Nimesimamishwa masomo Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

watu kama wewe ndio mnatupa taabu na ID zenu nyingi nyingi, afadhali "wamekunyamazisha", argh!!

duh?
Kumbe ukisimamishwa masomo unakuwa umenyamazishwa eh?
Nilikuwa siyajui hayo mie...
 
Kwema wanajamvi?
Kama kichwa kinavyojieleza, nilipokea ujumbe kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi saa 3 hivi asubuhi, ikinitaarifu kuwa nisubiri chumbani kwangu niletewe barua yangu. Karibu saa 7 hivi, baada ya kusubiri sana uvumilivu ukaniisha, nikaenda Nyerere Campus, nikapata barua yangu pale Auxilliary Police, iliyoeleza, nanukuu, "RE: SUSPENSION FROM STUDIES PENDING INVESTIGATION
Be informed that following your participation in the making of an illegal USRC desicion to defy Council orders, you have been suspended from studies pending futher investigation...", mwisho wa kunukuu. Nikakabidhi kitambulisho cha chuo kwa askari, tukaonana na viongozi wenzangu wa DARUSO, tukafarijiana na kuelekezana cha kufanya wakati huu mgumu.
Saa 11 jioni nikawa Mabibo Hostel kufanya taratibu zote za kuondoka chuoni, saa 11:30 hivi nikaondoka maeneo ya hostel kurudi nyumbani, ninakoishi.
Hii ni ID mpya, anayehitaji taarifa zaidi ani-PM.

Watanzania ni uvumilivu...ujinga kama huu ungefanyika elsewhere mambo yangekuwa ni magumu sana.Otherwise stand firm brother,hope you will stand!! Naumia wakuu natamani hata kufa,hali hii mpaka lini?
 
nashukuru sana mkuu kwa kunijali. Mimi ni Mtanganyika, usitishike na hayo maneno hapo juu...

Nna mashaka makubwa na uyasemayo, Watanganyika tulimaliza kusoma zamani, kama ndio kwanza upo chuoni, wewe hata hiyo Tanganyika hujaiona, pengine hata wazee wako hawajaiona wanaisikia tu.

Utaifa wako unanitia mashaka na namna unavyoandika nna uhakika si Mtanzania na wala si msomi, labda ndio ulikuwa "bize" kwa kuandaa na maandamano na vurugu hata masomo yakakupiga chenga?

Hustahiki hata kupewa pole. Waswahili hunena "kiranga komo", tena namuomba Mkandala asiwarudishe chuoni, wenye kutaka kusoma tunawaona wako "bize" wakijitayarisha na mitihani.
 
Wanafunzi lazima kila siku mkumbuke kuwa kile kilichowapeleka chuoni ni kusoma. Hicho ndicho kitu cha kwanza. Mambo ya siasa yapo uraiani mtayakuta mtakapomaliza shule. Mimi siungi mkono hata siku moja njia mnayotumia kudai haki zenu kama vile kwa kuwalazimisha wanafunzi wasioafiki matakwa yenu kwa kuwafukuza madarasani.
 
hahaha :lol::A S 465::lol::lol: mimi nasindwa hata kuhukumu au kulaumu sielewi maana ya kugoma ni nini maana cha zaidi nasikia uhribufu wa mali kumwagia chakula michanga kuwachapa viboko wenzao wanaoingia madarasani kujisomea na mengine neyo yanayoudhi. hivi ndio maana ya migomo na kudai haki kwa kufanya uharibifu? hapohapo wakati wengine wanagoma wengine wa EAC wanasoma je soko la ajira hapo baadaye litakuwa na uwiano wakati kutwa kucha ni migomo na uharibifu.
Tatizo la watu wazembe wa kufikiri. Nenda UDSM ukafanye research u will get the truth na usitegemee taarifa kutoka kwa TBC1, Star TV na n.k
 
Usife moyo, utarudi shule, kwa sasa tafuta shughuli ya kufanya ujipange upya
 
Usife moyo, utarudi shule, kwa sasa tafuta shughuli ya kufanya ujipange upya

Hana cha uanafunzi huyo, ni mtu ambae katumwa kufanya chokochoko, kila hoja yeye huingia au huanzisha kwa kusudi la kutenganisha na si kujenga, wengine tumesha mstukia ni nani. Msome vizuri utanielewa nnachosema.
 
nashukuru kwa upendo wako mkuu. Ila hata nikirudishwa masomoni, itanifaa nini endapo wenzangu 98+41 hawatarudishwa, itanifaa nini endapo umma wa UDSM, ambako kulitakiwa kuwa kitovu cha mafikara, utaendelea kugandamizwa kimawazo na watawala wetu wakishirikiana na wakuu wa vyuo?
Nadhani ipo jinsi mkuu, zaidi ya kutegemea huruma ya MUUMBA.

Hiyo kauli ni tosha kabisa kuwa wewe ni mchonganishi na si mwanafunzi wa UDSM na wala hukufukuzwa chuo.
 
Usife moyo, utarudi shule, kwa sasa tafuta shughuli ya kufanya ujipange upya

nashukuru mkuu.
Kwa sasa niko kitaa, kwa kuwa kuna fununu kuwa senate ya chuo inaeza kutuita muda wowote. Siwezi kuwa na long plan kwa sasa...
 
Watanzania ni uvumilivu...ujinga kama huu ungefanyika elsewhere mambo yangekuwa ni magumu sana.Otherwise stand firm brother,hope you will stand!! Naumia wakuu natamani hata kufa,hali hii mpaka lini?

I'll stand firm.
I promise, ila usife ndugu. Ukifa nani atasimama kwa wanyonge?
Tunataka uzao utakaotukoa na mabosi wa akina FF, we need way forward...
Sawasawa?
 
mungu atakusaidia.sina mengi ya kukwambia ndugu yangu zaidi yakuona nchi inaelekea pabaya badala ya kuongeza wasomi tunapunguza
 
Wanafunzi lazima kila siku mkumbuke kuwa kile kilichowapeleka chuoni ni kusoma. Hicho ndicho kitu cha kwanza. Mambo ya siasa yapo uraiani mtayakuta mtakapomaliza shule. Mimi siungi mkono hata siku moja njia mnayotumia kudai haki zenu kama vile kwa kuwalazimisha wanafunzi wasioafiki matakwa yenu kwa kuwafukuza madarasani.

eti eh?
Ile sio siasa ndugu, ni kudai haki ya wengi inayoporwa na wachache. Kuidai ni wajibu wa yeyote, na sio mtu fulani.
Kusoma kunakuwaje kwa raha kama wengi wenu hawana mikopo, ambayo ndiyo inayowaweka mjini. Yet, haohao ndio walisomeshwa bure na JKN.
Inauma uchungu alooo...
 
Hivi bado hamjamstukia huyu Sobhuza? hata lugha yake inaonesha kabisa kuwa huyu si Mtanzania na yupo hapa kutia fitna. Nawashangaa sana ambao bado mnamuunga mkono.

Mimi nnapinga huyu si mwanafunzi wa UDSM na wala hajafukuzwa chuo.
 
Hivi bado hamjamstukia huyu Sobhuza? hata lugha yake inaonesha kabisa kuwa huyu si Mtanzania na yupo hapa kutia fitna. Nawashangaa sana ambao bado mnamuunga mkono.

Mimi nnapinga huyu si mwanafunzi wa UDSM na wala hajafukuzwa chuo.
wewe kijana wa nape, inatosha sasa
 
DARUSO kwa upande mwngn mmeboa sana, mmesubiri sana watu wasahau ndo nyie mnaibuka w,isho ndo maana mmekosa mashiko na sapot toka kwa watu. pia seikali yenu imegawanyika sana na mmesababisha wanafunzi wengi zaidi kufukuzwa.
hongera sana na nyie mmeonja utam wa kuvaa kaptura kuuuubwa wakati viuno vyenu vidogo.
:hat:
 
Jiandae kuwa mtu wa vijiweni. CDM wamekuponza. Nenda kawaone, labda wanaweza hata kukupa kaz ya kuwa mfagizi wa ofisi zao chafu chaf pale Kinondoni!
 
Back
Top Bottom