GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Ingawa Afrika Kusini ni mojawapo ya nchi zilizoendelea duniani, inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa usalama. Mara kadhaa kumesharipotiwa na vyombo vya habari juu ya matukio ya kihalifu katika majiji makubwa kama Johannesburg, n.k.
Sina uhakika kama matatizo kama hayo yalikuwepo pia kipindi cha utawala wa Wazungu. Hisia zangu zinanishawishi kuamini kuwa hata kama changamoto za kiulinzi zilikuwepo, si kwa kiwango kama cha sasa.
Kwa kuwa hali ya mahali hutoa taswira ya aina ya uongozi uliopo, hakuna namna itakosekana kuuhusisha utawala wa sasa ambao kimsingi ni wa weusi, na hali hiyo. Pengine, utawala uliopo umeshindwa kukabiliana ipasavyo na hiyo changamoto.
Unafikiri, Makaburu wangerudishiwa usukani wa utawala wa South Africa kungeweza kuleta mabadiliko chanya kiuchumi, kisiasa na kiusalama?
Sina uhakika kama matatizo kama hayo yalikuwepo pia kipindi cha utawala wa Wazungu. Hisia zangu zinanishawishi kuamini kuwa hata kama changamoto za kiulinzi zilikuwepo, si kwa kiwango kama cha sasa.
Kwa kuwa hali ya mahali hutoa taswira ya aina ya uongozi uliopo, hakuna namna itakosekana kuuhusisha utawala wa sasa ambao kimsingi ni wa weusi, na hali hiyo. Pengine, utawala uliopo umeshindwa kukabiliana ipasavyo na hiyo changamoto.
Unafikiri, Makaburu wangerudishiwa usukani wa utawala wa South Africa kungeweza kuleta mabadiliko chanya kiuchumi, kisiasa na kiusalama?