Nimesimamishwa masomo Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Pole sana ila kwanini umeogopa kuja na ID Yako ya zamani? Unanipa mashaka kama kweli wewe ni mpigania haki au bendera.

Si vibaya kuja na ID mpya ila hata mimi nashaka kwanini kwenye haki yako uwe Muoga? hapa ndio panaponitia wasiwasi kwani uliyoyafanya wewe ni kuua mtu au? Mi nadhani kama vyombo vya hbr vinatoa hbr hizi wewe uliyeathirika unajificha nani atakusaidia? Je leo Wakija TBC kwa kutaka uwaeleze nini kilitokea utaficha sura yako?
 
migomo mogomo hili lichuo ukiingia tu pale unapata degree mbili my self niunazo mbili na hii ya mgomo nina first class.........
 
Mnapokuwa Viongozi feedback ni muhimu sana kwa wale mnaowaongoza ni nani Mwana UD alijua kuwa mlikuwa mnakosa VENUE? kama mliamua kukaa kimya hamkuona si utawala Bora huo ? Kiongozi panapotokea hali yoyote ile ya matatizo au mazuri cha kwanza ni Taarifa? Leo hii hakuna Mwana UD utakaye Mwambia mlikuwa bega kwa Bega ili kushughulikia matatizo yote yale yaliyokuwa yakitokea. Ni wazi kuwa mliweka matabaka kiasi cha kulaumiwa na Wanachuo wote hadi wanachuo wakataka kuanza harakati za kuuondoa Uongozi wa chuo madarakani? Je Mlikuwa wapi toka harakati zinaanza Mbona zilitolewa makala kibao za kushindikiza wanafunzi waache migomo kwani wanavunja sheria.Mliona nini kutoa makala kama hizo na za kueleza umma kuwa Utawala unaweka vikwazo kama hivyo? Leo hii hakuna anaeona uchungu kwa kuondoka kwenu kwani kila aliyekuwa akidai haki aliwachukulia kama wasaliti tu.....Leo hii kimya chenu cha muda mrefu ndio kimezua balaa lakini kama kiongozi taarifa ni Muhimu sana ...mwanaphilosophy Jean Jacques Rousseau alisema
''Absolute silence leads to sadness. It is the image of death''.

inawezekana taarifa hazikuwa zinafika kwa muda, ni tatizo hilo.
Ila tatizo kubwa zaidi ni wanafunzi kutokuelewa jinsi mfumo wa kiutendaji wa DARUSO ulivyo, hali inayopelekea kulaumu kila kiongozi wa DARUSO kwa jambo lolote. Mfano, sisi tulikuwa ni wajumbe wa kawaida wa USRC, hatuwezi kutoa maazimio mpaka tukae kikao chetu, ila mara nyingi huwa tunalaumiwa kwa makosa ambayo yanafanywa na viongozi wa DARUSO upande wa Cabinet...
 
Si vibaya kuja na ID mpya ila hata mimi nashaka kwanini kwenye haki yako uwe Muoga? hapa ndio panaponitia wasiwasi kwani uliyoyafanya wewe ni kuua mtu au? Mi nadhani kama vyombo vya hbr vinatoa hbr hizi wewe uliyeathirika unajificha nani atakusaidia? Je leo Wakija TBC kwa kutaka uwaeleze nini kilitokea utaficha sura yako?

hapana mkuu. Haya ni masuala ya jamvini, hata ningekuja na ID yangu ya siku zote, ni wachache sana wanaonifahamu in personal humu. Na karibu wote wanafahamu chenye kilinikuta...
Naomba nieleweke ivo untill further notice.
 
hapana mkuu. Haya ni masuala ya jamvini, hata ningekuja na ID yangu ya siku zote, ni wachache sana wanaonifahamu in personal humu. Na karibu wote wanafahamu chenye kilinikuta...
Naomba nieleweke ivo untill further notice.

Uhuru una gharama kubwa, hongera kwa ajili ya uhuru, pia pole kwa ajili ya mwili. kama hutojali waweza nijibu, wewe ni mtz, mkenya au mbaganda.
 
Uhuru una gharama kubwa, hongera kwa ajili ya uhuru, pia pole kwa ajili ya mwili. kama hutojali waweza nijibu, wewe ni mtz, mkenya au mbaganda.

nashukuru sana mkuu kwa kunijali. Mimi ni Mtanganyika, usitishike na hayo maneno hapo juu...
 
Enyi DARUSO msiwe mbwa koko, nendeni mahakani kutengua maamuzi ya kibabe ya mkandara. HUBE AMKENI
 
Chuo kikuu kinaendeshwa mechanically kuliko hata mechanical engineering department. Haiwezekani kila siku ni kufukuzana chuo tu. That is not the permanent solution to the existing problems. Naamini kuna namna bora ya kuendesha mambo pale zaidi ya kufukuzana tu.
 
Sasa kusimamishwa masomo wana udsm na Chadema vina uhusiano gani?? Mbona hujasema CCM itamlipia masomo india?? I dought you might be having a.al fistula.

Mkuu ingawa rizione katoa comment yake kishabiki shabiki lakini ana point.
Serikali inaamini kwamba kila mgomo unapo tokea ni kazi ya chadema
na kwakua hawataki kushindwa na chadema,yeyote atakae goma anafukuzwa haraka sana wakiamini kwamba
ni mwana chadema au kashinikizwa na chadema.
Hapa inabidi wabunge wahoji kwanini fukuza fukuza hii ya kipuuzi namna hii?

Nakumbuka rafiki zangu hawa,ninasoma nao cozi moja walikua wanapinga sana uonevu,lakini wakawa
wanaamini kwamba kugoma sio njia muafaka kwanza,....siku hiyo waliposema waliniudhi sana
kwani naamini mgomo ndio njia pekee hapa udsm ya kupata suluhisho la matatizo yenu.

Leo wamefukuzwa kwa sababu tu,wamehudhuria kikao cha bunge,na wameshiriki kikao
kilicho pitisha maazimio ya mgomo,so painful.

hawa hapa kwenye nipashe:
Wanafunzi wengine waliotimuliwa ni pamoja na Mkenda Paul, Msigwa Pangani, Nafti Daniel, Mwasakafyuka Edward,
Amoni Stephano, Wilfred Bocasa, Garubindi Gaston, Mwalusanya Wilfred, Mwalo Innocent na Malipula Edgar.
 
"You can ban an organization, you can liquidate people, but revolutionally idea never dies"
 
well said mkuu.
Jamaa ni watu wa visasi sana, hawachelewi kukomoa kabisa, kuzungumza nao kuna-make sense kwa sasa kuliko kukimbilia mahakamani, ukizingatia jamaa wana back-up ya mkuu wa kaya.

hapa wakuu mi naona hivi ni visasi tuu, vimezalishwa na uchaguzi mkuu uliopita, na msumari wake ukapigiliwa mlipo mzomea mzee wa kaya mbele ya M7.
haya ni maamuzi makubwa sana na magumu yaliyo tolewa na chuo. kufukuza serikali si mchezo. hivyo inahitajika busara kuu ku solve,.
 
me sikupi pole, ila nakutia moyo. Me niko home toka mwezi wa 6 last year baada ya mgomo, nimehojiwa nasubiria majibu yao. Ila bilieve me hali hii imenijenga nakujua maisha hasa. Utakutana na wengi watakaokulaumu hata wa2 wa karibu, usiwamind we waeleweshe au wapotezee pia wapo wachache watakao kutia moyo. Ts just a mater of time..haki ya mtu haipotei
haki ya mtu haipotei na daima tutashinda hii vita ya ukandamizaji mnachokipigania kimanufaa kwa wengi kwame siwalaumu nasintothubutu ..maamuzi ya daruso ni halali kabisa kwani ndio chombo halali cha kuwawakilisha wanafunzi hapo udsm .. Migomo imesadia wengi nikiwamo mimi .. Kuna watu wengi wamesumbuliwa sana kwa kutetea umma wa wanaudsm na vitisho vingi ila mwisho wa siku tuko nao na mtaani wanaendeleza pambano mfano mzuri ni david silinde(mbunge mbozi magharibi ) mpaka mahakama walimpeleka mtatiro julius (naibu katibu mkuu cuf bara) na wengine wengi tu so kamanda usiogope utashinda kwani mtachotetea ni haki yenu
 
pole sana ila jambo la msingi ni kuwa jasiri na kuamini kuwa umefanya sehemu yako kwa maslahi ya uma. na ni vema sasa kujipanga pamoja na wenzio kuona namna gani mnaweza kulikabili hili. Mkumbuke umoja ni nguvu
 
well said mkuu.
Jamaa ni watu wa visasi sana, hawachelewi kukomoa kabisa, kuzungumza nao kuna-make sense kwa sasa kuliko kukimbilia mahakamani, ukizingatia jamaa wana back-up ya mkuu wa kaya.

pole sana mwanaharakati. Ila kam ni mtoto wa mkulima, imekula kwako mambo yakienda viceversa, itabid boom la mwisho ununulie power tiller.
 
pole mkuu ndio maisha yalivyo, jaribu njia nyingine sio mwisho wa maisha ndugu yangu.
 
pole sana kamanda ...haya yataisha wala usikate tamaa na mapambano. Ha wengine nikiweme mimi nishapatwa na mikasa hiyo,ila ninasonga mbele.
 
Kwema wanajamvi?
Kama kichwa kinavyojieleza, nilipokea ujumbe kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi saa 3 hivi asubuhi, ikinitaarifu kuwa nisubiri chumbani kwangu niletewe barua yangu. Karibu saa 7 hivi, baada ya kusubiri sana uvumilivu ukaniisha, nikaenda Nyerere Campus, nikapata barua yangu pale Auxilliary Police, iliyoeleza, nanukuu, "RE: SUSPENSION FROM STUDIES PENDING INVESTIGATION
Be informed that following your participation in the making of an illegal USRC desicion to defy Council orders, you have been suspended from studies pending futher investigation...", mwisho wa kunukuu. Nikakabidhi kitambulisho cha chuo kwa askari, tukaonana na viongozi wenzangu wa DARUSO, tukafarijiana na kuelekezana cha kufanya wakati huu mgumu.
Saa 11 jioni nikawa Mabibo Hostel kufanya taratibu zote za kuondoka chuoni, saa 11:30 hivi nikaondoka maeneo ya hostel kurudi nyumbani, ninakoishi.
Hii ni ID mpya, anayehitaji taarifa zaidi ani-PM.

Mkuu pole kwa kusimamishwa masomo. Naona umechanganyikiwa mpaka unaweka quotes zenye wrong spelling. Au hiyo barua ya chuo imekosewa hivyo hivyo? Mmesimamishwa wangapi so far?

Tiba
 
Nakupongeza sana kwa moyo wako wa kijasiri, nchi hii itajengwa na watu kama wewe, usikate tamaa, endelea na mapambano popote ulipo, waelimishe na wenzako wote wasikate tamaa, tupo pamoja.
 
Back
Top Bottom