Nimesimamishwa masomo Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Kwema wanajamvi?
Kama kichwa kinavyojieleza, nilipokea ujumbe kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi saa 3 hivi asubuhi, ikinitaarifu kuwa nisubiri chumbani kwangu niletewe barua yangu. Karibu saa 7 hivi, baada ya kusubiri sana uvumilivu ukaniisha, nikaenda Nyerere Campus, nikapata barua yangu pale Auxilliary Police, iliyoeleza, nanukuu, "RE: SUSPENSION FROM STUDIES PENDING INVESTIGATION
Be informed that following your participation in the making of an illegal USRC desicion to defy Council orders, you have been suspended from studies pending futher investigation...", mwisho wa kunukuu. Nikakabidhi kitambulisho cha chuo kwa askari, tukaonana na viongozi wenzangu wa DARUSO, tukafarijiana na kuelekezana cha kufanya wakati huu mgumu.
Saa 11 jioni nikawa Mabibo Hostel kufanya taratibu zote za kuondoka chuoni, saa 11:30 hivi nikaondoka maeneo ya hostel kurudi nyumbani, ninakoishi.
Hii ni ID mpya, anayehitaji taarifa zaidi ani-PM.
 
lol. Pole sana mdogo wangu. Hata sijui nianzie wapi but tatizo kubwa lililopo ni mfumo tulionao unaohalalisha UNYANYASAJI mkubwa namna hii. Panahitajika UMOJA hapa otherwise these guyz will screw us forever. Remember leo kwako kesho yaweza kuwa kwa mwingine. Hasira hizi unaweza pata hamasa ya kuingia msituni
 
Kwema wanajamvi?
Kama kichwa kinavyojieleza, nilipokea ujumbe kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi saa 3 hivi asubuhi, ikinitaarifu kuwa nisubiri chumbani kwangu niletewe barua yangu. Karibu saa 7 hivi, baada ya kusubiri sana uvumilivu ukaniisha, nikaenda Nyerere Campus, nikapata barua yangu pale Auxilliary Police, iliyoeleza, nanukuu, "RE: SUSPENSION FROM STUDIES PENDING INVESTIGATION
Be informed that following your participation in the making of an illegal USRC desicion to defy Council orders, you have been suspended from studies pending futher investigation...", mwisho wa kunukuu. Nikakabidhi kitambulisho cha chuo kwa askari, tukaonana na viongozi wenzangu wa DARUSO, tukafarijiana na kuelekezana cha kufanya wakati huu mgumu.
Saa 11 jioni nikawa Mabibo Hostel kufanya taratibu zote za kuondoka chuoni, saa 11:30 hivi nikaondoka maeneo ya hostel kurudi nyumbani, ninakoishi.
Hii ni ID mpya, anayehitaji taarifa zaidi ani-PM.


Pole sana, so painful.
Nyie ni representatives na hamkupaswa kuadhibiwa. Wenye uwezo wa kuwasaidia ni umoja wa wanafunzi wenzenu waliobaki.
Rest assured yana mwisho na watanzania wote wapenda haki tuko upande wenu.
 
Pole sana kwa masahibu yaliyokukumba, binafsi nimeona taarifa ya habari na kusikitika sana mustakabari wa elimu yetu unapoelekea.
 
lol. Pole sana mdogo wangu. Hata sijui nianzie wapi but tatizo kubwa lililopo ni mfumo tulionao unaohalalisha UNYANYASAJI mkubwa namna hii. Panahitajika UMOJA hapa otherwise these guyz will screw us forever. Remember leo kwako kesho yaweza kuwa kwa mwingine. Hasira hizi unaweza pata hamasa ya kuingia msituni

yeah mkuu.
Hatuna umoja kabisa, mwanzo DARUSO ilinyimwa vikao vya bunge lake, raia wakasema hawana wawakilishi. Juzi Jumamosi tukapata kikao halali, tukapitisha maazimio, ndio hayo yamezaa haya.
 
Pole sana, so painful.
Nyie ni representatives na hamkupaswa kuadhibiwa. Wenye uwezo wa kuwasaidia ni umoja wa wanafunzi wenzenu waliobaki.
Rest assured yana mwisho na watanzania wote wapenda haki tuko upande wenu.

wanafunzi waliobaki hawana umoja, na uoga umetawala sana. Lecture zote zinasimamiwa na defender moja ya FFU, na wenzetu bado wanataka kuenda madarasani. Tatizo ndipo lilipo...
 
pole sana ndugu yetu..naamini yote yataisha.

nashukuru mkuu. Haya hayawezi kuisha kwa kudra za muumba, madaraka matamu ndugu yangu, hasa haya yasiyo na uwajibikaji, ndio maana hawataki kuyaachia hao wenye nayo...
 
Sikio la MUNGU si zito,hata lishindwe kusikia.Mkono wake si mfupi hata ashindwe kuokoa.Pole sana kwa yaliyokukuta,naamini kwa Bwana YESU kila GOTI litapigwa kwa vitu vya Duniani na MBINGUNI.Najua ni hbr mbaya kwa wote wana jf kusikia walivyokutenda ila naamini baada ya kumaliza UCHUNGUZI wao watakurudisha.
 
yani ulivyoandika ni kama hujui whats next. Pole kwa kweli ila ndio hali halisi. Ngugi aliandika a grain of wheat. Yesu alikufa ili tupone. Nafaka huoza ili kuzaa zaidi. Chuo utarudi ila kama ulishiriki katika kuwa punje ya ngano, jua kuwa marekebisho yatafanyika chuoni kwa ghsrama ya nyinyi kuwa wahanga, jambo ambalo si baya. Cha msingi na wale waliobaki wasihofie kwa kashikashi mliyopata bali wawe na juhudi ya kuhakikisha kuwa kusimamishwa kwenu na wengine kufukuzwa ni njia ya kuwaandalia kilicho bora. Cha msingii zaidi ni madai yenu yawe yanapimika
 
Sikio la MUNGU si zito,hata lishindwe kusikia.Mkono wake si mfupi hata ashindwe kuokoa.Pole sana kwa yaliyokukuta,naamini kwa Bwana YESU kila GOTI litapigwa kwa vitu vya Duniani na MBINGUNI.Najua ni hbr mbaya kwa wote wana jf kusikia walivyokutenda ila naamini baada ya kumaliza UCHUNGUZI wao watakurudisha.

nashukuru kwa upendo wako mkuu. Ila hata nikirudishwa masomoni, itanifaa nini endapo wenzangu 98+41 hawatarudishwa, itanifaa nini endapo umma wa UDSM, ambako kulitakiwa kuwa kitovu cha mafikara, utaendelea kugandamizwa kimawazo na watawala wetu wakishirikiana na wakuu wa vyuo?
Nadhani ipo jinsi mkuu, zaidi ya kutegemea huruma ya MUUMBA.
 
pole sana mapinduzi ni magumu sana hasa kuwaangaikia watu wasiojua umuhimu wakile mnachokihitaji..
 
pole sanat. Utarudi cio mda mrefu. Na hao wanafiki na wazandiki walaaniwe kwa mambo yao haya ambayo enzi za udikteta ndio yalikuwepo. Lakini wajue. TRUETH NEVER DIE
 
I have a suggestion.....have you considered a COURT IN JUNCTION to over rule the university decision pending fair discharge of justice?
 
Kwema wanajamvi?
Kama kichwa kinavyojieleza, nilipokea ujumbe kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi saa 3 hivi asubuhi, ikinitaarifu kuwa nisubiri chumbani kwangu niletewe barua yangu. Karibu saa 7 hivi, baada ya kusubiri sana uvumilivu ukaniisha, nikaenda Nyerere Campus, nikapata barua yangu pale Auxilliary Police, iliyoeleza, nanukuu, "RE: SUSPENSION FROM STUDIES PENDING INVESTIGATION
Be informed that following your participation in the making of an illegal USRC desicion to defy Council orders, you have been suspended from studies pending futher investigation...", mwisho wa kunukuu. Nikakabidhi kitambulisho cha chuo kwa askari, tukaonana na viongozi wenzangu wa DARUSO, tukafarijiana na kuelekezana cha kufanya wakati huu mgumu.
Saa 11 jioni nikawa Mabibo Hostel kufanya taratibu zote za kuondoka chuoni, saa 11:30 hivi nikaondoka maeneo ya hostel kurudi nyumbani, ninakoishi.
Hii ni ID mpya, anayehitaji taarifa zaidi ani-PM.

usihofu baada ya week moja watawarudisha lengo ni kupunguza Tension iliyoko sasa. ni week ya ngapi sasa kwenye semister hii?
 
Pole sana,jitahidini kupata court injunction angalau mfanye mitihani next week! Mungu awape nguvu,tupo pamoja.
 
yeah mkuu.
Hatuna umoja kabisa, mwanzo DARUSO ilinyimwa vikao vya bunge lake, raia wakasema hawana wawakilishi. Juzi Jumamosi tukapata kikao halali, tukapitisha maazimio, ndio hayo yamezaa haya.

Pole sana Chief. Hivi hamjaangalia uwezekano wa kufungua mashtaka mahakamani. Kwa uwelewa wangu, hamuwezi kuwa na hatia kama nyie ni bunge halali la wanafunzi na mmetumia kikao halali kupitisha maazimio. Labda kama kuna mambo mengine mliyoyafanya baada ya hayo maazimio
 
Back
Top Bottom