Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,748
Nimepokea hivi karibuni voice note kutoka kwa Mtanzania anayeishi Afrika Kusini. Sauti hiyo ya Dudula Master ambaye ni mhamasishaju mkubwa wa Xhenophobia ametoa onyo dhidi ya wageni wote kuondoka Afrika ya Kusini kuanzia tarehe 02 Septemba 2022 hadi March 2023.
Nchi zetu hususan Tanzania zinapaswa kuhakikisha usalama kwa raia wao wanaoishi kule kihalali na ikiwezekana kuweka utaratibu wa kuwaondoa raia wake Afrika ya Kusini.
Matishio haya yamekuwa yakifanyika bila hatua zozote kuchukuliwa hivyo inawezekana baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola vya Afrika ya Kusini ni wahusika wa hizi operesheni dhidi ya wageni Afrika Kusini.
Hatulipi ubaya kwa ubaya bali kumtenga mtu mbaya ni sehemu ya kumpa fundisho dhidi ya mtenda ubaya. Ni wakagi sasa wa nchi za SADC kuitenga Afrika ya Kusini na ikiwezekana Umoja wa Africa (AU) kuiwekea vikwazo Afrika Kusini mpaka watakapoondoa vitisho dhidi ya usalama wa wageni ndani ya nchi hiyo.
Nchi zetu hususan Tanzania zinapaswa kuhakikisha usalama kwa raia wao wanaoishi kule kihalali na ikiwezekana kuweka utaratibu wa kuwaondoa raia wake Afrika ya Kusini.
Matishio haya yamekuwa yakifanyika bila hatua zozote kuchukuliwa hivyo inawezekana baadhi ya watumishi wa vyombo vya dola vya Afrika ya Kusini ni wahusika wa hizi operesheni dhidi ya wageni Afrika Kusini.
Hatulipi ubaya kwa ubaya bali kumtenga mtu mbaya ni sehemu ya kumpa fundisho dhidi ya mtenda ubaya. Ni wakagi sasa wa nchi za SADC kuitenga Afrika ya Kusini na ikiwezekana Umoja wa Africa (AU) kuiwekea vikwazo Afrika Kusini mpaka watakapoondoa vitisho dhidi ya usalama wa wageni ndani ya nchi hiyo.