababu ile miti kwanza ni mirefu kiasi kwamba hata siku ikikatwa inabidi wakati wawe na kamba, pia waangalie upepo unaelekea wapi ili isiangukie nyumba. hahahhahaha. ahsante kwa ushauri wako mwaya
 
hahahahh, monde arabe, hiyo ngumu kwa sababu ile miti kwanza ni mirefu kiasi kwamba hata siku ikikatwa inabidi wakati wawe na kamba, pia waangalie upepo unaelekea wapi ili isiangukie nyumba. hahahhahaha. ahsante kwa ushauri wako mwaya
Kuna majirani hawana utu mioyoni mwao hata kidogo...atataka msumbuane mpaka mmalize fedha na muda kwa jambo dogo!
 
Unamuwaza huyo waki? Tafuta chain saw kata miti hiyo mwekee hapo kiwanjani kwake aje achukue kuni. Ukimwendekeza atakuona lofa.

Akileta za kuleta mtandike kisha mpeleke sero alale siku tatu apate akili.
Hiyo ya kukata miti siwezi ni mirefu sana inatakiwa kukatwa kwa ufundi ili isiangukie nyumba. Kuhusu kumtandika makofi sina nguvu za kumpiga ni mwanamme. hahahahah mimi ni mwanamke. Kumlaza selo ni ngumu ni POLISI
 
Kuna majirani hawana utu mioyoni mwao hata kidogo...atataka msumbuane mpaka mmalize fedha na muda kwa jambo dogo!
Yaani huyo kaka ni jeuri sana (mkurya). Ananijibu kwa kiburi eti "hiyo miti ndio thamani ya kiwanja changu, sina mpango wa kujenga hapo, hicho kiwanja kiko sokoni. Labda nikate mti mmoja tu." Kiwanja kizima kimejaa mikaratusi, na kiko katikati ya nyumba za watu!!!!:(:(:(:(:(:(:(:(
 
Kweli kabisa Joblee hata mimi nimepata ufumbuzi, yaani jana nilikosa raha sana na vile mvua ilikuwa kubwa upepo, tafrani.
Sema kwa kuwa ni jirani yako, kama na yeye atakuwa na mpango wa kujenga hapo ni vyema mkayaongea kabla ya kufika kwenye vyombo vya sheria... maana huenda baadae mmoja wenu akawa msaada kwa mwingine hapo baadae... ujirani mwema
 
Back
Top Bottom